CUF: Yauona Ugaidi Zanzibar

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
JOTO la kisiasa visiwani Zanzibar halijapoa na sasa Chama cha Wananchi (CUF) kinakuja na tamko zito hivi karibuni, anaandika Michael Sarungi

Chama hicho kinaeleza kuwa, maisha ya dhiki, wasiwasi, mashaka na unyama uliokithiri katika baadhi ya nchi zinazotawaliwa na ugaidi duniani yanatokana na watawala kudhani kwamba wao ni sehemu ya familia ya Mungu.

Magdalena Sakaya, Naibu Katibu Mkuu wa CUF-Bara ameueleza mtandao huu kuwa, nchi za Nigeria, Somalia na nyingine Afrika zimetawaliwa na vitendo vya kigaidi kutokana na serikali zao kudhulumu wananchi wao jambo ambalo limewapa mwanya magaidi kupata wafuasi.

“Hata haya matukio mengi ya kigaidi tunayoyashuhudia katika nchi kama Nigeria, Somalia na kwingine ni matokeo ya watawala kudharau matakwa ya wananchi kwa kudhani kuwa, wao ndio wenye maamuzi dhidi ya maisha yao ya kila siku,” anasema na kuongeza, matakwa ya Wazanzibari yamepuuzwa.

Amesema, demokrasia ni utawala wa watu, uliowekwa na watu na kwa ajili ya watu tofauti na hapo ni udikteta uchwara.

Amesema pamoja na Tanzania kuridhia mikataba mingi ya Umoja wa mataifa juu ya amani, lakini imekuwa bingwa wa kuikanyaga.

“Demokrasia maana yake ni utawala wa watu, uliowekwa na watu kwa ajili ya watu, kinyume cha hapo ni udikteta unaolenga kulinda maslahi ya watu wachache,” amesema Sakaya.

Amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizo na amani kwa kipindi kirefu na kuwa, tuendako huenda mambo yakawa tofauti.

“Hapa nchini kuna watu wanadhani wana ukoo na Mungu kwa kudhani kuwa Tanzania haiwezi kutawalika bila yao, huko ni kujidanganya, ipo siku ukweli utajitenga na uongo,” amesema Sakaya.

Amesema, wanatarajia kukutana kama chama na kutoa msimamo mzito juu ya ukandamizaji wa haki za wananchi uliofanyika visiwani Zanzibar ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanaCUF kubambikiwa kesi, kuswekwa rumande bila sababu.

“Tunatarajia kukutana kama chama na kutoa maamuzi mazito juu ya mstakabali wa Zanzibar na Tanzania nzima kwa ujumla,” amesema Sakaya.

Amesema viongozi wengi wa kisiasa kwa sasa wanaotanguliza maslahi binafsi badala ya wananchi “na ndio maana dunia nzima imeshuhudia sauti ya wengi ikikataliwa visiwani Zanzibar.”
 
Kwahiyo turuhusu utawala wa sharia za Kiislam Zanzibar ili kuepusha matatizo kama yanayojitokeza Somalia na Northern Nigeria . Nyani kasoro mkia mnajiandikia tu pumba bila kufanya uchambuzi wa kina unatoa mifano ya Somalia na Nigeria kwa Zanzibar. Huu ni upuuzi.
 
Kila kilichokuwa na mwanzo ni lazima ipo siku kitakuwa na mwisho.

Kwa CCM kuamini kuwa ni wao pekee waliopewa hati miliki na Mwenyezi Mungu ya kuitawala nchi hii hadi mwisho wa dunia ni kujidanganya kupita kiasi.

Hebu CCM wajiulize tu kidogo, hivi iko wapi KANU ya Kenya?

Wajiulize pia iko wapi UNIP iliyoasisiwa na Kaunda kule Zambia?

Wajiulize pia iko wapi Malawi Congress Party ya kule Malawi?

Vyama vyote hivyo vikongwe katika nchi zinatuzunguka, tayari vishakwenda 'kuudongo'

Sasa kama Vyama vyote hivyo vimeshatoweka katika ulimwengu wa siasa, sasa ni kitu gani kinachowaamisha CCM na kudhani kuwa wataendelea kutawala nchi hii milele na milele?
 
Sasa wao si walisusia uchaguzi. Zama za kubembelezana zimekwisha wamevuna walichopanda.
 
Tegemeo pekee walilobaki nalo CCM la kuendelea kuitawala nchi hii ni kwa kutumia vyombo vya dola.

Ikitokea siku vyombo vya dola vikapata 'ufahamu' na kuamua kutojiegemeza kwenye upande wa chama tawala, ndiyo utakuwa mwisho wa chama hicho.

Kwa kuwa CCM bila kutegemea 'mbeleko' ya vyombo vya dola, ni wepesi kuliko ubua!
 
Kila kilichokuwa na mwanzo ni lazima ipo siku kitakuwa na mwisho.

Kwa CCM kuamini kuwa ni wao pekee waliopewa hati miliki na Mwenyezi Mungu ya kuitawala nchi hii hadi mwisho wa dunia ni kujidanganya kupita kiasi.

Hebu CCM wajiulize tu kidogo, hivi iko wapi KANU ya Kenya?

Wajiulize pia iko wapi UNIP iliyoasisiwa na Kaunda kule Zambia?

Wajiulize pia iko wapi Malawi Congress Party ya kule Malawi?

Vyama vyote hivyo vikongwe katika nchi zinatuzunguka, tayari vishakwenda 'kuudongo'

Sasa kama Vyama vyote hivyo vimeshatoweka katika ulimwengu wa siasa, sasa ni kitu gani kinachowaamisha CCM na kudhani kuwa wataendelea kutawala nchi hii milele na milele?
Hata CUF ilikuwa na mwanzo na mwisho wake umeshafika!
 
Kamuzu Banda Rais wa maisha yuko wapi?

Yuko wapi Gaddafi? Yuko wapi Iddi Amin dadaa?

Viko wapi vyama vikongwe?

Ku wapi kuringa kwako ewe uelekeaye kuzimu?

Iko wapi Roman empire? Yu wapi Nebkadneza?

Tatizo la nchi hii tuna wafu!!! Hawajifunzi chochote na hawafikirii chochote....

IPO SAA na dakika itakaposemwa sasa imetosha!!! Utakapochorwa mstari.... Laana na balaa itaandikwa ktk vizazi vya wazalimu wa sasa....

Muda si mrefu usiku utakwisha....

PAMBAZUKO KUU li karibu.
 
VITISHO VYA NYAU...WAMESHATOA TAMKO NA VITISHO VINGI HAKUNA UTENDAJI.NDYO MANA WENZAO CCM WANAWAZARAU NAKUFANYA WANACHOTAKA WAO
 
Sasa wao si walisusia uchaguzi. Zama za kubembelezana zimekwisha wamevuna walichopanda.

Wenye akili walijua hakuna uchaguzi Bali njia ya kutangaza CCM ameshinda kwa kishindo.Kura za watu 58175 ndizo nimeamua kurudisha CCM madarakani.Kwa kiongozi makini lazima angaejiuliza mata tatu tatu je ni halali walichokifanya??

Kama CUF wangekubali kuingia kwenye uchaguzi, tungekuwa tuna sema mengine. kila kitu kulikuwa kinajionyesha.
 
Kwahiyo turuhusu utawala wa sharia za Kiislam Zanzibar ili kuepusha matatizo kama yanayojitokeza Somalia na Northern Nigeria . Nyani kasoro mkia mnajiandikia tu pumba bila kufanya uchambuzi wa kina unatoa mifano ya Somalia na Nigeria kwa Zanzibar. Huu ni upuuzi.
Nenda kaombewe wewe sawa
 
Kamuzu Banda Rais wa maisha yuko wapi?

Yuko wapi Gaddafi? Yuko wapi Iddi Amin dadaa?

Viko wapi vyama vikongwe?

Ku wapi kuringa kwako ewe uelekeaye kuzimu?

Iko wapi Roman empire? Yu wapi Nebkadneza?

Tatizo la nchi hii tuna wafu!!! Hawajifunzi chochote na hawafikirii chochote....

IPO SAA na dakika itakaposemwa sasa imetosha!!! Utakapochorwa mstari.... Laana na balaa itaandikwa ktk vizazi vya wazalimu wa sasa....

Muda si mrefu usiku utakwisha....

PAMBAZUKO KUU li karibu.

Haya si maneno mepesi mkuu.
 
Nchi hii inaongozwa na Mungu mwenyewe ndio maana bado tuna amani ingawa kuna wanasiasa wachache kama akina SAKAYA wanalala na kuamka wakiomba nchi iingie kwenye machafuko.

Mwenzenu natamani sana maneno tunayoongea yasiwe na element yeyote ya uchochezi.

Mkitamani ugaidi uingie Tanzania utaingia lakini tambueni hata ninyi wanasiasa mtaathirika tu.

Ushauri wangu epukeni sana maneno ya uchochezi. Watanzania wanapenda sana maendeleo fanyeni kila mnaloweza ili kuisimamia serikali ili iweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi na sio kutafuta wawaunge mkono mnapong'ang'ania kutafuta madaraka.

Mimi napenda sana amani sijui wenzangu. Wana siasa acheni kuutafuta umaarufu ndani ya mitandao ya kijamii sisi tunataka maendeleo.
 
Kwahiyo turuhusu utawala wa sharia za Kiislam Zanzibar ili kuepusha matatizo kama yanayojitokeza Somalia na Northern Nigeria . Nyani kasoro mkia mnajiandikia tu pumba bila kufanya uchambuzi wa kina unatoa mifano ya Somalia na Nigeria kwa Zanzibar. Huu ni upuuzi.
Tanua ubongo kabla ujapanua mdomo
 
Nchi hii inaongozwa na Mungu mwenyewe ndio maana bado tuna amani ingawa kuna wanasiasa wachache kama akina SAKAYA wanalala na kuamka wakiomba nchi iingie kwenye machafuko.

Mwenzenu natamani sana maneno tunayoongea yasiwe na element yeyote ya uchochezi.

Mkitamani ugaidi uingie Tanzania utaingia lakini tambueni hata ninyi wanasiasa mtaathirika tu.

Ushauri wangu epukeni sana maneno ya uchochezi. Watanzania wanapenda sana maendeleo fanyeni kila mnaloweza ili kuisimamia serikali ili iweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi na sio kutafuta wawaunge mkono mnapong'ang'ania kutafuta madaraka.

Mimi napenda sana amani sijui wenzangu. Wana siasa acheni kuutafuta umaarufu ndani ya mitandao ya kijamii sisi tunataka maendeleo.
Soma thread uwelewe usikurupuke
 
Hata CUF ilikuwa na mwanzo na mwisho wake umeshafika!
Hivi kwa mawazo yenu wanaccm mlifikiri kwa 'kumuamuru' Jecha aufute ule uchaguzi wa tarehe 25/10/2015 uliokuwa huru na haki ndiyo mtakuwa mmeiua CUF?

Kwa mawazo hayo mtakuwa mnajidanganya kupita kiasi, kwa kuwa badala ya CUF kudhoofika, ndiyo mmeipaisha mno na hivi sasa chama hicho ndiyo kimekuwa more stronger.
 
Back
Top Bottom