EL+RA=UFISADI
Member
- Jul 4, 2010
- 56
- 6
CUF yaomba fedha za kampeni kwa mafisadi?
Kuna tetesi kuwa Mbunge wa kuteuliwa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Ismail Jussa, wiki hii amekutana na mtuhumiwa mkubwa wa ufisadi hapa Tanzania, Yusuf Manji, kwa lengo la kukiombea CUF msaada wa pesa kwa ajili ya kampeni zinazoendelea za uchaguzi mkuu.
Manji ni mmiliki wa kampuni ya Quality Group Limited inayohusishwa na ukwepaji mkubwa wa kodi za serikali na ufisadi wa pesa za umma kupitia mifuko ya pensheni ya umma NSSF na PSPF.
Jussa ameonekana akiwa na mazungumzo na Manji Kempinski Hotel na haikuweza kufahamika mara moja nini hatma ya mazungumzo haya.
Ni kawaida kwa vyama vya siasa nchini kuomba msaada wa pesa kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa.
Tajiri wa Kihindi, Mzee Sabodo (ambaye hana tuhuma zozote za ufisadi), tayari ametoa 200 million/- kwa CCM na 100m/- kwa CHADEMA kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
Chama cha upinzani kama CUF kinapopewa pesa na watuhumiwa wakubwa wa ufisadi kama Manji, Rostam Aziz, Subhash Patel na wengineo kweli ni jambo jema?
Tunaijua CCM ndiyo siku zote iko karibu na mafisadi na imekuwa ikipokea pesa nyingi kutoka kwao. Sasa inapofika hatua ambayo hata chama cha upinzani kama CUF kinaomba msaada wa fedha kwa mafisadi ujue kuwa taifa hili la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kweli limeuzwa.
Huyu Jussa, ambaye ni msaidizi wa karibu wa Maalim Seif Shariff Hamad kule Zanzibar, anajulikana kuwa na rafiki wa karibu wa Rostam Aziz.
Wengine wamediriki kusema kuwa Rostam ndiye alisaidia kumshauri swahiba wake, Rais aliyemaliza muda wake, Jakaya Kikwete, amteuwe Jussa kuwa mbunge.
Kuna taarifa za muda mrefu sana kuwa Rostam Aziz amekuwa akitoa msaada kwa CUF tangu zamani kupitia kwa Jussa.
HII NDIYO NCHI YETU NA HAWA NDIYO VIONGOZI WETU!
Kuna tetesi kuwa Mbunge wa kuteuliwa wa Chama Cha Wananchi (CUF), Ismail Jussa, wiki hii amekutana na mtuhumiwa mkubwa wa ufisadi hapa Tanzania, Yusuf Manji, kwa lengo la kukiombea CUF msaada wa pesa kwa ajili ya kampeni zinazoendelea za uchaguzi mkuu.
Manji ni mmiliki wa kampuni ya Quality Group Limited inayohusishwa na ukwepaji mkubwa wa kodi za serikali na ufisadi wa pesa za umma kupitia mifuko ya pensheni ya umma NSSF na PSPF.
Jussa ameonekana akiwa na mazungumzo na Manji Kempinski Hotel na haikuweza kufahamika mara moja nini hatma ya mazungumzo haya.
Ni kawaida kwa vyama vya siasa nchini kuomba msaada wa pesa kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa.
Tajiri wa Kihindi, Mzee Sabodo (ambaye hana tuhuma zozote za ufisadi), tayari ametoa 200 million/- kwa CCM na 100m/- kwa CHADEMA kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
Chama cha upinzani kama CUF kinapopewa pesa na watuhumiwa wakubwa wa ufisadi kama Manji, Rostam Aziz, Subhash Patel na wengineo kweli ni jambo jema?
Tunaijua CCM ndiyo siku zote iko karibu na mafisadi na imekuwa ikipokea pesa nyingi kutoka kwao. Sasa inapofika hatua ambayo hata chama cha upinzani kama CUF kinaomba msaada wa fedha kwa mafisadi ujue kuwa taifa hili la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kweli limeuzwa.
Huyu Jussa, ambaye ni msaidizi wa karibu wa Maalim Seif Shariff Hamad kule Zanzibar, anajulikana kuwa na rafiki wa karibu wa Rostam Aziz.
Wengine wamediriki kusema kuwa Rostam ndiye alisaidia kumshauri swahiba wake, Rais aliyemaliza muda wake, Jakaya Kikwete, amteuwe Jussa kuwa mbunge.
Kuna taarifa za muda mrefu sana kuwa Rostam Aziz amekuwa akitoa msaada kwa CUF tangu zamani kupitia kwa Jussa.
HII NDIYO NCHI YETU NA HAWA NDIYO VIONGOZI WETU!