CUF wapinga Uteuzi wa Prof. Muhongo

CUF wapinga Uteuzi wa Prof. Muhongo

Ujue kwenye hivi vyama kunamijitu mijinga sana hivi cuf wanamuunga mkono lowasa halafu wanampinga muhongo jamaa zero kweli.
 
"
Hawajitambui hao.ukiwauliza makosa ya muhongo ninini utaona watakavyojiumauma midomo. By the way wao siwalimchagua lowasa. Watulie tuli.

Muhongo ndiye waziri sahihi wa ile wizara ama wengine ni wababaishaji.

Yaani mtu yeyote wa ukawa au aliyekuwa shabiki anayeweza kumnyoshea kidole muhongo basi huyo mtu mtindio wake wa ubongo haupo sawa kwani anamjua lowasa ni nani lakini alimshabikia na kumuona kuwa anafaa kuwa rais wake na hakuona kama hilo ni tatizo sasa leo anaibuka na Mzalendo anayepinga wababaishaji

"Mtindio wake wa ubongo hauko sasa"
Jifunze kiswahili ulichoandika Ni utumbo mtupu
 
Prof. Muhongo ni mmoja kati ya viongozi bora kabisa, mwacheni achape kazi. Aliyemteua anamwani na yeye ndiye atakayetoa hesabu kwa wananchi. JPM ana mkataba na Watanzania, endapo hatatekeleza majukumu ya kutufanyia kazi tutamhukumu mwaka 2020.
 
na kwa bahati nzuri JPM amejipambanua vema kabisa, kwamba mkataba wake na serikali yake ni miaka mitano, ili atekeleze ilani ya chama cha ccm pia na mambo aloyaahidi kuwafanyia watz, kwa msingi huo ni lazima achague watu ambao watatekeleza kasi yake na si jukumu lako ww kumpagia nani afanye nae kazi kwa kipindi hicho, kazi yako ss ni kisubiri ulichoahidiwa kama utatekelezewa kwa kipindi hicho au la.
 
Badala ya kung'ang'ana Dk Shein awaachie madaraka ya kuitawala Zanzibar kufuatia ushindi mlioupata ktk uchaguzi mkuu uliopita mnang'ang'ana na mambo ya Muhongo asiyewahusu. Sijui nyie ngisi tuwaeleweje?

Ndio maana kwa ujinga wenu mlimsapoti fisadi 'numero um' Lowassa mkamtosa Lipumba m/kiti wenu.
 
haya nayo hayajielewagi

Wakati ule yanaambatana na CCM Chadomo walikuwa wanawaimbia "dada huyo ameolewa" leo wametulizwa na Chadomo basi kila la CCM wanahoji......yaani wanafanya kila bidii kuwaridhisha Chadomo.

....kaaazi kwelikweli....
 
Wasikose amani tayari baraza limeshatangazwa sheria zetu na katiba yetu vinafahamika kuhusu mamlaka ya rais
 
Badala ya kung'ang'ana Dk Shein awaachie madaraka ya kuitawala Zanzibar kufuatia ushindi mlioupata ktk uchaguzi mkuu uliopita mnang'ang'ana na mambo ya Muhongo asiyewahusu. Sijui nyie ngisi tuwaeleweje?

Ndio maana kwa ujinga wenu mlimsapoti fisadi 'numero um' Lowassa mkamtosa Lipumba m/kiti wenu.

Wewe FUNZA katu huwezi kuwaaelewa NGISI faida waliyoipata pale walipomtosa Pr Lipumba na kumsapoti huyo unaemwita fisadi Lowassa.

Moja wapo ya faida ambayo NGISI waliipata kwa kitendo chao hicho ni kuwazuia MAFUNZA ya CCM kusahau mikakati yao waliyoizowea ya wizi wanayoifanya wakati wa uchaguzi mkuu Zanzibar hivyo kupelekea NGISI kushinda kirahisi mno Zanzibar

Faida nyengine ambayo ngisi waliipata ni kuwazuia MAFUNZA ya CCM kufanya utaratibu wao waliouzowea wa kumwaga majeshi na mapolisi kama utitiri Zanzibar ili kuwarahisishia wao kufanya uharamia wao waliouzoea wa wizi wa KURA.

Hizi ni baadhi ya faida ambazo NGISI wa CUF walizipata pale walipoamua kumsapoti huyo unaemwita fisadi Lowassa, jee nikuulize wewe FUNZA hizi ni faida ndogo!?!? Usisahau ile ya kutoka viti viwili hadi viti kumi vya ubunge Tanganyika, bila kusahau halmashuri kadhaa.

SIKU ZOTE FUNZA HAWEZI KUMZIDI AKILI NGISI
 
Wajinga tu nyumbu namba moja.

Wajinga ni wale waliokuzaa ambao walishindwa kukufundisha adabu na maarifa ya kuvumilia au kukosoa mawazo ya wengine kwa njia za heshima maana katika maisha ya kila siku katu haitotokezea wote tukawa na mawazo sawa.
 
Wakati ule yanaambatana na CCM Chadomo walikuwa wanawaimbia "dada huyo ameolewa" leo wametulizwa na Chadomo basi kila la CCM wanahoji......yaani wanafanya kila bidii kuwaridhisha Chadomo.

....kaaazi kwelikweli....

Nyinyi wasengerema wa CCM hivi Mnadhani upinzani ni UADUI!!!!???? Wakati mwengine mnabidi mtumie akili kupambanua mambo na sio kukashifu kila wazo linalotolewa na wapinzani

Mfano mzuri ni hii hoja ya siku ya uhuru kabla ya magufuli kuingia madarakani na kuigeuza siku ya usafi tayari mawazo haya yalikwishatolewa bungeni na wapinzani kupitia mbunge wa CUF MHESHIMIWA MKIWA A. KIMWANGA ubunge wa viti maalum.

Msiwe wasengerema wa kupiga makofi tu bila ya kuchuja mambo kama wabunge wenu ambao Mh. Kikwete aliposema bungeni kuwa safari zake za nje ya nchi zinameleta tija kubwa ikiwemo kupata msaada wa vyandarua vya bure "wabunge wa CCM makofi PWA PWA PWA kufurahia""

Na juzi katika bunge Mh. Magufuli aliposema kukandia safari za kikwete pale aliposema "mtu anasafiri kwenda ulaya kuliko hata anavyosafiri kwenda kijijini kwake kuangalia wazee wake" wale wale wabunge wa CCM waliozifagilia kwa makofi safari za kikwete wakapiga tena makofi "PWA PWA PWA PWA" kuonesha Mh Magufuli aliyosema ni point.

Sasa nyinyi wasengerema manataka wote tuwe na akili hizi za kusifu hataka kama ni kibovu!!??

Mwisho utambue katika siasa hakuna adui wala rafiki wakudumu! Na pia siasa si uadui hivyo CUF walipoamua kushirikaana na CCM ilikuwa ni kwa maslahi yao CUF na sasa wanaposhirikiana na CHADEMA, NCCR NA NLD pia wamefanya hivyo kwa maslahi yao CUF.
 
Ukawa ebu jifunzeni kutunza kumbukumbu.Miezi miwili iliyopita mlikuwa mnamnadi mtu aliyejiuzuru Uwaziri Mkuu kwa kashfa ambayo hadi sasa madhara yake yanalitafuna Taifa,awe Rais wa JMT.Au ndio nyani halioni Ku......le?

Labda UKAWA Hawa Ni Wale Walosutwa Na Dhamira.
 
Ni lini CUF wamemtambua Rais Magufuli mpaka wanaanza kukosoa uteuzi wa Baraza lake la Mawaziri?

Hizi siasa za kinafiki na kilaghai hazitakiwi nchini.

Matokeo Ya Urais Bongo Hayapingwi Mahakamani, Hvyo Matakwa Ya Sheria Yanawafanya Wakubali Urais Wake Hawana Namna.
 
Lowasa alijiuzulu Uwazi mkuu na hakuwa anagombea cheo hicho tena bali Urais, Mwinyi alijiuzulu Uwaziri wa mambo ya ndani na alivyorudi hakugombea hiyo nafasi bali Urais. Huyu Muhongo alijiuzulu Uwaziri wa Nishati na Madini na karudi nafasi hiyo tena na ndiyo maana watu wanalalanika. Angepewa Kilimo au nyingine tofauti na aliyojiuzulu watu wasingelalamika.
Hizi ni akili za sisimizi!!
 
Yani hizi ndio siasa za majitaka kabisa, muda wote walikaa kimya kama wamemwagiwa maji, wakijifariji kuwa eti Magufuli alikuwa anatekeleza sera za UKAWA,ameteuliwa Nape, Muhongo tayari nongwa zimeanza !! hizo si ndio sera za UKAWA kaeni kimya.alafu mbona nyie wakati mnamchagua Lowasa kuwa mgombea wenu hakuna aliyewagusa kwani nyie ni nani hasa eh? nyie muwe na haki ya kumteua mtuhumiwa wa Richmond wengine hawana haki ya kuteua watuhumiwa wa Escrow!

Ninasubiri Kuona Kama Kuna Atakaesutwa Na Dhamira Kwenye CCM Kama Utakuwa Umelinganisha Vitu Sawa!
 
Usafi wa Lowasa na uchafu wa Muhongo just thinking loud uyu alipita kama Waziri mwengine kama raisi.
Let's be fair to all at all times
 
JUMUIYA ya Vijana wa Chama cha Wananchi (CUF) imesema wanasikitishwa na uteuzi wa baraza la mawaziri lililotajwa juzi na Rais John Magufuli na kudai kuwa, katika baraza hilo wamerudishwa wale mawaziri waliokumbwa na kashfa za ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.

Pia imesema katika baraza hilo hakuna uteuzi ambao umewiana hasa katika suala la usawa wa kijinsia na wala haukuzingataia Muungano uliokuwepo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Hamidu Bobali amesema wanashangaa kuwaona aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Sospeter Muhongo na aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Harson Mwakyembe kuwepo tena.

Amesema, Waziri Muhongo alikuwa anatuhumiwa na suala la Escrow na akajiuzulu halafu Magufuli amemrudisha tena kitu ambacho kinawakosesha amani.

Inatusikitisha sana kitendo cha Rais wetu kumteua tena Waziri Muhongo kurudi tena wizarani hapo wakati alikuwa na kashfa kubwa ya escrow lakini amerudishwa tena inaonyesha Magufuli pia pamoja na kusifiwa juu ya utendaji wake hayuko makini,?amesema Bobali.

Pamoja na Muhongo pia Waziri Mwakyembe alikuwa katika wizara ambayo sasa hivi inakubwa na matatizo makubwa ya kupitisha makontena na wakati alikuwa waziri katika wizara hiyo, hilo lilitosha kwa Magufuli kufanya upembuzi wa Mawaziri. Hao wote hawakufaa tena kuridi kuwa mawaziri,? amesema.

Ameongeza kuwa, wanasikitishwa sana kwani ile kasi ambayo Magufuli alianza nayo wanaiona inakufa siku si nyingi kwa kuwarudia tena mawaziri hao mizigo.

Wananchi tunasikitika sana kwa kuwa tulimuamini Rais Magufuli lakini imani hiyo inakaribia kukatika kutokana na kurudishwa kwa mawaziri hawa na kusababisha kasi kupungua,?ameeleza

Aidha aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Sospeter Muhongo hakuwahi kupatikana na hiyo ya Escrow kwani alijiuzulu mwenyewe. Kwa kuhofia kupatikana na hatia.

Kwa upande mwingine Mwenyekiti huyo alizungumzia mgogoro uliokuwepo Zanzibar na kusema kuwa Baraza la vijana wa chama hicho kwa kushirikiana na vyama vinavyunda Umoja wa Katiba Wananchi (Ukawa) wameandaa mkutano juu ya kuzungumzia mgogoro huo.

Tunafurahishwa na mazungumzo yanayoendelea kati ya viongozi kwetu wa huko Zanzibar lakini baraza letu limeandaa mkutano huo ili kuzungumzia suala hili,?amesema Bobali

Hata hivyo Bobali amesema wanamuomba Rais Magufuli kuliingilia kati suala la Zanzibar kwani kutokufikia kikomo kunasababisha mambo mengi kurudi nyuma ikiwa moja na uchumi kushuka.

Jumuiya ya vijana inawatahadharisha wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuacha mara moja kauli chafi na vitendo vya kichochezi vinavyofanywa na wanachama hao kwani vinaweza kuamsha hasira za vijana wa CUF Zanzibar,? amesema Bobali.

Ni kitu gani alichofanya Muhongo hadi asiteuliwe kuwa waziri?hao wazalendo uchwara wanaowatuma waambie wasome namba....hatuwezi kuweka rasilmali yetu rehani......Muhongo ni chaguo sahihi na wananchi wanatambua uwezo wake na hasara waliyopata baada ya wabunge wala rushwa kufanya jitihada za kumuondoa.
 
inaonekana prof.lipumba alipewa jibu la kukatisha tamaa na magufuli,
 
Back
Top Bottom