Nimeshtuka sana baada ya kuona habari tbc1 kuhusu harakati za vyama vya siasa kupoka jimbo la igunga kwenye uchaguzi mdogo ujao. CcM wanaita OPERESHENI TETEA IGUNGA, wakati Chadema ni OPERATION CHUKUA IGUNGA..cuf ndio wamewapoteza wote wenyewe wanaita OPERATION LOLOTE LIWALO IGUNGA..! ina maana cuf hawana cha kupoteza igunga?
<br />
<br />
Tumesikitishwa sana na propaganda hizi zinazoendeshwa na vyombo vya habari juu yetu.
Mimi naitwa mohammed mtutuma , msaidizi maalum wa naibu katibu CUF tanzania bara.
Kwa niaba ya mhe. Mtatiro naomba kueleza kwa uwazi kuwa hizo oparesheni zinazotangazwa ni za kutengenezwa,
Cuf haijatangaza oparesheni yoyote igunga au mahali kokote kule.
Oparesheni ya mwisho kutangazwa na cuf ni zinduka, hiyo oparesheni bora liende, au bora liwe au vyovyote vile inavyosema na za kutengenezwa tu.
Siku zote tumekuwa tukilalamika kuwa vyombo vya habari vinatuhujumu na kuna watu muhimu katika jamii wanatuhujumu na kila wakati kutaka tueleweke hasi kwa jamii.
Nasisitiza kuwa cuf haijazindua oparesheni yoyote igunga, siyo linda igunga , chagua igunga, tetea ingunga, kotekote igunga n.k.
Tunaomba wapenzi na wafuasi wetu na wananchi wote wapuuze propaganda hizi.
Cuf imejipanga kushinda uchaguzi wa igunga na kama tukizindua oparesheni itakuwa OPARESHENI CHAGUA MAHONA AONGOZE IGUNGA,
We have a strong party network in igunga, we have stable leaders in there, we have the best candidate of all parties. We have no reason not to win this seat.
MHD MTUTUMA,
MSAIDIZI MAALUM WA NKM-BARA,
CHAMA CHA WANANCHI CUF.