CUF ikifa CCM itapata faida gani?

CUF ikifa CCM itapata faida gani?

hazole1

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2015
Posts
4,319
Reaction score
3,919
Hakuna asiyejua kuwa CCM wanafanya kila linalowezekana na wanakesha usiku na mchana kuhakikisha CUF inakufa au UKAWA kwa ujumla na wanapoteza mamilioni ya wakati na pesa nyingi sana kwa ajili ya kuua upinzani.

Lakini mwisho wa siku sijui watakuja kuambulia nini. Hilo ndio swali ambalo najiuliza kila siku na sipati jibu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna asiyejua kuwa CCM wanafanya kila linalowezekana na wanakesha usiku na mchana kuhakikisha CUF inakufa au UKAWA kwa ujumla na wanapoteza mamilioni ya wakati na pesa nyingi sana kwa ajili ya kuua upinzani.

Lakini mwisho wa siku sijui watakuja kuambulia nini. Hilo ndio swali ambalo najiuliza kila siku na sipati jibu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Haya ni makosa katika namna ya kufikiri. Nadhani wao wanadhani wanaweza kuua upinzani wakati upinzani upo hata ndani yao wenyewe. Kama kuna jambo Magufuli anafeli basi ni vita alivyoanzisha dhidi ya wapinzani. vita hivi vitamgharimu sana.
 
Hakuna asiyejua kuwa CCM wanafanya kila linalowezekana na wanakesha usiku na mchana kuhakikisha CUF inakufa au UKAWA kwa ujumla na wanapoteza mamilioni ya wakati na pesa nyingi sana kwa ajili ya kuua upinzani.

Lakini mwisho wa siku sijui watakuja kuambulia nini. Hilo ndio swali ambalo najiuliza kila siku na sipati jibu.


Sent using Jamii Forums mobile app
kitatokea chama kimoja cha upinzani chenye nguvu kuluko UKAWa. bora wangeacha kama ilivyo ili angalau waisaivu tumiaka tutatu tulikobaki, hii kitu wananafanya wakidhani wameshinda itawagharimu
 
tujiulize kwanza ACT ikifa kama CHADEMA wanavyokesha wakiomba na kufanya kila aina ya fitna na majungu, chadema itapata faida gani?!!! kama ipo basi itakuwa ni sawa na ile ambayo ccm itaipata kwa kufa cuf.
 
Zanzibar, Zanzibar, shein atatawala kwa uhuru na amani.
 
kuitawala zanzibar kama koloni lao.
Ni kweli! CUF kimsingi ndo Zanzibar halisi au wazawa kama ni neno sahihi. CCM inafahamu fika CUF ikishika dola na Muungano ni kwisha. Why? Kwasababu, hakuna Rais wa Zanzibar ambaye anatokea CCM hajapikwa CCM na kubeba unafiki na ubabe wa CCM katika kuongoza. Shein ameishi bara, amekuwa makamu wa Rais na amepewa urais zanzibar kwa masharti ya kufanya kazi kwa kufuata maelekezo toka CCM Bara. CUF ikifa CCM watahakikiksha anayechukua Urais wa Zanzibar ni Mzanzbar mamluki na kuanzia hapo ni ubabe ubabe tuu!! Ndo maana nakuunga mkono, Zanzibar itakuwa koloni jumla.
 
Haya ni makosa katika namna ya kufikiri. Nadhani wao wanadhani wanaweza kuua upinzani wakati upinzani upo hata ndani yao wenyewe. Kama kuna jambo Magufuli anafeli basi ni vita alivyoanzisha dhidi ya wapinzani. vita hivi vitamgharimu sana.
Kati ya makosa makubwa ambayo CCM huwa wanajutia sana lakini hawataki kukiri ni kumuamini Karume kuchukua serikali Zanzibar. Yeye ndiye alileta muafaka ulioleta mwanga kwa upinzani kuichungulia ikulu na mantiki yake ni kwamba naye ni mmoja wa wanaharakati wa kudai Zanzibar huru. Kwahyo kukua kwa upinzani kulitokana na spport ya jamaa kwa upande mmoja. Namwona na bint wa Karume Fatma, naye anacheza mule mule. Yote anayofanya ni muakisio wa kile kilichoko ndani tu kuwa dola la bara linatunyanyasa. Na atakachotendewa chochote kile kitakuja siku moja kuunganishwa na anachotendewa Maalim na kitakuja kuwajumuisha wanzanzibar kama Taifa. Hapatatosha. Nafikiri uvumilivu ulitakiwa uwepo. Wangecheza hii ngoma taratibu waje wafanye figisu figisu huko 2019 lakini kukosa ustahimilivu wasishangae hiyo hiyo CUF wanayofikiri ni 'yao' kupitia Lipumba ikija kuwageuka huko 2020 na kuwa kitu kingine na inakuwa too late kulizima. Muda utaamua...
 
Kati ya makosa makubwa ambayo CCM huwa wanajutia sana lakini hawataki kukiri ni kumuamini Karume kuchukua serikali Zanzibar. Yeye ndiye alileta muafaka ulioleta mwanga kwa upinzani kuichungulia ikulu na mantiki yake ni kwamba naye ni mmoja wa wanaharakati wa kudai Zanzibar huru. Kwahyo kukua kwa upinzani kulitokana na spport ya jamaa kwa upande mmoja

Analysis yako haiko katika reality. Tatizo kuu CCM Zanzibar imekataliwa from day one, haijawahi kushinda uchaguzi tokea 1995, kinachotokea ni Tanganyika kutumia mabavu, si suala la whether Amani kaleta muafaka au Fatma kasema nini. Hao kina Shein na wengine wote ni mateka , hawani hiyari, huo ndio ukweli.

Mbunge huyo ni wa CCM, kabla hawajatishwa, hata bunge la katiba, walikuwa na msimamo wa Znz bila kujali vyama, mambo yalivurugika baada ya kutishwa.
 
kimsingi ndo Zanzibar halisi au wazawa kama ni neno sahihi. CCM inafahamu fika CUF ikishika dola na Muungano ni kwisha
Cuf na Wazanzibari walio wengi hawapingi muungan, wanachotaka ni muungano wa haki, sio wa mwenye maguvu kumuonea dhaifu.
 
Absence of democracy gives rise to militancy. Sisemi mimi, historical truth. CCM tread carefully.
 
Hakuna asiyejua kuwa CCM wanafanya kila linalowezekana na wanakesha usiku na mchana kuhakikisha CUF inakufa au UKAWA kwa ujumla na wanapoteza mamilioni ya wakati na pesa nyingi sana kwa ajili ya kuua upinzani.

Lakini mwisho wa siku sijui watakuja kuambulia nini. Hilo ndio swali ambalo najiuliza kila siku na sipati jibu.


Sent using Jamii Forums mobile app
madai ya cuf ya 2015 yatakufa tutapumuwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ni hivi kuna mtu anawaza kuwa anaweza kuua upinzani kwahiyo anatumia mapesa na ngvu kuua upinzani ...mara madiwani mara cuf lakini sisi wengine hata tukatwe shingo hatuikubali ccm neverrrrrrrrrr
 
Kwani shetani anapomwaribu binadamu hadi kuangukia dhambini anafaidi nini? si anaona anamkomoa Mola wetu? the same apply.
 
Huu uzushi una wiki sasa ila aliyeuleta ndio anauchangiachangia sasa amefikisha post 13
 
Chadema wanataka cuf ife self ahamie kwao ccm wanataka cuf ife ili ukawa ikose nguvu

Swali la kujiuliza

Je hivi vyama viwili vinanufaika vipi na mgogoro wa cuf
 
Hakuna asiyejua kuwa CCM wanafanya kila linalowezekana na wanakesha usiku na mchana kuhakikisha CUF inakufa au UKAWA kwa ujumla na wanapoteza mamilioni ya wakati na pesa nyingi sana kwa ajili ya kuua upinzani.

Lakini mwisho wa siku sijui watakuja kuambulia nini. Hilo ndio swali ambalo najiuliza kila siku na sipati jibu.


Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mimi sikubaliani na hoja yako kwa sababu zifuatazo
1-unataka kuaminisha watanzania kwamba ccm ilimtuma Lipumba ajiuzulu?
1
2-Unataka kuaminisha watanzania kwamba maalim seif kutoitisha mkutano wa baraza kuu alitumwa na ccm?
3-Wanasheria wa cuf walikuwa wapi kumshauri katibu mkuu juu ya athari ya kutoitisha mkutano kujadili barua ya kujiuzulu ya Lipumba?
4-Katiba ya cuf ilitungwa na ccm?
5-Cuf hawana vyombo vyombo vya kuelezea mchakato wa kumaliza migogoro?
6-Chadema kuanzisha operation toa msikiti buguruni walitumwa na ccm?
Mbona vitu vingine viko wazi mno kuliko kusingizia ccm kwa makosa dhahiri ya vyama usika.
 
Back
Top Bottom