Crisis leads to Chaos: Udanganyifu kozi za Ualimu

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Wengi wenu inawezekana mmeliona hili au hamkuliona na kulipa umaana na umakini.

Lakini nimeguswa sana na kuhuzunika kuona jinsi Mtanzania anavyoendelea kuhangaika na kutafuta kila mbinu kujipatia kipato.

Mtakayosoma hapa chini, si ya kupuuza au kufikiria kuwa ni suala la "ukihiyo" au elimu feki, mlipokee kama kiu ya wananchi kujiendeleza na wanashindwa kuona tumaini kutokana na mfumo mbovu wa elimu, mfumo uliozorota wa uchumi na uongozi.

Ikiwa karibu nusu ya wanachuo hiki walikuwa wamefoji vyeti, wametumia majina bandia ili wapate nafasi kwenda shule, je tunajiambia nini kama Taifa? je tumekaa chini na kujihoji kujua tatizo letu ni nini?

Je serikali ilipobaini yaliyotokea kupitia Baraza la Mitihani, imechukua hatua gani kutafuta ufumbuzi wa kudumu?

Nukuu kutoka gazeti la Majira:
 
...yaani, mtu unakosa hata pakuanzia. ingelikuwa nyumba, yaani mtu unabomoa yote na kuanza kujenga tofali moja baada ya jingine mpaka ujenzi unakamilika.

...kila kitu shaghalabagala tu, please bring on some good news for once! Grrrrrrrr
 
Kila kona uozo. Hii inatuonyesha kwa mara ingine tena umuhimu wa uongozi makini. Watanzania tunacheza na maisha yetu na uhai wa nchi yetu tunapoendelea kucheza na uongozi wa nchi kwa kuwachekea hawa CCM, ni hatari tena sio kidogo
 
...yaani, mtu unakosa hata pakuanzia. ingelikuwa nyumba, yaani mtu unabomoa yote na kuanza kujenga tofali moja baada ya jingine mpaka ujenzi unakamilika.

...kila kitu shaghalabagala tu, please bring on some good news for once! Grrrrrrrr

Inawezekana kuanza upya hata katika siasa; ni kubadilisha mfumo kwa maana ya kuanza upya na chama kingine kabisa. CCM wafanyeje ndio tujue kwamba ni waharibifu?
 
Truth of matter is that BAMITA na Serikali watachukulia hatua makosa yaliyotokea, lakini si chimbuko au mzizi wa makosa kutokoea.

Wanasema kinga ni bora kuliko matibabu, wao wanatafuta kinga kuzuia kufoji vyeti na si kujiuliza kwa nini watu wanafoji vyeti au kughushi nyaraka ili wapate kwenda vyuoni!
 
KUFOJI VYETI KUNAHUSIANA VIPI NA CCM AU CHADEMA?
ni swali tu..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…