CRDB SimBanking mnazingua

CRDB SimBanking mnazingua

Kijana Mzeeeh

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2015
Posts
295
Reaction score
324
Hivi hawa Jamaa huwa wanafanya kusudi kung'ang'ania vihela hela vyetu kila inapofika weekend au?

Maana, kwa uzoefu wangu, kila weekend unakuta SimBanking haifanyi kazi na ata ATM vilevile.

Mfano nimehangaika kuhamishia kihela changu tiGO pesa ili nifanye yangu; nimejaribu bila mafanikio kuanzia saa 6 hadi 8 usiku, nikaona nirudi kulala tu.

Na sio mara ya kwanza hiyo. Kuna weekend tena niko maeneo na Mbebez, salio likakata mfukoni nikamwambia "ngoja nitoe hela kwa wakala nje hapo". Bado sijasahau ile AIBU.

Hii Bank iheshimu haki yetu ya kutoa vihela vyetu muda wowote ule tunapo-vihitaji, sikufungua Fixed deposit mimi.
 
Dah.... Kama mambo yaliisha pita na Pesa yako ikabaki salama kwenye account yako hapo huoni Kama ni ushindi tayari?? Sasa Unaweza kutumia hiyo Pesa kwenye mambo ya "msingi"
 
Dah.... Kama mambo yaliisha pita na Pesa yako ikabaki salama kwenye account yako hapo huoni Kama ni ushindi tayari?? Sasa Unaweza kutumia hiyo Pesa kwenye mambo ya "msingi"
Sawa mwisho wa siku hela yangu imepona, lakini inakera sana.
 
Sawa mwisho wa siku hela yangu imepona, lakini inakera sana.
CRDB ni bank ya ovyo sana ATM zao nyingi hawaweki pesa na simbanking kuipata ni kwa bahati; naona kuna tatizo ambalo hatujalijua bado na huenda wanaelekea kufilisika
 
Nami leo nimesomeshwa namba baada ya kushindwa kabisa kuhamishia fedha kwenye simu!
 
Nami leo nimesomeshwa namba baada ya kushindwa kabisa kuhamishia fedha kwenye simu!
imenikuta mm asubuhi hii ilinibidi nirudi nyumbani nivunje kibubu changu cha mbao maana kuhamisha kwenye tigo pesa naambiwa subiri tu kwenye Atm network down ,ila huenda kweli kuna kitu sio kizuri wanatuandalia hawa viumbe.
 
Usiombe sasa kununua LUKU kwa CRDB SIMBANKING utajuta.
 
mkuu ela imepona shukuru mungu maana najua ulikua na yule Dem nilikuona nae jana
 
Na hata mikopo wamesitisha kutoa kwa muda sasa
 
Nliona tangazo walisema kutakuwa na system shutdown jana usiku mpaka leo asubuhi ya leo. Nahisi hukuzifikia hizo taarifa.
 
Nliona tangazo walisema kutakuwa na system shutdown jana usiku mpaka leo asubuhi ya leo. Nahisi hukuzifikia hizo taarifa.
Dah... Mbona wana namba zetu, email add hata id zetu za JF mbona hawakitujilisha?? Sema wameanza kulewa sasa
 
CRDB ni bank ya ovyo sana ATM zao nyingi hawaweki pesa na simbanking kuipata ni kwa bahati; naona kuna tatizo ambalo hatujalijua bado na huenda wanaelekea kufilisika
Natumia sana hii huduma lkn hivi sasa siitaki tena. Kuna mfanyakazi aliniambia kuwa hii huduma ya simbanking bado iko kwenye maharibio na niiepuke haraka sana, kuna kipindi pesa yangu imekaa siku 16 pasipo kujulikana kama imefika CRDB ama bado iko mpesa. Ukipiga CRDB Huduma kwa wateja wanakupokea, ukitoa maelezo yako wanakuambia subiri usikate simu ndo imetoka kwani hakuna atakayerudi kukujibu hadi simu inakata automatically. Ukipiga tena unaambiwa subiri usikate simu.........
 
Walisema wkend hasa leo watakua na matengenezo yao kuboresha huduma, niliona kwenye mwananchi la jana
 
Walisema wkend hasa leo watakua na matengenezo yao kuboresha huduma, niliona kwenye mwananchi la jana
Wangetuma ata SMS kama ambavyo huwa wanatuma katika ku-promote huduma zao tungefahamu mapema kuliko kuweka tangazo kwenye gazeti.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom