CRDB CRDB CRDB, Nawaita mara tatu!!

CRDB CRDB CRDB, Nawaita mara tatu!!

Sniper

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2008
Posts
2,008
Reaction score
949
Hii CRDB mnatutendea vibaya sana! 😡 Jana mmekata hela kutoka kwenye akaunti yangu bila idhini yangu. Hata mbaya zaidi, nimetuma hela kwenda M-Pesa na hazijafika wala kurudi tena kwenye akaunti yangu. Hii ni dharau kubwa kwa wateja wenu.

Hivi mnajua maisha yalivyo magumu huku chini? Kila senti tunayoitafuta ni kwa shida, halafu ninyi mnachezea jasho la watu namna hii? Tunawaamini muweke na kutunza fedha zetu salama, siyo kuzichezea kama mchezo wa kamari.

Tunauliza maswali na hatupati majibu. Hivi hii ndiyo huduma mnayosema ni ya “kibunifu na ya uhakika”? Sasa mtu akipotezewa hela hivi ataendelea kuwa na imani na benki kweli?

Mnatufanya tufikirie mara mbili kama kweli ni salama kuweka fedha zetu CRDB. Rudisheni hela zetu, na muache kuwakandamiza wananchi mnaotegemea ili muendelee kuwepo! 😡
 
Poleni sana "Thed weld dwellers" , hend to mouth, the 99% na wang'atwa na mbu.

Mimi wala siwezi kukutana na Huo upuuz nilipohifadh hela zangu JP Morgan, Goldman Sachs, Deutsche bank, Swiss credit, HSBC ma offshore huko Jersey, Panama, virgin islands Bahamas na Monaco.
 
Mafisadi yameingia hapo

Yapo kutakatisha pesa zao na kutafuta pesa za uchaguzi zile bilion 86 yalikuwa maigizo!

Binafsi juzi,Jana na leo nimefanikiwa kuhamisha pesa zangu zote crdb.

Ingawa wamelamba 300k yangu
 
Tangu Siku ya kwanza CRDB walipomuajiri Huyu! ?
👇
Niligundua userious kwenye mambo ya msingi /pesa za watu....umekwisha!

Na kweli Kimei kaondoka kwenda Bungeni na benki yake!👇👇
1000024239.jpg
 
hii benki siioni mbali, yaani tuliowaamini hatuwaoni nao wameingia mitini
 
Mafisadi yameingia hapo

Yapo kutakatisha pesa zao na kutafuta pesa za uchaguzi zile bilion 86 yalikuwa maigizo!

Binafsi juzi,Jana na leo nimefanikiwa kuhamisha pesa zangu zote crdb.

Ingawa wamelamba 300k yangu
you’re holding assets, move to cold storage ASAP and avoid unverified dApps.
 
Hii CRDB mnatutendea vibaya sana! 😡 Jana mmekata hela kutoka kwenye akaunti yangu bila idhini yangu. Hata mbaya zaidi, nimetuma hela kwenda M-Pesa na hazijafika wala kurudi tena kwenye akaunti yangu. Hii ni dharau kubwa kwa wateja wenu.

Hivi mnajua maisha yalivyo magumu huku chini? Kila senti tunayoitafuta ni kwa shida, halafu ninyi mnachezea jasho la watu namna hii? Tunawaamini muweke na kutunza fedha zetu salama, siyo kuzichezea kama mchezo wa kamari.

Tunauliza maswali na hatupati majibu. Hivi hii ndiyo huduma mnayosema ni ya “kibunifu na ya uhakika”? Sasa mtu akipotezewa hela hivi ataendelea kuwa na imani na benki kweli?

Mnatufanya tufikirie mara mbili kama kweli ni salama kuweka fedha zetu CRDB. Rudisheni hela zetu, na muache kuwakandamiza wananchi mnaotegemea ili muendelee kuwepo! 😡
Poleni sana, bila shaka kwa hali hii watakuja kubadilisha jina kama vile Tigo -Yash
 
Kama hizi taarifa za kweli basi umefika muda Sasa wanasheria mahiri wakusanye ushahidi kwa waathirika wa upotevu wa pesa kisha wafungue kesi ya pamoja.
Mfano wa ile inaitwa CLASS ACTION kule Marekani.
Kuna watu wamepoteza maisha kwa matatizo ya kushindwa kupata pesa zao toka bank.
 
Back
Top Bottom