Crdb bank Mlimani City rushwa nje nje!

:ballchain:
Nawasilisha hii ni kero iliyokomaa pale CRDB Mlimani City, Kumbe hata uwahi kiasi gani huwezi kupata namba za kwanza kwanza ili kukaa kwenye foleni ya kupata huduma ya kibenki.Kisa ni washikaji wale wawili askari na binti mmoja walioko pale mlangoni kwenye mizani ya kutolea namba!! Huwa wanatoa namba za mbali kama 60,70 nk na zile za karibu 1,2,3,nk wanakuwa nazo kuwauzia wateja wale wenye haraka zao na wasiotaka kupanga foleni li wapatei huduma za haraka. Mchezo huo mchafu hufanywa kwa tactics za hali ya juu hata wakati mwingine kuwahusisha wateja.Bei ya tikiti ya namba hufika hadi 5,000/=, mara nyingi book mbili, tatu na nne.Uongozi wa Benki wanajua maana husema "mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake"!!Ndg zangu wateja wengine kero hii mmeiona? Mwasemaje??

Uongozi wa benki jaribu kurekebisha kero hizi. Mnatuhabisha na kutukela sisi wateja wenu.
 
Mzaha mzaha hutumbuka usaha. Ni aibu sana kwa wananchi kutetea uozo Huu . Anayeenda benki anatarajia kupata huduma awahi kufanya shughuli nyingine.Hakuna aliyeenda kushinda benki kusubiri wachache wahudumiwe haraka kwa kutofoleni.Ni jambo la kukemea kwa nguvu zote.
 
Dosari ya jinsi hii isimfanye mteja kukimbia Benki ili hali inarekebishika.Wahusika watasoma hapa na wachukue hatua mara moja!!!!Tusilee rushwa katika jamii zetu!!

Naomba kutofautiana na wewe kuhusu hili. Njia bora kabisa ya kuwafanya wajirekebishe ni kuwahama. Kusema ukweli CRDB huduma zao ni mbovu mno, sielewi hata recruitment yao ikoje, maana wana wafanyakazi wengi wanaofanya kazi as if hawajui hata basic banking principles.
 
Acha fitina na majungu, serious issues unazi-bypass unaleta majungu, zungumzia kwenye hospitali zetu wagonjwa wanavyokosa matibabu au watoto wetu na shule za chini ya miti aghhhhhhhhhhhhhhhhhhh kaa foleni au weka vijisenti vyako mchagoni


Ndio tatizo lenu wadanganyika. Kwa kuwa hospital kuna matatizo pia ndio avumilie uozo kwingine? Ni watu kama nyinyi mnaolea uzembe!
 
Nawasilisha hii ni kero iliyokomaa pale CRDB Mlimani City, Kumbe hata uwahi kiasi gani huwezi kupata namba za kwanza kwanza ili kukaa kwenye foleni ya kupata huduma ya kibenki.Kisa ni washikaji wale wawili askari na binti mmoja walioko pale mlangoni kwenye mizani ya kutolea namba!! Huwa wanatoa namba za mbali kama 60,70 nk na zile za karibu 1,2,3,nk wanakuwa nazo kuwauzia wateja wale wenye haraka zao na wasiotaka kupanga foleni li wapatei huduma za haraka. Mchezo huo mchafu hufanywa kwa tactics za hali ya juu hata wakati mwingine kuwahusisha wateja.Bei ya tikiti ya namba hufika hadi 5,000/=, mara nyingi book mbili, tatu na nne.Uongozi wa Benki wanajua maana husema "mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake"!!Ndg zangu wateja wengine kero hii mmeiona? Mwasemaje??

Sipendi rushwa sana 2 kwani ndio iliyo2fanya watanzania wengi kuwa masikini....kwa hili cjalielewa vizuri labda mtoa mada na m2 mwingine anieleweshe kwa hili.Mfano huyo m2 mwenye haraka amechelewa let say amekuja kama saa 3.30 asb na akapewa hiyo tiketi let say no.20 ambayo kwa muda huo hiyo namba itakuwa imeshapita muda mrefu,hapo inakuaje?(ukumbuke ina2mia electronics programmable device to perform that operation)
 
TAKUKURU MPOOO? Ujumbe mmeusoma na viongozi wa CRDB kama ni members lifanyieni kazi maana hii ni indicator mabaya sana kwa benki kama hii
 
Acha fitina na majungu, serious issues unazi-bypass unaleta majungu, zungumzia kwenye hospitali zetu wagonjwa wanavyokosa matibabu au watoto wetu na shule za chini ya miti aghhhhhhhhhhhhhhhhhhh kaa foleni au weka vijisenti vyako mchagoni

wewe una akili kweli?
 
Mkuu unanikumbusha siku moja nimefika pale kama kwenye saa nane hivi mchana, nikafika nikachukua tiketi namba 703, kusikiliza tiketi namba 397 ndo ikaitwa ilibidi nishtuke, nikiangalia watu waliopo hata 200 hawafiki, nikajisemea hapa sio nikaenda zangu mlimani chuoni nikakuta watu hata 30 hawafiki, kumbe ndo mchezo wao.
 
sidhan kama kuna ukweli hapa nnavyojua ile kitu iko electronically programed sasa ukifikiria kwa makin there is no such issue... this the home of great thinker...think wize!
 
Hata mimi naona kuna upotoshwaji wa mambo hapa na wanajamii nao wanameza tu! siku hizi kuna competitions za kibenki kama ilivyo kwenye makampuni ya simu mnajuaje kama huyu mtoboasiri ni mdau kwenye benki nyingine na anaeneza sumu...? jamani kabla hatujaongea tuwe tunafanya uchunguzi wa kutosha na sio kuharibu makampuni ya watu for cheap popularity....With a light touch....
 
halafu huu utaratibu wa namba huu...
hivi waliwaza nini?

halafu mkuu benki zipo nyingi, tena hazina hata foleni hama huko washashiba hao ndo maana wanawapelekesha wateja
 
Hii thread ingekuwa nzuri zaidi ya ilivyo kama mhusika angefanya uchunguzi yeye binafsi.. Jinsi slivyoaiandaa thread yake utasema kasikia kwa mtu..
 
Nawasilisha hii ni kero iliyokomaa pale CRDB Mlimani City, Kumbe hata uwahi kiasi gani huwezi kupata namba za kwanza kwanza ili kukaa kwenye foleni ya kupata huduma ya kibenki.Kisa ni washikaji wale wawili askari na binti mmoja walioko pale mlangoni kwenye mizani ya kutolea namba!! Huwa wanatoa namba za mbali kama 60,70 nk na zile za karibu 1,2,3,nk wanakuwa nazo kuwauzia wateja wale wenye haraka zao na wasiotaka kupanga foleni li wapatei huduma za haraka. Mchezo huo mchafu hufanywa kwa tactics za hali ya juu hata wakati mwingine kuwahusisha wateja.Bei ya tikiti ya namba hufika hadi 5,000/=, mara nyingi book mbili, tatu na nne.Uongozi wa Benki wanajua maana husema "mbuzi hula kwa urefu wa kamba yake"!!Ndg zangu wateja wengine kero hii mmeiona? Mwasemaje??


kaka i agree with u 100% mimi nilienda pale bank niliwahi nikawa kama mtu wa 7 kuingia benk nikapewa kile kikaratasi na yule dada anayefungua mlango...masikini ya mungu nilikuta kimeandikwa namba 73. nakubaliana na wewe asilimia 100 kweli wnakera sana.!!!
 
sidhan kama kuna ukweli hapa nnavyojua ile kitu iko electronically programed sasa ukifikiria kwa makin there is no such issue... this the home of great thinker...think wize!

ni hivi mkuu, ukifika pale kabla hawajafungua kunakuwa na msongamano wa watu so always anakuwepo dada mmoja hivi,,,anakuwa tayari anavikaratasi vingi mkononi anawagawia watu....sasa unajua unapoingia tuuu kwakuwa zinakuwa vurugu ukipewa karatasi huangalii unakimbilia kiti kukaa. ukifika kwenye kiti ndugu yangu .ukiangalia namba ya kwenye karatasi unaweza kufa presure...!!
 
ni hivi mkuu, ukifika pale kabla hawajafungua kunakuwa na msongamano wa watu so always anakuwepo dada mmoja hivi,,,anakuwa tayari anavikaratasi vingi mkononi anawagawia watu....sasa unajua unapoingia tuuu kwakuwa zinakuwa vurugu ukipewa karatasi huangalii unakimbilia kiti kukaa. ukifika kwenye kiti ndugu yangu .ukiangalia namba ya kwenye karatasi unaweza kufa presure...!!

Mwambie! Anadhani electronic programs haziwezi kuwa manipulated!
 
Back
Top Bottom