kwa jinsi ulivyouliza, inaonesha hufahamu haya mambo ya dunia ya kwanza, hivyo nakusamehe tuu. Nimeweka karatasi kwasababu ya privacy, sina haja ya kukudanganya.
Nchi hii... account za utilities, phone bills n.k zinakuwa zimeunganishwa na SSN, ni unique namba ambayo ina taarifa zako zote. Mtoto akizaliwa tuu hupewa hiyo namba na anakuwa nayo mpaka anakufa. Kwa hiyo, kwa privacy yangu nimeamu kuiziba.
Dah, sijui nisemeje, ungejua bills za hapa zilivyo wala usingeshangaa... hiyo $97 ni champ change kwa bili ya umeme wakati wa winter. Nyumba hapa zinakuwa na central heating/air system, washer/dryer, stove n.k vitu hivi vinakula sana wattage.
Mfano, sasa hivi tupo fall (season) lakini leo asubuhi teyari temperature nje ilikuwa 28F (-2 Celcius) na winter itakapo changanya (Jan - Feb) temp itashuka mpaka -6F (-21 Celsius). Sasa kwa temp hizo unafikiri bill itakuwa kiasi gani au unafikiri tunatumia kuni ku-warm nyumba?