Chuo kipi kinatoa wanafunzi Bora kuliko vyuo vyengine?

Chuo kipi kinatoa wanafunzi Bora kuliko vyuo vyengine?

Kwa maoni yangu, nenda 'Open University of Tanzania' (OUT) - Chuo Kikuu Huria Tanzania, ambayo ina 'approach' ya 'student-oriented study' na siyo 'teacher-oriented study': utajiona wewe ni kuku wa kienyeji anyajitafutia chakula na nyama yake ni tamu kuliko ya 'broilers'.
These guys are coming.

Education orientation ya Open University ni nzuri sana na ndio maana watu wengi kwa sasa wanaenda Open University kufanya Masters' degree na Ph.D
 
Salam wanajukwaa

Mara nyingi kumekuwa na majibizano juu ya mwanafunzi au mhitimu wa chuo kipi ni bora na yupi si bora?. huenda mkaona chapisho hili lisiwe na maana sana, au mkadhani ni upotezaji wa muda, wapo wanaoona hii tabia ya kujiona bora haiathiri chochote katika ustawi wa elimu na jamii kwa ujumla.

Lakini nimeona kuna haja ya kusema lile naloliona kuwa sawa, na huenda baadhi ya watu wasinielewe na wakabaki na mitizamo yao. Kwanza kabisa naamini elimu (education) ina maana pana na kuna mitizamo tofauti ya nini hasa kinabidi kiwe ndio kiini cha elimu. wapo walioona elimu kuwa ni maarifa (knowledge) ambayo huifadhiwa kichwani, wapo waliona kuwa elimu ni ujuzi wa kufanya mambo kwa mikono, wengine wakaona elimu ni maadili, hulka na tabia njema na kuwa na imani juu ya kitu fulani kama vile Mungu dini n.k. Lakini wengi tunaamini kuwa elimu ni muunganiko wa mambo yote hayo (all aspect of human development)

Sasa swali je nani kaelimika? Nani ana mamlaka au uwezo wa kuona kiwango cha elimu cha mwenzake? Mimi naamini kabisa mwanafunzi anaweza kuwa bora au si bora, yupo ambae amesoma na bado hajaelimika, na yupo ambae amesoma na ameelimika, na elimu ya mtu haipimwa kwa marks za darasani.

Elimu ya mtu inapimwa kwa kile anachokifanya katika maisha yake ya kila siku akiwa kazini, nyumbani na katika jamii na hivyo basi si kweli kuwa wanafunzi wa chuo fulani wameelimika zaidi kuliko wa vyuo vyengine, hata kama amesoma Harvard, Oxford au Cambridge huenda hana hule ujuzi, maarifa na hulka ya kilichokusudiwa katika program aliyosoma. Sasa sikuuambii hivi vyuo vyetu vya Tanzania ambavyo ubora au ranking hazitofautiani sana. Si ajabu kusikia mtu anasema chuo chetu ndio kinatoa wahitimu bora kuliko wa vyuo vyote na kila mtu anasimama upande wa chuo chake.

Huenda aliesoma ualimu UDSM asiwe bora kabisa ukimlinganisha na Yule wa MNMA na kinyume chake. kuna sababu nyingi zinazomfanya mwanafunzi kuwa bora mbali na chuo anachosoma au ufaulu wa levels alizopita. Ubora wa mtu unaweza ukaletwa na jinsi mtu anavyoyapenda masomo yake, anavyoshiliki kujifunza katika forums mbalimbali katika internet, workshops, seminars. Binasfi nilisoma GIS darasani na kwenye internet lakini niliona kwenye internet kuna msaada zaidi kuliko hata darasani kwaiyo hamu yangu ya kujifunza zaidi ya nilichojifunza darasani ndio ilisababisha mimi kuelewa na kuwa mahiri zaidi. Hivi kweli mwanafunzi wa chuo X anafahamu kabisa namna chuo Y wanavyosoma, course contents, assessment zao na mambo mengine mpaka akawaona kuwa wao si bora?

Wapo wasomi wa vyuo Fulani wanaotumia ufaulu wao wa nyuma (A level na O level) kujiona wao ni bora kuliko wengine jambo ambalo si kweli hata kidogo. Kwanza ufaulu wako wa nyuma kaukufanyi kuwa na ufaulu mkubwa chuoni au wewe kuwa bora. Nakumbuka kuna watu chuoni walikuwa wanajitapata kuwa walikuwa wazuri high school na walipata supplementary, carry na hata disco kabisa. Wangapi wenye division 1 wamedisco na wale wenye three ni best student vyuoni, ipo tena mara nyingi tu.

Kwakweli inasikitasha kuona wasomi wetu wanabishana juu ya nani ni bora. Tupo tofauti sana na forums za wenzetu nchi mbalimbali ambao wanatumia hizo forums kudiscuss masuala mbalimbali yenye kuleta faida. Tunaweza kutumia majukwaa na yakawa na faida kubwa sana. lakini leo hii hata ukimuambia mtu kuwa nimeuliza swali jamii forum atakuona mpuuzi na unapoteza muda tu, kwasababu hata kama unauliza au unataka kujifunza kitu wapo watakukatisha tamaa, kukukashifu na kukuletea mzaha.

Mimi naamini kama elimu yako ni bora basi itakusaidia wewe katika ulimwengu huu ambao maisha ni tight sana, ajira ni ngumu kwelikweli na kila kitu kimebadilika. Mwenye elimu bora hasemi mimi au sisi tuna elimu bora bali elimu yake itaonekana kwa kile anachofanya. Binasfi watu naowaona hawajaelimika kabisa na degree zao ni bure ni wale wanaojitapa kuwa wao ni bora kuliko wengine no matter wanasoma au wamesoma wapi.

Ulimwengu wa sasa ni wenye changamoto tele, magonjwa, uchafuzi wa mazingira, elimu duni, ukosefu wa ajira, umaskini uliokithiri, rushwa, maadili mabovu, teknolojia duni, lakini sisi bado tupo tunabishana tu mara utasikia “UDOM NDIO BORA, UDSM BABALAO, SAUT NDIO CHUO, SUA FUNGA KAZI, MZUMBE KWA VICHWA PALE” inasaidia nini?, nathubutu kusema huu ni UJINGA mkubwa wa baadhi ya wanaojiita wasomi, maneno hayo hayakupaswa kusemwa na watu walioko level ya chuo kikuu. Niaminini tunaweza kutumia majukwaa haya vizuri na yakatuletea faida, kweli kama tutashare links za wapi tunaweza kujifunza, sehemu za kuaccess materials, online lectures, kuleta mijadala yenye faida n.k

Naimani nimeeleweka.
Uzi merfu sana , unachosha kusoma!!!!! mwenye summary plz
 
Salam wanajukwaa

Mara nyingi kumekuwa na majibizano juu ya mwanafunzi au mhitimu wa chuo kipi ni bora na yupi si bora?. huenda mkaona chapisho hili lisiwe na maana sana, au mkadhani ni upotezaji wa muda, wapo wanaoona hii tabia ya kujiona bora haiathiri chochote katika ustawi wa elimu na jamii kwa ujumla.

Lakini nimeona kuna haja ya kusema lile naloliona kuwa sawa, na huenda baadhi ya watu wasinielewe na wakabaki na mitizamo yao. Kwanza kabisa naamini elimu (education) ina maana pana na kuna mitizamo tofauti ya nini hasa kinabidi kiwe ndio kiini cha elimu. wapo walioona elimu kuwa ni maarifa (knowledge) ambayo huifadhiwa kichwani, wapo waliona kuwa elimu ni ujuzi wa kufanya mambo kwa mikono, wengine wakaona elimu ni maadili, hulka na tabia njema na kuwa na imani juu ya kitu fulani kama vile Mungu dini n.k. Lakini wengi tunaamini kuwa elimu ni muunganiko wa mambo yote hayo (all aspect of human development)

Sasa swali je nani kaelimika? Nani ana mamlaka au uwezo wa kuona kiwango cha elimu cha mwenzake? Mimi naamini kabisa mwanafunzi anaweza kuwa bora au si bora, yupo ambae amesoma na bado hajaelimika, na yupo ambae amesoma na ameelimika, na elimu ya mtu haipimwa kwa marks za darasani.

Elimu ya mtu inapimwa kwa kile anachokifanya katika maisha yake ya kila siku akiwa kazini, nyumbani na katika jamii na hivyo basi si kweli kuwa wanafunzi wa chuo fulani wameelimika zaidi kuliko wa vyuo vyengine, hata kama amesoma Harvard, Oxford au Cambridge huenda hana hule ujuzi, maarifa na hulka ya kilichokusudiwa katika program aliyosoma. Sasa sikuuambii hivi vyuo vyetu vya Tanzania ambavyo ubora au ranking hazitofautiani sana. Si ajabu kusikia mtu anasema chuo chetu ndio kinatoa wahitimu bora kuliko wa vyuo vyote na kila mtu anasimama upande wa chuo chake.

Huenda aliesoma ualimu UDSM asiwe bora kabisa ukimlinganisha na Yule wa MNMA na kinyume chake. kuna sababu nyingi zinazomfanya mwanafunzi kuwa bora mbali na chuo anachosoma au ufaulu wa levels alizopita. Ubora wa mtu unaweza ukaletwa na jinsi mtu anavyoyapenda masomo yake, anavyoshiliki kujifunza katika forums mbalimbali katika internet, workshops, seminars. Binasfi nilisoma GIS darasani na kwenye internet lakini niliona kwenye internet kuna msaada zaidi kuliko hata darasani kwaiyo hamu yangu ya kujifunza zaidi ya nilichojifunza darasani ndio ilisababisha mimi kuelewa na kuwa mahiri zaidi. Hivi kweli mwanafunzi wa chuo X anafahamu kabisa namna chuo Y wanavyosoma, course contents, assessment zao na mambo mengine mpaka akawaona kuwa wao si bora?

Wapo wasomi wa vyuo Fulani wanaotumia ufaulu wao wa nyuma (A level na O level) kujiona wao ni bora kuliko wengine jambo ambalo si kweli hata kidogo. Kwanza ufaulu wako wa nyuma kaukufanyi kuwa na ufaulu mkubwa chuoni au wewe kuwa bora. Nakumbuka kuna watu chuoni walikuwa wanajitapata kuwa walikuwa wazuri high school na walipata supplementary, carry na hata disco kabisa. Wangapi wenye division 1 wamedisco na wale wenye three ni best student vyuoni, ipo tena mara nyingi tu.

Kwakweli inasikitasha kuona wasomi wetu wanabishana juu ya nani ni bora. Tupo tofauti sana na forums za wenzetu nchi mbalimbali ambao wanatumia hizo forums kudiscuss masuala mbalimbali yenye kuleta faida. Tunaweza kutumia majukwaa na yakawa na faida kubwa sana. lakini leo hii hata ukimuambia mtu kuwa nimeuliza swali jamii forum atakuona mpuuzi na unapoteza muda tu, kwasababu hata kama unauliza au unataka kujifunza kitu wapo watakukatisha tamaa, kukukashifu na kukuletea mzaha.

Mimi naamini kama elimu yako ni bora basi itakusaidia wewe katika ulimwengu huu ambao maisha ni tight sana, ajira ni ngumu kwelikweli na kila kitu kimebadilika. Mwenye elimu bora hasemi mimi au sisi tuna elimu bora bali elimu yake itaonekana kwa kile anachofanya. Binasfi watu naowaona hawajaelimika kabisa na degree zao ni bure ni wale wanaojitapa kuwa wao ni bora kuliko wengine no matter wanasoma au wamesoma wapi.

Ulimwengu wa sasa ni wenye changamoto tele, magonjwa, uchafuzi wa mazingira, elimu duni, ukosefu wa ajira, umaskini uliokithiri, rushwa, maadili mabovu, teknolojia duni, lakini sisi bado tupo tunabishana tu mara utasikia “UDOM NDIO BORA, UDSM BABALAO, SAUT NDIO CHUO, SUA FUNGA KAZI, MZUMBE KWA VICHWA PALE” inasaidia nini?, nathubutu kusema huu ni UJINGA mkubwa wa baadhi ya wanaojiita wasomi, maneno hayo hayakupaswa kusemwa na watu walioko level ya chuo kikuu. Niaminini tunaweza kutumia majukwaa haya vizuri na yakatuletea faida, kweli kama tutashare links za wapi tunaweza kujifunza, sehemu za kuaccess materials, online lectures, kuleta mijadala yenye faida n.k


BEST STUDENT ANATEMBEZA BAHASHA ''ZERO CREATIVITY AND INNOVATION''
 
Kinaitwa "street university". Ukiweza kutoboa ktk chuo hiki, hakika mambo yanakuwa mazuri sana.
 
These guys are coming.

Education orientation ya Open University ni nzuri sana na ndio maana watu wengi kwa sasa wanaenda Open University kufanya Masters' degree na Ph.D
Hakuna kitu cha hivyo,wengi wanasoma OUT kutokana na kubanwa na majukumu mengine hasa ya kazi za kuajiriwa, Hivyo wanasoma huko kwa sababu kunaruhusu wao kusoma na kutekeleza majukumu mengine aidha ya muajiri au ya kujiajiri.

Time will Tell!
 
Hakuna kitu cha hivyo,wengi wanasoma OUT kutokana na kubanwa na majukumu mengine hasa ya kazi za kuajiriwa, Hivyo wanasoma huko kwa sababu kunaruhusu wao kusoma na kutekeleza majukumu mengine aidha ya muajiri au ya kujiajiri.

Time will Tell!
Ni kweli, lakini wako vizuri sana kwenye supervision. Hawana longolongo sana kama masupervisor wa vyuo vikuu vingine hapa nchini
 
Back
Top Bottom