Chuo kikuu kipya cha kilimo Katavi, ni haraka mno

Lyimo

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,826
2,017
Nimestushwa na taarifa ya serikali kutaka kujenga chuo kikuu kingine cha Kilimo katika mkoa wa Katavi, kama ilivyoandikwa kwenye gazeti la Majira la leo. Sababu ya mstuko huo ni hali mbaya ya vyuo vyetu vya kilimo vilivyopo ambayo vinashindwa kijikidhi na kutoa huduma stahiki kutokana na bajeti finyu inayopokea kutoka serikalini. Chuo kikuu kilichopo (SUA) bado kinahitaji kujitanua na hakijajitosheleza wataalamu, hivyo ni heri serikali ingeongeza nguvu kwenye chuo hicho kama inajali zaidi wakulima. Kwa miaka ya karibuni sasa kumekuwa na mfumuko wa vyuo vikuu Tanzania jambo lililopelekea hata kushusha viwango vya kuingia kwenye vyuo hivyo, jambo ambalo lilibarikiwa na Tume ya vyuo Vikuu (TCU). Mfumuko huu utasababisha kutozalisha wataalamu waendeshaji/ watendaji wenye ngazi ya Diploma na Cerificates ambao ni wanahitajika sana kutokana na mahitaji ya Taifa. Bado wataalamu wa Kilimo hawatoshelezi Kata zote nchini, licha kimfumo kila kijiji kinahitaji bwana shamba na bwana mifugo ambao vijiji vingi sana hawana, hivyo hata kupata maelekezo/ushauri wa kitaalamu haiwezekani. Sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kina katika kuwekeza kwenye mahitaji ya wataalamu wa kilimo nchini.

Vyuo vya Kilimo na Utafiti vya serikali ninavyovikumbuka kwa uchache, (wachangiaji mtanisaidia kuongezea vingine vingi):
- Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) – Morogoro;
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole – Mbeya
- Chuo cha maendeleo ya Mifugo Tengeru (LITI-Tengeru) – Arusha
- Tengeru Horticultural Reasearch and Trainning (HORTI).- Arusha
- Chuo cha kilimo na Utafiti Kilombero (KATRIN) – Morogoro
- Chuo cha Kilimo taaluma ya umwagiliaji Igurusi - Mbeya
- Chuo cha kilimo na Utafiti Ilonga (MATI – Ilonga) – Morogoro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Kilimanjaro (KATC) - Kilimanjaro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Mlingo
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Morogoro (LITI – Morogoro) – Morogoro
- Chuo Cha Utafiti wa Kilimo Cha Ukiriguru
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Buhuri (LITI – Buhuri) – Tanga
- Chuo cha Maendeleo ya Kilimo Inyala – Mbeya
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Selian (SARI) – Arusha
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Mpwapwa (LITI – Mpwapwa) - Mpwapwa
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Naliendele – Mtwara
- Chuo cha utafiti wa Kilimo Tumbi – Kibaha
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Mlingano – Tanga
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Tumbe – Tabora
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa magonjwa ya wanyama (ADRI) – DSM
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Madaba - Songea

Vyuo hivi vingeweza kutumika vizuri kufundisha wataalamu na hata wakulima ili kuweza kuendesha kilimo chenye tija. Tukumbuke kuwa, wananchi wengi maskini Tanzania ni wakulima, hivyo tukiacha hivi vyuo vijiendeshe kibiashara kama vyuo vya uhasibu ama IT ambavyo wahitimu wake ni rahisi kuajiriwa mijini. Vilevile mazingira bora ya watumishi wa vijijini yanahitajika ili kuwavutia wataalamu kufanya kazi vijijini. Kama serikali haitaweka kipaumbele kwenye kuboresha miundombinu vijijini na kuelimisha wakulima ili waweze kufanya kilimo chenye tija ni dhahiri kuwa wimbi la vijana kukimbilia mijini halitakoma. Serikali ilitakiwa kuvisaidia kwa hali na mali vyuo hivi vilivyotawanyika nchi nzima japo vina wataalamu wachache bado. Sioni mantiki ya kukimbilia Kujenga chuo kikuu cha Kilimo Katavi wakati wahadhiri/watafiti hawapo wa kutosha nchini (SUA haijajitosheleza bado). Vilevile kwa Tanzania ya leo bado ni ndoto kuwa na mabwana shama wenye taaluma ya degree, hivyo ni vema tukaweka mkazo kwanza kwenye hivi vyuo vya diploma na certificate. Wakati utafika ambapo tutakuwa na hitaji la vyuo vikuu baada ya kujitosheleza kwenye hii ngazi ya kati kimahitaji. Swala la Chuo kikuu Katavi ni la haraka mno na linaonekana lina maslahi kisiasa zaidi kuliko kutoa huduma ya elimu, ushauri na utafiti kwa wananchi.
 
si unajua sera zetu za sasa ni kuwa na institutions za kikata? hopefully, kitakuwa chuo kingine cha kata!
 
Pale wananchi watakapokuwa na nguvu ya kuamua pesa zao zitumike kufanya nini ndipo tutakapoachana na bajeti zinazofuata kuwapendezesha na kuwapa utukufu wanasiasa. Possibly kitaitwa Mtoto wa Mkulima University
 
Hi kile cha JK Nyerere Agricultural university - Musoma kilichoahidiwa na jk wakati wa kampeni kiliishia wapi?
 
hapa nchini fani yenye wasomi wengi kuliko zote na PH kibao ni kilimo!!! lakini ebu nambie ....
 
Nimestushwa na taarifa ya serikali kutaka kujenga chuo kikuu kingine cha Kilimo katika mkoa wa Katavi, kama ilivyoandikwa kwenye gazeti la Majira la leo. Sababu ya mstuko huo ni hali mbaya ya vyuo vyetu vya kilimo vilivyopo ambayo vinashindwa kijikidhi na kutoa huduma stahiki kutokana na bajeti finyu inayopokea kutoka serikalini. Chuo kikuu kilichopo (SUA) bado kinahitaji kujitanua na hakijajitosheleza wataalamu, hivyo ni heri serikali ingeongeza nguvu kwenye chuo hicho kama inajali zaidi wakulima. Kwa miaka ya karibuni sasa kumekuwa na mfumuko wa vyuo vikuu Tanzania jambo lililopelekea hata kushusha viwango vya kuingia kwenye vyuo hivyo, jambo ambalo lilibarikiwa na Tume ya vyuo Vikuu (TCU). Mfumuko huu utasababisha kutozalisha wataalamu waendeshaji/ watendaji wenye ngazi ya Diploma na Cerificates ambao ni wanahitajika sana kutokana na mahitaji ya Taifa. Bado wataalamu wa Kilimo hawatoshelezi Kata zote nchini, licha kimfumo kila kijiji kinahitaji bwana shamba na bwana mifugo ambao vijiji vingi sana hawana, hivyo hata kupata maelekezo/ushauri wa kitaalamu haiwezekani. Sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kina katika kuwekeza kwenye mahitaji ya wataalamu wa kilimo nchini.

Vyuo vya Kilimo na Utafiti vya serikali ninavyovikumbuka kwa uchache, (wachangiaji mtanisaidia kuongezea vingine vingi):
- Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) – Morogoro;
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole – Mbeya
- Chuo cha maendeleo ya Mifugo Tengeru (LITI-Tengeru) – Arusha
- Tengeru Horticultural Reasearch and Trainning (HORTI).- Arusha
- Chuo cha kilimo na Utafiti Kilombero (KATRIN) – Morogoro
- Chuo cha Kilimo taaluma ya umwagiliaji Igurusi - Mbeya
- Chuo cha kilimo na Utafiti Ilonga (MATI – Ilonga) – Morogoro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Kilimanjaro (KATC) - Kilimanjaro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Mlingo
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Morogoro (LITI – Morogoro) – Morogoro
- Chuo Cha Utafiti wa Kilimo Cha Ukiriguru
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Buhuri (LITI – Buhuri) – Tanga
- Chuo cha Maendeleo ya Kilimo Inyala – Mbeya
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Selian (SARI) – Arusha
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Mpwapwa (LITI – Mpwapwa) - Mpwapwa
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Naliendele – Mtwara
- Chuo cha utafiti wa Kilimo Tumbi – Kibaha
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Mlingano – Tanga
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Tumbe – Tabora
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa magonjwa ya wanyama (ADRI) – DSM
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Madaba - Songea

Vyuo hivi vingeweza kutumika vizuri kufundisha wataalamu na hata wakulima ili kuweza kuendesha kilimo chenye tija. Tukumbuke kuwa, wananchi wengi maskini Tanzania ni wakulima, hivyo tukiacha hivi vyuo vijiendeshe kibiashara kama vyuo vya uhasibu ama IT ambavyo wahitimu wake ni rahisi kuajiriwa mijini. Vilevile mazingira bora ya watumishi wa vijijini yanahitajika ili kuwavutia wataalamu kufanya kazi vijijini. Kama serikali haitaweka kipaumbele kwenye kuboresha miundombinu vijijini na kuelimisha wakulima ili waweze kufanya kilimo chenye tija ni dhahiri kuwa wimbi la vijana kukimbilia mijini halitakoma. Serikali ilitakiwa kuvisaidia kwa hali na mali vyuo hivi vilivyotawanyika nchi nzima japo vina wataalamu wachache bado. Sioni mantiki ya kukimbilia Kujenga chuo kikuu cha Kilimo Katavi wakati wahadhiri/watafiti hawapo wa kutosha nchini (SUA haijajitosheleza bado). Vilevile kwa Tanzania ya leo bado ni ndoto kuwa na mabwana shama wenye taaluma ya degree, hivyo ni vema tukaweka mkazo kwanza kwenye hivi vyuo vya diploma na certificate. Wakati utafika ambapo tutakuwa na hitaji la vyuo vikuu baada ya kujitosheleza kwenye hii ngazi ya kati kimahitaji. Swala la Chuo kikuu Katavi ni la haraka mno na linaonekana lina maslahi kisiasa zaidi kuliko kutoa huduma ya elimu, ushauri na utafiti kwa wananchi.
Mi naona huu ni uamuzi wa kisiasa zaidi kuliko uhalisia. Hivi kweli tuna tatizo la wataalamu wa kilimo? Serikali haijui adha wanayopata wanafunzi wa SUA ktk soko la ajira?Kuna wanafunzi wengi wa SUA wako ktk mabenki na wengine ni waalimu wanafundisha shule za sekondari kwa leseni. Na wengine wapo tu mtaani, hii ina maana serikali inasomesha nguvukazi ambayo haitumiki ipasavyo. Serikali inapaswa kufanya utafiti kwanza kabla ya kuanzisha vyuo vikuu mbali mbali huku ikiviacha vingine yatima (kifedha). Kuna faida gani ya kuwa na vyuo vingi vilivyojaa maTA (ambao nao kimsingi ni wanafunzi), badala ya kuwa na vichache vyenye ubora wa miundombinu na wabobezi? Kupeleka Chuo Kikuu cha Kilimo Katavi ni kumfurahisha Ndugu Pinda kwa kuwa anapenda kulima.
 
Ahhh kaka hujui sera ya serikali ya awamu ya nne chini ya JK??? Basi ni kujenga chuo kikuu katika kila majimbo ya uchaguzi wanayotoka viongozi wakuu wa serikali. Ilianza University ya Bagamoyo kwa JK, haya sasa inakuja university jimboni kwa Mtoto wa mkulima, usishangae ukisikia kikifuatia jimboni kwa Ghalibu bilali au kwa Makinda!!!
 
kila kiongozi CCM anakilmbilia kuwekeza kwao, hii rushwa mamboleo! huoni shule ya msingi kujengwa na wachina?
Ni Nyerere tu hakufanikiwa kufanya hivyo.
 
Nimestushwa na taarifa ya serikali kutaka kujenga chuo kikuu kingine cha Kilimo katika mkoa wa Katavi, kama ilivyoandikwa kwenye gazeti la Majira la leo. Sababu ya mstuko huo ni hali mbaya ya vyuo vyetu vya kilimo vilivyopo ambayo vinashindwa kijikidhi na kutoa huduma stahiki kutokana na bajeti finyu inayopokea kutoka serikalini. Chuo kikuu kilichopo (SUA) bado kinahitaji kujitanua na hakijajitosheleza wataalamu, hivyo ni heri serikali ingeongeza nguvu kwenye chuo hicho kama inajali zaidi wakulima. Kwa miaka ya karibuni sasa kumekuwa na mfumuko wa vyuo vikuu Tanzania jambo lililopelekea hata kushusha viwango vya kuingia kwenye vyuo hivyo, jambo ambalo lilibarikiwa na Tume ya vyuo Vikuu (TCU). Mfumuko huu utasababisha kutozalisha wataalamu waendeshaji/ watendaji wenye ngazi ya Diploma na Cerificates ambao ni wanahitajika sana kutokana na mahitaji ya Taifa. Bado wataalamu wa Kilimo hawatoshelezi Kata zote nchini, licha kimfumo kila kijiji kinahitaji bwana shamba na bwana mifugo ambao vijiji vingi sana hawana, hivyo hata kupata maelekezo/ushauri wa kitaalamu haiwezekani. Sidhani kama serikali imefanya utafiti wa kina katika kuwekeza kwenye mahitaji ya wataalamu wa kilimo nchini.

Vyuo vya Kilimo na Utafiti vya serikali ninavyovikumbuka kwa uchache, (wachangiaji mtanisaidia kuongezea vingine vingi):
- Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) – Morogoro;
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Uyole – Mbeya
- Chuo cha maendeleo ya Mifugo Tengeru (LITI-Tengeru) – Arusha
- Tengeru Horticultural Reasearch and Trainning (HORTI).- Arusha
- Chuo cha kilimo na Utafiti Kilombero (KATRIN) – Morogoro
- Chuo cha Kilimo taaluma ya umwagiliaji Igurusi - Mbeya
- Chuo cha kilimo na Utafiti Ilonga (MATI – Ilonga) – Morogoro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Kilimanjaro (KATC) - Kilimanjaro
- Chuo cha Mafunzo ya Kilimo cha Mlingo
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Morogoro (LITI – Morogoro) – Morogoro
- Chuo Cha Utafiti wa Kilimo Cha Ukiriguru
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Buhuri (LITI – Buhuri) – Tanga
- Chuo cha Maendeleo ya Kilimo Inyala – Mbeya
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Selian (SARI) – Arusha
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Mpwapwa (LITI – Mpwapwa) - Mpwapwa
- Chuo cha Utafiti wa Kilimo cha Naliendele – Mtwara
- Chuo cha utafiti wa Kilimo Tumbi – Kibaha
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Mlingano – Tanga
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa Kilimo cha Tumbe – Tabora
- Chuo cha Mafunzo ya Utafiti wa magonjwa ya wanyama (ADRI) – DSM
- Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Madaba - Songea

Vyuo hivi vingeweza kutumika vizuri kufundisha wataalamu na hata wakulima ili kuweza kuendesha kilimo chenye tija. Tukumbuke kuwa, wananchi wengi maskini Tanzania ni wakulima, hivyo tukiacha hivi vyuo vijiendeshe kibiashara kama vyuo vya uhasibu ama IT ambavyo wahitimu wake ni rahisi kuajiriwa mijini. Vilevile mazingira bora ya watumishi wa vijijini yanahitajika ili kuwavutia wataalamu kufanya kazi vijijini. Kama serikali haitaweka kipaumbele kwenye kuboresha miundombinu vijijini na kuelimisha wakulima ili waweze kufanya kilimo chenye tija ni dhahiri kuwa wimbi la vijana kukimbilia mijini halitakoma. Serikali ilitakiwa kuvisaidia kwa hali na mali vyuo hivi vilivyotawanyika nchi nzima japo vina wataalamu wachache bado. Sioni mantiki ya kukimbilia Kujenga chuo kikuu cha Kilimo Katavi wakati wahadhiri/watafiti hawapo wa kutosha nchini (SUA haijajitosheleza bado). Vilevile kwa Tanzania ya leo bado ni ndoto kuwa na mabwana shama wenye taaluma ya degree, hivyo ni vema tukaweka mkazo kwanza kwenye hivi vyuo vya diploma na certificate. Wakati utafika ambapo tutakuwa na hitaji la vyuo vikuu baada ya kujitosheleza kwenye hii ngazi ya kati kimahitaji. Swala la Chuo kikuu Katavi ni la haraka mno na linaonekana lina maslahi kisiasa zaidi kuliko kutoa huduma ya elimu, ushauri na utafiti kwa wananchi.

Nadhani cha Tabora ni TUMBI- siyo TUMBE. Kulikuwepo pia cha MARUKU - Kagera na kipo cha Minazi pwani sijui wakiitaje.
 
Lyimo umesema vyema, katika harakati za serikali za kuongeza wataalam wa kilimo na mifugo (maafisa ugani) imekua ikiwasomesha kwenye vyuo vyake vya MATI na LITI, na wanahitimu huwapangia kazi ktk halmashauri zake, tatizo linakuja pale hao wataalam wanapokwenda kwenye maeneo ya kazi wanakutana na mazingira magumu ya kazi, maslahi mabovu, hakuna vitendea kazi, sasa anawezaje kugawa utaalamu alioupata kwa hao watanzani wenzetu ili kilimo na ufugaji viweze kumsaidia mkulima huyu ambaye Pinda anapigia kelele, w
 
Kuna wale waliosomeshwa kwa mtindo wao wa zimamoto katika vyuo vya MATI na LITI, bado wapo mtaani ajira hakuna!
 
Pale wananchi watakapokuwa na nguvu ya kuamua pesa zao zitumike kufanya nini ndipo tutakapoachana na bajeti zinazofuata kuwapendezesha na kuwapa utukufu wanasiasa. Possibly kitaitwa Mtoto wa Mkulima University
.......:...... True mkuu kwani umestukiaje kwamba son of a poor dad anashadadia kupata umaarufu wa milele...MKP UNIVERITY OF AGRICULTURE... P.O BOX 00000 MPANDA RUKWA... JIWE LA MSINGI LILIWEKWA MWAKA 2012 NA WAZIRI..........BW MKP....TU du mizengo bwana... Shabaabi kweli kweli wa umaarufu wakati mafisadi wamemweka kwapani anapelekwa kama bajaza..
 
pinda et al.JPG
Waziri mkuu akizungumza na viongozi wa mfuko wa Dr David Livingstone Academy Ltd-mara baada ya kikao cha kujadili uanzishwaji wa chuo kikuu cha katavi
Binafsi naona kuliko wangeanzisha chuo kipya-ni bora wangeboresha hiv vilivyopo sasa hivi
 
Have you noticed one thing; kila waziri mkuu anapoingia madarakani ajenda yake ni kwanza ni kutengeneza mkoa mpya huko kwao anakotoka. Sumaye kabla ya kumaliza ngwe yake alitengeneza mkoa wa Manyara na sasa Pinda nae ametemgeneza mkoa wa Katavi na sasa anataka kupeleka chuo kikuu cha kilimo!! Is there any economic justification for a poor country like Tanzania to embark on such uncalled for projects? Huo wote ni kuonesha ubinafsi kwa hawa viongozi.
 
badala ya kupongeza hatua nzuri tunaponda.....MIMI NAPONGEZA TENA VYUO VINGI ZAIDI VIANZISHWE ILI PIA KUJIJENGA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO TUTAKAZOKUTANA NAZO NA KUZITATUA
 
badala ya kupongeza hatua nzuri tunaponda.....MIMI NAPONGEZA TENA VYUO VINGI ZAIDI VIANZISHWE ILI PIA KUJIJENGA NA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO TUTAKAZOKUTANA NAZO NA KUZITATUA


Tunachotaka ni kuwa na vyuo vyenye ubora na sio idadi; pale tutakapoweza kuvihudumia hivi tulivyokuwanavyo kwa kiwango cha kuridhisha hakuna ubaya kuongeza vingine vipya.
 
It is sickening to note that in the year 2011 there are still so many ignorant Tanzanians who have no clue what the meaning of higher education is. What escaped the narrow-minded who decried the idea of addition of a prestigious university to Tanzania in general and to Katavi in particular is the concept behind it.

A university is more than issuance of degrees. Degrees are more than what gives individuals licence to work in airconditioned offices in big cities like Dar es salaam. Show me a degree holder (in anything) who doesn't have anything to do, you will be showing me an ignorant buffoon who has wasted public funds in creating nothing more than a useless robot of self.

Higher education is supposed to open your mind to a higher level of thinking, higher level of reasoning, it is supposed to make you more inquisitive, more imaginative,definitely self-sufficient and forward looking. It is extremely idiotic to surmise that if you have a degree then you have to have an office job. If that is your thinking, then I am not surprised that there so many ignorant

Tanzanians who are quite contended to clean other peoples toilets in UK, America, etc rather than go back to their villages and do real respectable work. Looking at another aspect, the original author of this despicable blog (and those who supported it) is the fact that this person hails from a place where there are 5 or more institutions of higher education.

The whole of Western Corridor has no such luxury! Therefore, you don't need standard 7 education to figure out why an institution of higher education is so invaluable to this part of grossly marginalised world. Remember,Tanzania has massive land which is yet to be exploited commercially.

In the next 25 years we will need to produce in excess of 50,000 agriculturists annually to be anywhere near meeting the shortage of people with suffient skills to make use of our land. And if the idea of starting such an expensive university is politically motivated, so what?

And who gives a toss? What is important in the end is getting something useful for once. After all, is that not why we have politicians? Any politician who leaves a legacy of something as important as a university should be praised by all even if you never had a chance to get no more than primary education yourself.
 
Looking for something to say 2015.........no priorities these days, its just a matter of "what something physical and attractive" watakachotudanganya nacho kwenye next election
 
Back
Top Bottom