Chuo cha ufundi pikipiki

Chuo cha ufundi pikipiki

kilimo kwz

Member
Joined
Jan 18, 2022
Posts
26
Reaction score
48
Wakuu kwema?

Naomba kufahamishwa ni wapi nitapata chuo kinachofundisha ufundi pikipiki,kuna mdogo wangu nataka nimpeleke akajifunze ufundi kwanza baadae nitamfungulia duka la spea za pikipiki.

Asanteni.[/b]
 
Hamna chuo kinachofundisha ufundi wa pikipiki Tanzania hii kwa sasa.
Mtaftie kijiwe ambacho kina mafundi wanaokubalika na bodaboda umweke hapo. After 6months atakuwa vizuri Sana Kama kichwa ni chepesi.
Ili aelewe zaidi hiyo fani,mtaftie smartphone ya kueleweka ili awe anapitia video za theory ya ufundi pikipiki youtube.
Kwa kifupi garage ndio ataelewa haraka kuliko kwenda kukaa darasani.
 
Hii naona kama atachukua mda mrefu kuelewa..
Achana na chuo japo chuo hakipo hata kingekuepo nisingekushauri umpeleke sababu ukimpeleka bado atarudi field mtaani. Chuo hawafundishi vizuri kama mtaani, nakwambia hivyo sababu nimekaa chuo kusoma fani fulani na chuo Practical ni asilimia 20 kati ya 80. Mpeleke vijiwe vyenye mafundi stadi uone balaa lake na utarudi hapa kunishukuru.
 
Back
Top Bottom