Chuki na husda dhidi ya wanaDiaspora


Kama hujanielewa kwa mfano huo, basi sijui nikueleze nini ndugu yangu ili uelewe. Mdau hapo chini kishakujibu, na nchi karibu zote duniani kote citizenship ya kuzaliwa haipokonywi.

Nitasisitiza tena, Mkenya na mtu yeyote kutoka nchi zingine akija Tanzania akajifanya ana ukana uraia wake kwa kutumia sheria ya kinyanyembe iliopo, hapo ana wa mock tu na sheria yenu ya kinyanyembe. Kimsingi, anakuwa hajapoteza uraia wake wa kuzaliwa hii si kwa mkenya tu ni karibu nchi zote duniani ikiwemo korea kaskazini na Russia. Hivyo atajifanya anaukana uraia wake mnampa passport anarudi kwao anapewa passport nyingine.

Hivyo sheria hiyo ya kinyanyembe haimzuii mkenya kumiliki passport ya Tanzania na Kenya kwa wakati mmoja. Bali inamzuia Mtanzania wa kuzaliwa kumliki passport zaidi ya moja. Ni sheria kadamizi kwa watanzania wazawa tu, wakati inatoa loop hole ya dual kwa watu wasio wazawa. Sasa sheria ya Kinyanyembe na kilugaluga namna hii inalinda vipi masilahi ya Tanzania? ni sheria ya kijuha iliyopita viwango vyote vya kijuha.
 


Mkuu ni chuki ambayo sijui chanzo chake ni nini? Dunia ya leo yenye kujaa watu na ukosefu mkubwa wa ajira nchi nyingi zinaruhusu uraia pacha ili kuencouage watu kwenda kutafuta kwingine ili kuondoa pressure nchini kwao. Serikali imekazania wana diaspora hawajafanya lobbyng ya kutosha kuconvince watanzania wengi,jamani lobbying ya nini iwapo umuhimu unafahamika? Nchi za Kenya, Uganda na Rwanda hakuna lobbying iliyofanyika bali viongozi waliona muhimu wake na sio kila swala muhimu kwa taifa viongozi lazim watafute maoni kwa wananchi wa kawaida ndio maana ni viongozi. Hebu tujiulize kidogo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar wananchi waliulizwa? Viti maalumu wanawake nani aliulizwa? Mfumo wa vyama vingi wananchi wengi walikataa serikali ikapitisha maana yake kuna mambo muhimu serikali hupitisha kwa manufaa ya nchi kwa hiyo swala la uraia pacha serikali haiitaji kufanyiwa lobbying maana hizi ni haki za watanzania walio nje ya nchi
 
Mkuu you must have a crooked mind!
Huyo dada anaye fanya kazi NASA alitekwa nyara?
Hebu tuanzie hapo.
 
Mkuu you must have a crooked mind!
Huyo dada anaye fanya kazi NASA alitekwa nyara?
Hebu tuanzie hapo.

Do I have a crooked mind? Nah, far from it.

Mkuu, uliuliza swali - ngoja nirudie swali lako " Huo urai wa huko ughaibuni waliupata kwa minajili gani?", nikakupa jibu na mfano halisi. Lakini naona mwenzangu umeamua kuchanja mbunga kwenye personal attacks. Huyo dada hakutekwa, bali aliamua kufanya kazi anayoipenda, ambayo hawezi kuipata bila uraia wa Marekani na ni kazi ambayo Tanzania hakuna. Kama una hoja ya msingi ya kumlaani mtu kama huyu dada asipewe uraia pacha, ningependa kuisikia hiyo hoja yako. Ndiyo maana tuna mijadala kama hii ya wazi.


 


😛eace: well said. But you know there is something within our psychology as a people that is threatened by this kind of success story.

we all do it. all of us. i believe there was something that was inserted into our DNA when we were forged as a nation , to bind us together as one people.

this thing has positives like the rejection of tribalism and classism.

but it also creates a suspicion of ambition and individualism which our neighbours the kenyans celebrate and encourage.

its a fascinating dichotomy. any sociologists on here who can shed more light?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…