Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
Picha hii, ilipigwa wakati wachezaji hao walipowasili nchini, wakitokea Burkina Faso, kucheza mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2008.
Katika mechi hiyo, Stars ilishinda bao 1-0 ugenini, hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu lakini ilipoteza mchezo wa mwisho na Msumbiji, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kutokana na furaha ya ushindi, wachezaji hao walivua fulana na mashati, hivyo kubaki vifua wazi kisha wakazunguka na gari lililowapokea na kuwazungusha wachezaji wa Stars, Dar es Salaam.
Hata hivyo, baadaye wachezaji hao watatu, walitimuliwa baadaye, wakibainika kukutwa na vitendo vya utovu wa nidhamu.