Baba Mdogo wa Tz
Member
- Feb 2, 2015
- 7
- 1
Viongozi wetu wa Dini zote ninawasii sana kwenda taratibu na wanasiasa.Wachumia tumbo hawa wanaweza ahidi chochote wakati wanataka kura,lakini utekelezaji wake ukawa hadithi au hata ukaleta madhara kwa jamii nzima ya Tanzania!Ndugu zangu waislamu mahakama yenu mtaipata kwa njia kuuwelewesha umma wa watanzania wote bila kujali dini,kabila wala cheo cha kisiasa!Wakristu kama baadhi ya waislamu wanatafsiri tofauti sana na dhana halisi ya hiyo mahakama kwa mfano:wanasema itaruhusu watu kukatwa mikono,kupigwa mawe hadi kufa na mambo mengine ya hovyo wala haqazungumzii faida zake.Mimi nionavyo tumieni muda mwingi kuzungumza na umma acheni wanasiasa watumwe na umma kuianzisha na mtafanikiwa kirahisi mno.Kwasasa mtaleta mashindano ya kiimani kwani wakristu watawatisha wanasiasa na kura sijui itakuaje maana wachumia tumbo watagawanyika tu!!!Ni ushauri tu wakubwa.