Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,638
SEHEMU YA 01
Kila mu ana uhuru wa kuweka mada anaoitaka ?Naona ili jukwaa sasa limegeuzwa dampo kila takataka wanakuja kutupia huku
Lakini siyo kwa kukurupuka huko kuokoteza story isiyokamilika na Kuja kuitupia huku.Kila mu ana uhuru wa kuweka mada anaoitaka ?
Wewe shida yako nini?
Sio lazima kila kitu usome tu kama vipi ifuteLakini siyo kwa kukurupuka huko kuokoteza story isiyokamilika na Kuja kuitupia huku.
nakubarSEHEMU: 02
MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’
SIMU: 0713 646500.
...ILIPOISHIA:
“Vipi alitaka kukataa kukulipa?”
“Walaa.”
“Sasa pamechimbika vipi?”
“Mmh! Babu mzima”
“Kivipi?”
“Aah, J4 kwani we mtoto? Ulinipeleka nikaimbe taarabu.”
SASA ENDELEA…
“Ooh, nimekuelewa kweli anajiita babu wa Kisemvule.”
“Na kweli nimeneng’emuka ndipo nilipokula.”
“Wachaaa! Kwa hiyo?”
“Njoo uchukue chako.”
“Ok, nakuja”
Baada ya kukata simu, alimgeukia shoga yake aliyekuwa na shauku ya kujua kilichoendelea.”
“Unaniambia nitemee chini kulikoni?”
“Wee acha, yule babu si bure lazima anatumia dawa za kuongeza nguvu.”
“Kwa nini?”
“Yaani, mzee alipopanda juu nilijua atachemsha, mwari nimechemsha mimi, Mwenzake nimelia mara nne yeye hata mara moja.”
“Wacha!”
“Nakwambia bila kuomba msaada mbona pangewaka moto.”
“Au alikunywea pombe kali?”
“Walaa, hatumii kinywaji kikali chochote.”
“Basi atakuwa anatumia dawa za kuongeza nguvu.”
“Hata hilo alilikataa amesema dawa yake ni kula vizuri na mazoezi.”
“Ikawaje?”
“Mpaka ananiachia nipo hoi, japo fedha nimepata lakini cha moto nimekiona.”
Mara mlango iligongwa, alikuwa J4.
“Karibu J4.”
“Mbona tena kitandani?”
“Unauliza jibu, kumbe mtu wenu mnamjua hukuniambia nilijua ‘wazee bata’ moja yupo hoi tena akiguswa kidogo anawahi kufika. Lakini leo mwanangu umeniingiza chaka la nyani mashavu yote yamewaka moto.”
“Nimekwambia anaitwa Babu wa Kisemvule.”
“Kweli, leo nimeneng’emuka ile mbaya, kidogo gwaride linishinde.”
“Lakini mvuvi haogopi dhoruba, Adela sina muda nipe changu nitambae.”Adela alimpa elfu 30.
J4 baada ya kupata cha juu alitambaa zake lakini kabla ya kuondoka Mamu shoga wa Adela naye aliomba shavu la kukutana na Babu wa Kisemvule.
“ J4, nipe na mimi shavu kwa babu.”
“Wewe tu dada yangu, maelezo yote atakupa Adela, ukiafiki utanipigia.”
“Nimeisha yapata nipo tayari.”
“Poa, nipe namba yako ya simu ishu ikitiki nikutwangie,” Mamu alimpa J4 namba ya simu.
“Basi kati ya siku mbili nitakutwangia dada angu.”
“Poa.”
J4 aliwaaga na kuwaacha wakiendelea kupiga stori za kalinye kalinye la Babu wa Kisemvule.
Baada ya kuondoka Adela alimgeukia Mamu aliyekuwa akisubiri kwa hamu kusikia habari za Babu wa Kisemvule.
“Mhu, Mwari?”
“Temea chini, babu ukimwangalia kwa umbile hata mkononi hajai, lakini mambo anayaweza, uzeeni yupo vile ujanani alikuwaje?”
“Babu wee, inawezekana umepungua uwezo na madawa yako ya kujidunga, subiri auingie moto huu kama hajanifia kifuani.”
“Thubutu!, wewe au mwingine?”
“Mimi huyuhuyu Mamu, sijawahi kuchemka hasa kwa wazee kama wale.”
“Nakuombea tu dili likubali utakuja kuniambia.”
“Basi nikuache niwahi kijiweni maana mwenzangu umeua tembo kwa ubua mapemaa.”
“Tembo kwa ubua wakati pamechimbika.”
“Kwa heri.”
Mamu alimuaga shogae na kuingia kijiweni kuuza utamu, Adela baada ya kuondoka shoga yake alijigeuza upande wa pili na kuendelea kuutafuta usingizi kutokana na uchovu wa kazi ya asubuhi.
*****
Baada ya siku mbili J4 alimtwangia simu Mamu.
“Haloo mrembo.”
“Nani mwenzangu?” Mamu aliuliza baada ya kuona namba ngeni machoni mwake.
“J4.”
“J4 yupi?”
“Au mrembo hutaki dili?”
“Ooh, sorry mpenzi, namba imenichanganya, niambie mtu wangu?”
“Upo wapi mida hii?”
”Nipo home si unajua nimerudi mida si mirefu.”
“Mmh! Nikikupa dili leo utaweza?”
“Nitaweza kwa nini nishindwe?”
“Wee umekesha utaiweza kasi ya mchezo?”
“Kwani hiyo jana kulikuwa na ishu? Nimeumwa na mbu bure sijafanya kazi yoyote.”
“Basi kama kawaida jipige pamba za ukweli ili babu asijue muuza pipi ya mwili.”
“Kwa hilo shaka ondoa.”
“Nikupe dakika ngapi kujiandaa?”
“Nipe nusu saa.”
“Poa ukimaliza kujiandaa nijulishe.”
“Hakuna tatizo mtu wangu.”
Mamu baada ya kukata simu alikwenda bafuni kuoga kujiandaa kwenda kwa Babu wa Kisemvule. Baada ya kuoga alikaa mbele ya kioo kujitengeneza aonekane si muuza pipi ya mwili bali mtoto wa waziri.
Baada ya kuhakikisha amependeza mbele ya kioo alitafuta suti moja matata na kuivaa kisha alichukua miwani yake ndogo na kuivaa.
“Nimetoka kama waziri na si mtoto wa waziri,” Mamu aliusifia muonekano wake mbele ya kioo kwa sauti ya chini.
Baada ya kuwa na uhakika yupo sawa alimpigia simu J4,
“J4 nipo tayari.”
“Lakini umetoka kimauzo?”
“Zaidi ya mauzo.”
“Poa, nakuja sasa hivi.”
Mamu baada ya kukata simu aliketi kwenye kitanda chake kusubiri kwenda Babu wa Kisemvule. Zilipita dakika mbili honi nje ya chumba chake ilimuashiria anaitwa. Alipitia mkoba wake na kutoka taratibu kwa mwenzo wa madaha, alipofika nje alilisogelea gari lililokuwa limefunguliwa mlango na kuingia ndani na gari liliondoka.
“Mamu ni wewe?”
“Ni mimi J4.”
“Mmh! Umempita hata Adela, kweli unaijua biashara.”
“Bila hivi tungekimbia mjini mapema.”
“Huku nje safi, ndani mambo unayaweza?”
“J4, baada ya gemu muulize sijui Babu wa Loliondo nimemfanyaje?.”
“Mamu siyo Mwasapile, huyu ni Babu wa Kisemvule.”
“Haya, uje umuulize Babu wa Kisemvule, leo ataneng’emuka yeye.”
“Na dau najua litapanda.”
“Basi kazi niachie miye, kachezea vyeupe hivi vyekundu vinachafua,” Mamu alizidi kujishebedua.
Gari lilisimama mbele ya ofisi ya Mzee Kuyu, Mamu alifunguliwa mlango na kuongozwa mpaka ndani ya ofisi.
“Karibu mrembo kutana na Mzee Kuyu.”
“Nimefurahi kukutana na babu,” Mamu alisema huku akizunguka meza na kwenda kumlalia kwa nyuma huku akilaza shingo yake begani kwake.
“Mmh! Mjukuu.”
“Babu, jamani babu.”
Mamu alisema kwa sauti ya kubana huku akiingiza mikono kwenye kifua cha mzee Kuyu kutaka kupekecha chuchu. Mzee Kuyu alimdaka mkono na kumvutia mbele, Mamu naye alijilegeza na kumkalia kwenye mapaja.
“Taratibu mrembo, J4 mtangulize kwenye gari nakuja.”
Nini kitaendelea?