Chenji ya rada yaibuka bungeni

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,145
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) jana, ilishindwa kutoa majibu ya

lissu.jpg

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu

Dodoma. Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) jana, ilishindwa kutoa majibu ya moja kwa moja kuhusu ahadi ya Serikali ya kupeleka madawati ya chenji ya rada kwenye halmashauri mbalimbali nchini.

Swali hilo liliulizwa na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ambaye alitaka kujua ni lini Serikali itakamilisha ahadi yake kwa kupeleka madawati 708 kwa kila wilaya yaliyotakiwa kununuliwa kutokana na fedha hizo.

Lissu alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ambako pia kulikuwa na ahadi ya aina hiyo, hakuna hata dawati moja ambalo lilinunuliwa na hajui mpango huo uliishiwa wapi.

Awali, Serikali iliahidi kupeleka madawati 708 kwa baadhi ya halmashauri za wilaya yakiwa katika muundo wa plastiki.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene alisema mpango huo bado upo na kwamba, kuna shule ambazo zilipelekewa madawati kama ilivyotakiwa.

Hata hivyo, alisema atapitia kuangalia ahadi katika baadhi ya maeneo, ikiwamo kupeleka bungeni mkakati maalumu wa Serikali ya Awamu ya Tano utakaohakikisha kuwa tatizo la madawati kwa shule za msingi na sekondari linakwisha.

Sh78.7 bilioni zilizozidi kununulia rada wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu maarufu kama ‘chenji ya rada’ zilirudishwa kwa Serikali ya Tanzania na kampuni ya kutengeneza vifaa vya kivita ya BAE Systems ya Uingereza.

Katika hatua nyingine, Serikali imetoa nafasi kwa baadhi ya wazazi na wadau wengine kuchangia michango ya upatikanaji wa madawati kwa kadri watakavyoona inafaa ilimradi wasisumbue au kufanya michango hiyo iwe kizuizi cha kupeleka watoto shule.

Wito huo ulitolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Stella Manyanya wakati akijibu swali la Mbunge wa Ndanda (Chadema), Cesil Mwambe.

Mbunge huyo alitaka kujua Serikali imejipanga vipi kuhakikisha wanafunzi hawarudishwi shule kwa sababu ya michango ya mlinzi, madawati na chaki.

Naibu waziri alisema hakuna mkuu wa shule ambaye atamrudisha mwanafunzi nyumbani kwa kutolipa michango ya mlinzi, madawati na chaki kwa sababu majukumu hayo ni ya Serikali.

Chenji ya rada yaibuka bungeni

 
Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) jana, ilishindwa kutoa majibu ya

lissu.jpg

Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu

Dodoma. Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) jana, ilishindwa kutoa majibu ya moja kwa moja kuhusu ahadi ya Serikali ya kupeleka madawati ya chenji ya rada kwenye halmashauri mbalimbali nchini.

Swali hilo liliulizwa na Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ambaye alitaka kujua ni lini Serikali itakamilisha ahadi yake kwa kupeleka madawati 708 kwa kila wilaya yaliyotakiwa kununuliwa kutokana na fedha hizo.

Lissu alisema katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ambako pia kulikuwa na ahadi ya aina hiyo, hakuna hata dawati moja ambalo lilinunuliwa na hajui mpango huo uliishiwa wapi.

Awali, Serikali iliahidi kupeleka madawati 708 kwa baadhi ya halmashauri za wilaya yakiwa katika muundo wa plastiki.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), George Simbachawene alisema mpango huo bado upo na kwamba, kuna shule ambazo zilipelekewa madawati kama ilivyotakiwa.

Hata hivyo, alisema atapitia kuangalia ahadi katika baadhi ya maeneo, ikiwamo kupeleka bungeni mkakati maalumu wa Serikali ya Awamu ya Tano utakaohakikisha kuwa tatizo la madawati kwa shule za msingi na sekondari linakwisha.

Sh78.7 bilioni zilizozidi kununulia rada wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu maarufu kama ‘chenji ya rada’ zilirudishwa kwa Serikali ya Tanzania na kampuni ya kutengeneza vifaa vya kivita ya BAE Systems ya Uingereza.

Katika hatua nyingine, Serikali imetoa nafasi kwa baadhi ya wazazi na wadau wengine kuchangia michango ya upatikanaji wa madawati kwa kadri watakavyoona inafaa ilimradi wasisumbue au kufanya michango hiyo iwe kizuizi cha kupeleka watoto shule.

Wito huo ulitolewa na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Stella Manyanya wakati akijibu swali la Mbunge wa Ndanda (Chadema), Cesil Mwambe.

Mbunge huyo alitaka kujua Serikali imejipanga vipi kuhakikisha wanafunzi hawarudishwi shule kwa sababu ya michango ya mlinzi, madawati na chaki.

Naibu waziri alisema hakuna mkuu wa shule ambaye atamrudisha mwanafunzi nyumbani kwa kutolipa michango ya mlinzi, madawati na chaki kwa sababu majukumu hayo ni ya Serikali.

Chenji ya rada yaibuka bungeni

hapo naona hata hajajibu swali. hovyo kabisa.bila shaka hiyo chenji ya rada ilishaliwa tena na hao mafisiem
 
Mh. Lissu mtake Simbachawene orodha ya halmashauri zilizopata madawati hayo hewa. Hakuna hata moja. Na aliyekuwa msimamizi ni Majaliwa ambaye alikuwa tamisemi akishughulikia elimu.
 
Chenji ilishaliwa long time hiyo... ndio maana watu walishauri waingereza watununulie vitu kabisa na sio kurudisha hela!
 
Duuh, hela walizokula kwenye mitumba ya mapangaboi hazijawatosha, aisee hii sasa ni laana
 
Tungepata watu wa kutosha wa kuwapa changamoto hawa viongozi wetu maendeleo katika hii nchi yangeonekana,lakini inasikitisha kuona watu wanabeza yale yanayoibuliwa na wapinzani wameshalewa ahadi tu za wanasiasa ambazo ningine hata hazitekelezeki! Embu waza wananchi tunabanwa mtaan huku maisha magumu watu wanafunga biashara na wengine wanashindwa kufungua biashara makato mengi na biashara hakuna tunatarajia labda baadae mambo yatakuwa mazuri kutokana na pesa zinazokusanywa lakini unaskia kuna chenchi za rada mabilion,pesa iliyopotea kwenye manunuzi ya ndege mabilion,wafanyakazi hewa hatuna tena lakin kuna ongezeko la mabilion watanzania wanajuzwa haya lakin wamerizika sasa lini tutaendelea?mamilion ya watu wanaumia kwa sababu ya watu wawili, watatu, wanne upinzani hauna tatizo siku zote inatakiwa watu wasapoti xana bila kijali we niwa itikadi gani ni kwa maslai ya nchi kiongozi ajue anawananchi makini kwamba nikikosea hatua moja tu watu wanaiona hizo pesa zilizopotea hapo tu zinatosha kuondoa matatizo sugu ya wananchi
 
Tungepata watu wa kutosha wa kuwapa changamoto hawa viongozi wetu maendeleo katika hii nchi yangeonekana,lakini inasikitisha kuona watu wanabeza yale yanayoibuliwa na wapinzani wameshalewa ahadi tu za wanasiasa ambazo ningine hata hazitekelezeki! Embu waza wananchi tunabanwa mtaan huku maisha magumu watu wanafunga biashara na wengine wanashindwa kufungua biashara makato mengi na biashara hakuna tunatarajia labda baadae mambo yatakuwa mazuri kutokana na pesa zinazokusanywa lakini unaskia kuna chenchi za rada mabilion,pesa iliyopotea kwenye manunuzi ya ndege mabilion,wafanyakazi hewa hatuna tena lakin kuna ongezeko la mabilion watanzania wanajuzwa haya lakin wamerizika sasa lini tutaendelea?mamilion ya watu wanaumia kwa sababu ya watu wawili, watatu, wanne upinzani hauna tatizo siku zote inatakiwa watu wasapoti xana bila kijali we niwa itikadi gani ni kwa maslai ya nchi kiongozi ajue anawananchi makini kwamba nikikosea hatua moja tu watu wanaiona hizo pesa zilizopotea hapo tu zinatosha kuondoa matatizo sugu ya wananchi
Hii nchi ni umiza kichwa kweli mpaka unachoka
 
Back
Top Bottom