Chenge: Mimi ni tumbili

Chenge: Mimi ni tumbili

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Gazeti la leo la Mwananchi limemnukuu Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge akijiita tumbili. Chenge alikuwa akizungumzia kuhusika kwake kwenye suala la Escrow na uwepo wa taarifa za kuachia ngazi kwake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge.

Akikanusha kuachia ngazi,Chenge alijiita tumbili kwa kusema: "Mimi ni tumbili. Na hata hili nitaliruka". Chenge amekana kuhusika kwa lolote kwenye maovu ya Escrow.

Hata Ngeleja naye amekanusha kujiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge.
 
  • Thanks
Reactions: Gor
huyu ndo kiboko ya ccm anapiga kila dili ccm hawana uwezo wa kumfanya chochote ndo mwandishi wa katiba ya ccm
 
Ataruka.? Sidhani kama anaweza hata kuhojiwa.
 
Ipo siku miti yote itateleza na asijione genius sana,angeipogeza system inayombeba pamoja na u-mbuta wa watz.

Ukimwona nguchiro anakufanyia mbwembwe jua yuko karibu na shimo lake.

Well said mkuu.!!
 
Hao ndiyo wanaojiita wenye nchi.
Wanafanya wanachokitaka kwa muda wanaojiamulia wao wenyewe.
 
Gazeti la leo la Mwananchi limemnukuu Mbunge wa Bariadi Mashariki Andrew Chenge akijiita tumbili. Chenge alikuwa akizungumzia kuhusika kwake kwenye suala la Escrow na uwepo wa taarifa za kuachia ngazi kwake kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge.

Akikanusha kuachia ngazi,Chenge alijiita tumbili kwa kusema: "Mimi ni tumbili. Na hata hili nitaliruka". Chenge amekana kuhusika kwa lolote kwenye maovu ya Escrow.Hata Ngeleja naye amekanusha kujiuzulu uenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge.
Mzee wa madili - Mzee wa mipango - Tuhuma zake ni nyingi tu!!
Rada akaramba akaruka viunzi,
Ndege ya Rais akabugia akaruka viunzi
EPA katia ndani akaruka viunzi
ESCROW kasonda!! sasa hapa hatuna uhakika kama ataruka viunzi kama kawaida yake; kama amejiita Tumbiri hilo ni sahihi kabisa maana tumbili anaweza kuruka toka mti mmoja kwenda mwingine - bila kuhitaji daraja wala kivuko - mnyama huyo ni noma!!

Mzee ni noma!! huna mpinzani inji hii.
 
Dawa yake ni wananchi wa mwanza tu. Juzi alikuja JB BELMONTE wakati anashuka tu kwenye gari watu wakaanza mwizi mwizi mwizi na kujaza watu hasa honi za magari ndo zilitia fora. Akatoa bastora watu wakamwambia kama utakuwa na risasi nyingi basi ni kumi kwahiyo utaua kumi na sisi tunakufanya kama Mabina. Polisi ndo walikuja kunusuru hali na kumchukua atujui alienda wapi. Japo ishu halikupata wa kuiriport lakini ilikuwa tamu kuzidi ya Makongoro Mahanga. Kama ye mwanamume aje tena aone
 
Dawa yake ni wananchi wa mwanza tu. Juzi alikuja JB BELMONTE wakati anashuka tu kwenye gari watu wakaanza mwizi mwizi mwizi na kujaza watu hasa honi za magari ndo zilitia fora. Akatoa bastora watu wakamwambia kama utakuwa na risasi nyingi basi ni kumi kwahiyo utaua kumi na sisi tunakufanya kama Mabina. Polisi ndo walikuja kunusuru hali na kumchukua atujui alienda wapi. Japo ishu halikupata wa kuiriport lakini ilikuwa tamu kuzidi ya Makongoro Mahanga. Kama ye mwanamume aje tena aone
Bastola kwenye kundi la watu 100?
 
Anajisifu si kwamba hajafanya maovu, bali kwamba anafanya maovu na uwezo mkubwa wa kuyaruka anao.

Mafioso.
Mafioso.

Actually anaamini kuwa hata kama kafanya kosa, hakuna wa kumuadhibu
 
Hawa wakubwa wataendelea kuitesa nchi hii wanaemkamata ndie arie chola diri.anaemfunguria mashitaka ndie arieshirika ki namna ya kufanikisha mipango.ivi ninani atakae msaliti mwenzie?jibu hakuna.mwisho ya yote nikubadiri mfumo wa uongozi wote .bila kufanya hivyo tutalalamika mpaka basi.wananchi tubadirike!tafakari
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom