figganigga
Platinum Member
- Oct 17, 2010
- 26,662
- 59,100
Kuna ndugu yangu ni chawa wa CCM(Jina Kapuni) Nilimfungia safari kuuliza kwanini anaunga mkono CCM na Mwenyekiti wa CCM Samia Suluhu Hassan ambaye Mdomo waake haukemei Mauaji wala hajali anaowaongoza wakipotea? Nilienda Iringa kwa Ukali sana. Nia ni tuvunje urafiki na kumblock hadi kwenye memory card. Nikaona nisifanye hivyo biila kumsikiliza.
Akanambia anapost tu apate mkate wake wa kila siku. Kasema vile anavyopost ameandikiwa wala siyo yeye. Aliungwa kwenye Group na kila siku wanapewa hela ya bando na posho. Akasema anamaliza kujenga nyumba. Pia akasema asipopost wenzake watapost tu.
So kasema njaa njaa zake ndo zinamfanya afanye hivyo. Pia mama yake anaumwa hakuna aliyemsaidia kumtibia bali hela za Uchawa.
Ila hapendi Uchawa. Kaomba nimsamehe nisivunje urafiki.. Hata kadi ya chama bado anayo mwaka huu kalipia kabisa Platinum. Kasema anaomba amuokoe mama yake.
Je, nimsamehe na nimuache aendelee kula hela za uchawa? Au Nimle ulimi?
Akanambia anapost tu apate mkate wake wa kila siku. Kasema vile anavyopost ameandikiwa wala siyo yeye. Aliungwa kwenye Group na kila siku wanapewa hela ya bando na posho. Akasema anamaliza kujenga nyumba. Pia akasema asipopost wenzake watapost tu.
So kasema njaa njaa zake ndo zinamfanya afanye hivyo. Pia mama yake anaumwa hakuna aliyemsaidia kumtibia bali hela za Uchawa.
Ila hapendi Uchawa. Kaomba nimsamehe nisivunje urafiki.. Hata kadi ya chama bado anayo mwaka huu kalipia kabisa Platinum. Kasema anaomba amuokoe mama yake.
Je, nimsamehe na nimuache aendelee kula hela za uchawa? Au Nimle ulimi?