CHAUMMA mpo?

CHAUMA mlikuja na nguvu ya kutisha. Naona pumzi imekata. Labda sababu ya maokoto. Mikutano haipo kama vile Chama kimekufa. Amkeni tunawasubiri.
Abdul amesitisha huduma, aliwastukia kuwa wasingetoboa hivyo alikuwa anatoa hela hatua kwa hatua hapo walipofikia amejiridhisha kuwa hawabebeki kwani hata kupewa majimbo yale ya nusu mkate italeta zogo kubwa kwa sababu hawaungwi mkono kabisa.
 
Chama kilikula ufadhili wa mifwedha kwa makubaliano kuwa mwamba naye atakuwa mkunja ngumi/mla ubwabwa,,,, mambo yamekuwa tofauti, wafadhili wamekula kona ,,,,,

Yaani wamwage pesa zao kwa ushawishi na kina kigaila ? Catherine? Salum mwalimu ? Mlevi mrema ? Wamepita hivi ,,,, !
 
Wale walidanganywa na ng'ambo hii wakaahidiwa makubwa na baadhi yao wakitumiwa wale wagonjwa 19, baada ya kuchomoka kule na kuja huku sisi tukaondoka kwenda matembezi tukiacha wageni kwenye boma
 
Ila wanasiasa hatari, Yaani mmepambana kujenga chama kwa miaka 20+ halafu unakuja kukiacha kisa kashinda usiyempenda, duh huku mkidai demokrasia🤣🤣🤣

Kwa kweli walinishangaza Sana. Na hapo mwanzoni walikuwa wanawashauri upande wa Lissu wasihame chama, ila wao waliposhindwa wakaanza kutafuta viasababu wahame chama. Wanasiasa sio wa kuwaamini.
 
Ilo liko wazo hawana ushawishi wowote.
Walidhani wao ni wakubwa kuliko chama yaani salumu?kigaila?mrema?sijui Catherine who cares
 
siasa za kufuata mkumbo, bora warudi chadema wao au waende ccm kabisa

Kweli kabisa nje ya CHADEMA wao ni watu wadogo Sana. Sijui walifikiria Nini kujiondoa. Maana Susan Kiwanga na Ruge walipigwa Chini kwenye uchaguzi.
 
Ushauri wangu kwa mzee Rungwe, hizo hela weka benki, Kula wali polepole, achana na kampeni, hizo hela watakula hadi vijukuu. Ukifanya kampeni kina Mdee watapita nazo, huwajui wachaga wewe, kiboko yao Lissu tu
Hahaha,
Wanaotoa hizo pesa wanafuatilia kwa karibu, baadhi ya gharama wanalipa direct, na wanaiba humo humo. Ndiyo, ataambulia ila siyo zote
 
CHAUMA mlikuja na nguvu ya kutisha. Naona pumzi imekata. Labda sababu ya maokoto. Mikutano haipo kama vile Chama kimekufa. Amkeni tunawasubiri.
Watoa asali walitegemea wapate nyomi kuliko cdm, badala yake wamejikuta watoa asali wamejikuta wanatoa hela nyingi impact ikiwa ndogo. Wamerudi kwenye drawing board ili waone watoke vipi.
 
Awamu ya kwanza hawakuimaliza, waliishia njiani. Walipanga kuzunguka siku kumi na SITA wakaishia siku Saba na helicopter kuharibika.
Ahaa,,ndio nikaona picha ya chopa imebebwa kwenye roli sikuelewa,kumbe ilikua Chopa yetu Chauma?
 
Hao wacha nao wale keki ya taifa.
Hawana issue yeyote zaidi ya watu kuchukua per diem tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…