Chanzo cha ndoa/mahusiano miaka hii Kutodumu...

Chanzo cha ndoa/mahusiano miaka hii Kutodumu...

Kipindi hiki ni kipindi ambacho

-mwanaume akiongea na mwanamke anaongea hakuna wa kujishusha, kitu ambacho kimsingi chapaswa kufanywa na mwanamke na si mwanaume kama kichwa cha familia.

-Wanawake kujiona wana ubora na kudeserve vitu perfect ambavyo hata kwenye uhalisia wa maisha havipatikani.

-Wanawake wengi kuwa wajuaji, kila kitu anajua(ngumu sana kuishi na mwanamke wa aina hii).

-Maonesho, watu wanapoingia kwenye ndoa wanagundua kuwa ndoa zenyewe hazivutii kama walivyofikiri kumbe ni kwamba kuna tofauti kati ya expectation and the reality of life.
Kwahiyo tatizo ni wanawake si ndio!!!
 
Kwahiyo tatizo ni wanawake si ndio!!!
Habari,kwa upande wa matatizo yanayoletwa na upande wa wanawake hayo ndiyo niliyoweza kuyaona kwa kuwa mimi ni Me.

Waweza funguka kwa upande wako matatizo tunayowaletea sisi kama me, ikiwa wewe ni ke.

Karibu.
 
Mkuu nimeguswa sana na hii thread. najua mambo ya ndoa ni magumu sana lakini naamini kuachana haijawah kuwa ndiyo best solution. hongera pia kwa kuweza wapatanisha. tunajifunza hekima pia kupitia hili.wakati kuna ambao wanafurahia sana ndo za watu kuvunjika kuna wachache wanaumia.mimi namfahamu jamaa ambaye anajitahidi kuhakikisha anavunja ndo ya rafiki yake ili wote wabaki kuwa single. ni jambo la aibu sana. miaka hii ndoa imekuwa mtihani mkubwa sana.



Gafla namkumbuka Joyce Kiria na Mange
 
nilikua nimenuna since morning ila through hii thread imenifanya nikumbuke tulipotoka na huyu chizi wangu..ngoja nimtoe leo akatumbue laki kidogo...
 
Hongera sana mkuu kwa kurudisha uhai kwenye hiyo ndoa iliyokuwa inaelekea kufa.

Pia hongera sana kwao hao wanandoa kwa sababu inaelekea ni watu waelewa na walikuwa wanapendana kweli ndio maana imekuwa rahisi kuelewana na maisha kuendelea.
itakuwa walikuwa anashoot bongo movies
 
ila kitu kinachochangia siku hizi ni hii kampeni ya USAWA WA KIJINSIA
Daah yaani hii kitu huwa siielewagi kabisa Mkuu... na hizi habari za USAWA MCHWARA ndo zinaleta kutokuheshimiana hata mtaani kama mwanamke akipata mafanikio, me naamini female ni INFERIOR kwa male na hiyo ni milele na milele
 
ila kitu kinachochangia siku hizi ni hii kampeni ya USAWA WA KIJINSIA
Daah yaani hii kitu huwa siielewagi kabisa Mkuu... na hizi habari za USAWA MCHWARA ndo zinaleta kutokuheshimiana hata mtaani kama mwanamke akipata mafanikio, me naamini female ni INFERIOR kwa male na hiyo ni milele na milele
 
ni kama mwenzi mmoja umepita tu nlikuwa na wenzangu kadhaa tunajaribu kuinusuru ndoa ya jamaa yetu ambayo ilifungwa miezi 4 iliyopita. imagine miezi 4 tu tena wao wanasema ni mingi sana..wameamua kuachana. ilikuwa ni kazi ngumu sana. siku hiyo tumekaa kuanzia saa kumi jioni moaka saa tisa usiku tunawasihi sana kuwa wasichukue uamuzi huo. si mwanamke si mwanaume wanasema kila mtu ashike hamsini zake na njia yake.

iliniuma nikikumbuka namna tulivyohangaika sana kwa ajili ya harusi ile ya kifahari ya jamaa yetu.walipendeza sana wakisifiwa na kila mtu. miezi miwili hawataki hata kutizamana.kila mtu anaona kama alioa ua kuolewa na shetani.nikarudi nyumbani saa 10 hivi nikiwa nimechoka sana nikakaa tu sebuleni mke wangu akanifuata na kuniuliza kulikoni huko.

machozi yakinitoka nilimweleza x na y wameamua kabisa kuachana. wazaz wao walishakaa nao, viongozi wa dini walsihakaa nao,wazee mbalimbali walishakaa nao.wameshikilia msimamo huo.hakuna anayetaka kujishusha... kila mtu anasema ana uwezo mzuri wa kuishi bila mwenzie.

nlisikitika sana..nlipata neno la kujifunza.nlimtimzama mke wangu sana akiwa amekaa kwenye kochi.sikutaka kuwaza kati yao nani ana makosa. sababu lengo kubwa la tuki lile lilikuwa ni kusuluhisha....sikulala.asubuh sana saa moja jumamosi nikaenda tena nyumban kwao. nilimkuta x amelala sebulen kwenye sofa na mkewe akiwa chumbani. nlimwomba shemeji yangu aje sebuleni baada ya kama dk 20 akawa amefika.

jamaa yangu aliamka akapiga mswaki akarudi tukakaa wote tukiwa hatujui cha kuzungumza.nlikaa tu natizama chini nao wakitizama sehemu walizojua wao. mle ndani kulikuwa kimya sana.hatukuwasha radio wala tv. kulikuwa kimya sana. tuliendelea kukaa vile kwa muda mrefu kiasi. mwishoni nikamwambia mke aanze kuongea tatizo la mumewe ni nini. aliongea mengi sana aliongea mpaka akalia....nikashukuru moyoni kwa hilo.

mwanaume nlimwambia asijibu hata kidogo. kwa lolote ambalo ameongea mke wake yeye anyamaze iwe kweli au si kweli. baadaye aliposema "shem mi nimemaliza" nikamwambia mwanaume asijibu zile hoja. ila naye aleze tatizo ni nini. alizungumza yake mengi pia akafikia akasema amemaliza. nikawaambia kwa kila mtu ambayo ameyasikia kutoka kwa mwenzie aanze kuyatafakari.si kuyapangua,au kujitetea.ayatafakari tu. pia wakumbuke walishakuwa pamoja kwa muda kabla ya kuamua kuoana. je hayakuwepo hayo?kama hayakuwepo kwa nini sasa yapo?

ule ugomvi uliisha..mke akaomba sasa arudi kwao kwa week moja akapumzike then atarudi kwa mumewe waendelee kuishi. mume akaridhia mwanamke akachukua nguo chache tu tofaut na mwanzo alikuwa amefunga kila kitu chake. nlikaa nao mchana tukatoka kwenda kula home kwangu. tukajikuta tumefikia hatua ule ugomvi umekuwa ni utani sasa nao wakitaniana kila mmoja anamwambia angemwacha mwenzie asingepata kama yeye..kwa utani na kicheko. yule dada hakwenda hata kwao tukawa wote mpaka usiku saa tano nikawarudisha kwao...nikawaambia walale wote chumbani ila walale mzungu wa 4 na hamna kugusana..walicheka na yakaisha walilala wakawa mke na mume tena. ni week kadhaa zimepita,

NINI TATIZO LA NDOA ZETU VIJANA? KWA WAKE NA WANAUME TUNAOCHAGUA WENYEWE?
Arrogance!
 
Amini usiamini hamna kitu chenye kutesa watu wengi kama ndoa tena zile za kikatoliki,ni ndoa chache sana zenye aman
 
Mkuuu ,, Watu wengi siku izi hawapitii ile hatua ya uchumba ...yaaaan kujuana ..

Uchumba unasaidia kujua madhaifu yamwenzako ,nini anapenda nann hapendi ,,ufanye nn asikasirike nahata style ya uombaji msamahaa n.k...siku izi hiyo haipo.

Unakuta namwanamke miezi 1-6 tayari ,ndoaa .....sawa matokeo yake nikasheshe balaaa yaaan nipatashika ,,nguo kuchanikaaaa...


LAKINI KAMA MMEKAA UCHUMBA WENU VIZURI NAKWAMUDA MZURI ,,MMEJUANA ,, JAMAN NAWAMBIENI NDOA NITAMU SANAAAAAAAAAAAA.
Ndoa tamu endapo utapata mtu sahihi kwenye ndoa. Kwanza kwenye uchumba wengi huficha madhaifu yao. Hivyo katika hili swala la ndoa ni kama kamali ni wewe kumuomba mungu wako akupe mke/mume sahihi atakaeijenga ndoa yenu ikawa mfano kwa jamii.

Kuna watu wanaishi maisha ya uchumba miaka tisa au zaidi wanakuja kuoana wanashindwa kumaliza hata mwezi wanaachana hapo ndio mtu unabaki unashangaaa.

Kikubwa kumuomba mungu tu na hapa hakuna ujuzi. Ndoa si lele mama ndoa ngumu na ndio mtihani mgumu kuliko yote huwezi kuelewa kirahisi kama hujaingia kwenye ndoa. Raha ya ngoma uingie kati ucheze.

Na unaweza kujuana na mwanaume kwa siku chache au mwanamke mw mungu akakujaalia ukapata aliye mwema na ww mkalisongesha life lenu kwa raha zenu.lakini mimi nakataa kusema uchumba ndio mtajuana tabia si kweli.
 
Hizi mavitu ya Beijing, women empowerment , sijui usawa wa kijinsia wanawake wengi hawajaandaliwa vema kuvipokea.

Wanatumia vibaya kubishana , kudharau, kujiamria mambo ovyo. Tuseme wanawake wamekuwa malimbukeni wa hii makitu

Na wanaume wamekuwa washamba sana wa hii makitu; kutojiamini,kufake uhalisia, waoga sana (badala ya kuchimba

mikwara mizito au mikwara ya kukaa kimya uso wa mbuzi nao wanarushiana maneno na matusi).Basi vurugu tuuuu.

Tukumbuke kuwa wakati mwingine kutengana/kutalikiana ndio njia sahihi ya kuwapa amani na usalama wahusika
 
Mkuuu ,, Watu wengi siku izi hawapitii ile hatua ya uchumba ...yaaaan kujuana ..

Uchumba unasaidia kujua madhaifu yamwenzako ,nini anapenda nann hapendi ,,ufanye nn asikasirike nahata style ya uombaji msamahaa n.k...siku izi hiyo haipo.

Unakuta namwanamke miezi 1-6 tayari ,ndoaa .....sawa matokeo yake nikasheshe balaaa yaaan nipatashika ,,nguo kuchanikaaaa...


LAKINI KAMA MMEKAA UCHUMBA WENU VIZURI NAKWAMUDA MZURI ,,MMEJUANA ,, JAMAN NAWAMBIENI NDOA NITAMU SANAAAAAAAAAAAA.
Point[emoji122] [emoji122] [emoji122]
 
Mmmhhh ndoa ndoana vijana wa sasa hatuwezi kuvumiliana mapungufu yetu
 
Back
Top Bottom