Chanzo cha ndoa/mahusiano miaka hii Kutodumu...

Chanzo cha ndoa/mahusiano miaka hii Kutodumu...

Sodoku

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2016
Posts
1,277
Reaction score
2,933
ni kama mwenzi mmoja umepita tu nlikuwa na wenzangu kadhaa tunajaribu kuinusuru ndoa ya jamaa yetu ambayo ilifungwa miezi 4 iliyopita. imagine miezi 4 tu tena wao wanasema ni mingi sana..wameamua kuachana. ilikuwa ni kazi ngumu sana. siku hiyo tumekaa kuanzia saa kumi jioni moaka saa tisa usiku tunawasihi sana kuwa wasichukue uamuzi huo. si mwanamke si mwanaume wanasema kila mtu ashike hamsini zake na njia yake.

iliniuma nikikumbuka namna tulivyohangaika sana kwa ajili ya harusi ile ya kifahari ya jamaa yetu.walipendeza sana wakisifiwa na kila mtu. miezi miwili hawataki hata kutizamana.kila mtu anaona kama alioa ua kuolewa na shetani.nikarudi nyumbani saa 10 hivi nikiwa nimechoka sana nikakaa tu sebuleni mke wangu akanifuata na kuniuliza kulikoni huko.

machozi yakinitoka nilimweleza x na y wameamua kabisa kuachana. wazaz wao walishakaa nao, viongozi wa dini walsihakaa nao,wazee mbalimbali walishakaa nao.wameshikilia msimamo huo.hakuna anayetaka kujishusha... kila mtu anasema ana uwezo mzuri wa kuishi bila mwenzie.

nlisikitika sana..nlipata neno la kujifunza.nlimtimzama mke wangu sana akiwa amekaa kwenye kochi.sikutaka kuwaza kati yao nani ana makosa. sababu lengo kubwa la tuki lile lilikuwa ni kusuluhisha....sikulala.asubuh sana saa moja jumamosi nikaenda tena nyumban kwao. nilimkuta x amelala sebulen kwenye sofa na mkewe akiwa chumbani. nlimwomba shemeji yangu aje sebuleni baada ya kama dk 20 akawa amefika.

jamaa yangu aliamka akapiga mswaki akarudi tukakaa wote tukiwa hatujui cha kuzungumza.nlikaa tu natizama chini nao wakitizama sehemu walizojua wao. mle ndani kulikuwa kimya sana.hatukuwasha radio wala tv. kulikuwa kimya sana. tuliendelea kukaa vile kwa muda mrefu kiasi. mwishoni nikamwambia mke aanze kuongea tatizo la mumewe ni nini. aliongea mengi sana aliongea mpaka akalia....nikashukuru moyoni kwa hilo.

mwanaume nlimwambia asijibu hata kidogo. kwa lolote ambalo ameongea mke wake yeye anyamaze iwe kweli au si kweli. baadaye aliposema "shem mi nimemaliza" nikamwambia mwanaume asijibu zile hoja. ila naye aleze tatizo ni nini. alizungumza yake mengi pia akafikia akasema amemaliza. nikawaambia kwa kila mtu ambayo ameyasikia kutoka kwa mwenzie aanze kuyatafakari.si kuyapangua,au kujitetea.ayatafakari tu. pia wakumbuke walishakuwa pamoja kwa muda kabla ya kuamua kuoana. je hayakuwepo hayo?kama hayakuwepo kwa nini sasa yapo?

ule ugomvi uliisha..mke akaomba sasa arudi kwao kwa week moja akapumzike then atarudi kwa mumewe waendelee kuishi. mume akaridhia mwanamke akachukua nguo chache tu tofaut na mwanzo alikuwa amefunga kila kitu chake. nlikaa nao mchana tukatoka kwenda kula home kwangu. tukajikuta tumefikia hatua ule ugomvi umekuwa ni utani sasa nao wakitaniana kila mmoja anamwambia angemwacha mwenzie asingepata kama yeye..kwa utani na kicheko. yule dada hakwenda hata kwao tukawa wote mpaka usiku saa tano nikawarudisha kwao...nikawaambia walale wote chumbani ila walale mzungu wa 4 na hamna kugusana..walicheka na yakaisha walilala wakawa mke na mume tena. ni week kadhaa zimepita,

NINI TATIZO LA NDOA ZETU VIJANA? KWA WAKE NA WANAUME TUNAOCHAGUA WENYEWE?
 
Kipindi hiki ni kipindi ambacho

-mwanaume akiongea na mwanamke anaongea hakuna wa kujishusha, kitu ambacho kimsingi chapaswa kufanywa na mwanamke na si mwanaume kama kichwa cha familia.

-Wanawake kujiona wana ubora na kudeserve vitu perfect ambavyo hata kwenye uhalisia wa maisha havipatikani.

-Wanawake wengi kuwa wajuaji, kila kitu anajua(ngumu sana kuishi na mwanamke wa aina hii).

-Maonesho, watu wanapoingia kwenye ndoa wanagundua kuwa ndoa zenyewe hazivutii kama walivyofikiri kumbe ni kwamba kuna tofauti kati ya expectation and the reality of life.
 
Umefanya vyema ku Reconciliate amicably, me nadhani maisha yanapokuwa na mafanikio huwa kila mmoja anataka afanye lake na kusababisha malumbano baina ya wanandoa, ila mara nyingi ni pale mwanamke akifanikiwa zaidi ya mwanaume kwa kipato chake, though nayo mara chache hutokea kwa wanaume malimbukeni wa mafanikio ya haraka...
 
NUKUU; " MKE MWEMA"

1.Cheo cha mtu hupanda,
ukipata mke mwema,
Kula chachu na maganda.
mfano kama mnyama,
Na nyumba iwe kibanda,
si nzuri ya kutazama,
Utaona umewanda,
moyo umekuterema.

2.Mke mwema ni johari,
yenye furaha daima,
Awe hasa na saburi,
na adili na huruma,
Hata ukiwa fakiri,
hutimizi pato jema,
Utajiona tajiri,
maliki dunia nzima.

3.Mke akiwa mbishi,
wa kushindana kusema,
Na majivuno na mashi,
na ulimi wake pima,
Hata kama wala pishi,
wali na kilo ya nyama,
Utajiona waishi,
duniani huna kima.

4.Mke mrembo si hoja,
hili nimekwisha pima,
Nimepima rejareja,
kila jambo kutazama,
Kujumlisha pamoja,
mambo yalivyosimama,
Nikaona kuwa tija,
ndogo kuliko gharama.

5.Awe mwema mke wangu,
nani hapendi kusema?
Wema asili ya ungu,
milele una heshima,
Kuwa wema walimwengu,
ni wajibu na lazima,
Wema dawa ya machungu,
moyoni yanayouma.
 
Kwakweli ndoa sio lelemama, nakumbuka siku moja nilikata shauri nimwambie wife ikiwa atakubali kuachana na mimi nitampa milioni 10 lakini kila nilipowaangalia watoto wangu, nikatafakari maisha watakayoishi baada ya hapo, nikajiona napoteza nguvu zote za mikono yangu niliyoipigania kwa watoto wangu kwa maisha yangu mpaka hapa nilipo, nikatulia.
Lakini kitindamimba atakapofika sekondari nikimpeleka boarding lolote linaweza kutokea.
 
Ndoa ngumu sana km hujawa tayari ni heri kusubiri, ubarikiwe kwa usuluhishi wako
 
Mkuu nimeguswa sana na hii thread. najua mambo ya ndoa ni magumu sana lakini naamini kuachana haijawah kuwa ndiyo best solution. hongera pia kwa kuweza wapatanisha. tunajifunza hekima pia kupitia hili.wakati kuna ambao wanafurahia sana ndo za watu kuvunjika kuna wachache wanaumia.mimi namfahamu jamaa ambaye anajitahidi kuhakikisha anavunja ndo ya rafiki yake ili wote wabaki kuwa single. ni jambo la aibu sana. miaka hii ndoa imekuwa mtihani mkubwa sana.
 
ila kitu kinachochangia siku hizi ni hii kampeni ya USAWA WA KIJINSIA
 
Kwenye ndoa kuna changamoto sana usipokua serious na jambo hilo aisee ni ngumu sana kusonga mbele
 
Hongera sana mkuu kwa kurudisha uhai kwenye hiyo ndoa iliyokuwa inaelekea kufa.

Pia hongera sana kwao hao wanandoa kwa sababu inaelekea ni watu waelewa na walikuwa wanapendana kweli ndio maana imekuwa rahisi kuelewana na maisha kuendelea.
 
ni kama mwenzi mmoja umepita tu nlikuwa na wenzangu kadhaa tunajaribu kuinusuru ndoa ya jamaa yetu ambayo ilifungwa miezi 4 iliyopita. imagine miezi 4 tu tena wao wanasema ni mingi sana..wameamua kuachana. ilikuwa ni kazi ngumu sana. siku hiyo tumekaa kuanzia saa kumi jioni moaka saa tisa usiku tunawasihi sana kuwa wasichukue uamuzi huo. si mwanamke si mwanaume wanasema kila mtu ashike hamsini zake na njia yake.

iliniuma nikikumbuka namna tulivyohangaika sana kwa ajili ya harusi ile ya kifahari ya jamaa yetu.walipendeza sana wakisifiwa na kila mtu. miezi miwili hawataki hata kutizamana.kila mtu anaona kama alioa ua kuolewa na shetani.nikarudi nyumbani saa 10 hivi nikiwa nimechoka sana nikakaa tu sebuleni mke wangu akanifuata na kuniuliza kulikoni huko.

machozi yakinitoka nilimweleza x na y wameamua kabisa kuachana. wazaz wao walishakaa nao, viongozi wa dini walsihakaa nao,wazee mbalimbali walishakaa nao.wameshikilia msimamo huo.hakuna anayetaka kujishusha... kila mtu anasema ana uwezo mzuri wa kuishi bila mwenzie.

nlisikitika sana..nlipata neno la kujifunza.nlimtimzama mke wangu sana akiwa amekaa kwenye kochi.sikutaka kuwaza kati yao nani ana makosa. sababu lengo kubwa la tuki lile lilikuwa ni kusuluhisha....sikulala.asubuh sana saa moja jumamosi nikaenda tena nyumban kwao. nilimkuta x amelala sebulen kwenye sofa na mkewe akiwa chumbani. nlimwomba shemeji yangu aje sebuleni baada ya kama dk 20 akawa amefika.

jamaa yangu aliamka akapiga mswaki akarudi tukakaa wote tukiwa hatujui cha kuzungumza.nlikaa tu natizama chini nao wakitizama sehemu walizojua wao. mle ndani kulikuwa kimya sana.hatukuwasha radio wala tv. kulikuwa kimya sana. tuliendelea kukaa vile kwa muda mrefu kiasi. mwishoni nikamwambia mke aanze kuongea tatizo la mumewe ni nini. aliongea mengi sana aliongea mpaka akalia....nikashukuru moyoni kwa hilo.

mwanaume nlimwambia asijibu hata kidogo. kwa lolote ambalo ameongea mke wake yeye anyamaze iwe kweli au si kweli. baadaye aliposema "shem mi nimemaliza" nikamwambia mwanaume asijibu zile hoja. ila naye aleze tatizo ni nini. alizungumza yake mengi pia akafikia akasema amemaliza. nikawaambia kwa kila mtu ambayo ameyasikia kutoka kwa mwenzie aanze kuyatafakari.si kuyapangua,au kujitetea.ayatafakari tu. pia wakumbuke walishakuwa pamoja kwa muda kabla ya kuamua kuoana. je hayakuwepo hayo?kama hayakuwepo kwa nini sasa yapo?

ule ugomvi uliisha..mke akaomba sasa arudi kwao kwa week moja akapumzike then atarudi kwa mumewe waendelee kuishi. mume akaridhia mwanamke akachukua nguo chache tu tofaut na mwanzo alikuwa amefunga kila kitu chake. nlikaa nao mchana tukatoka kwenda kula home kwangu. tukajikuta tumefikia hatua ule ugomvi umekuwa ni utani sasa nao wakitaniana kila mmoja anamwambia angemwacha mwenzie asingepata kama yeye..kwa utani na kicheko. yule dada hakwenda hata kwao tukawa wote mpaka usiku saa tano nikawarudisha kwao...nikawaambia walale wote chumbani ila walale mzungu wa 4 na hamna kugusana..walicheka na yakaisha walilala wakawa mke na mume tena. ni week kadhaa zimepita,

NINI TATIZO LA NDOA ZETU VIJANA? KWA WAKE NA WANAUME TUNAOCHAGUA WENYEWE?
Ili ndoa yako idumu lazima mambo mawili makuu yafanyike,

Kwanza lazima umfahamu mwenzako
Pili lazima umjue mwenzako

Hapo kwenye kumfaham haiwez kuchukua chini ya miaka minne then mwaka wa tano ndio unaanza kumjua. Na tafsiri halis ya kumjua mwenzako ni kuanza kumwelewa. Tatzo sisi tunataka kufahamiana ktk ndoa tayar na Mara nying tunakwama unapoanza kumjua na kumwelewa MTU wako kwa uhalisia,hapo ndo tatzo kinakuwepo, Ila wale waliofanikiwa kudumu zaid na zaid ktk ndoa asilimia kubwa ni wale waliofanikiwa ktk sekta ya kufahamiana kabla ya ndoa,unakua hakuna kipya zaid inapokuwepo imara.

Ndoa inayodumu ni ile watu waliofaulu compatibility test...(uwiano)ukifel hapa imekula kwako
 
Ndoa jamani sio ngumu,ugumu ni wahusika kutokuelewana na kufahamiana vzr
 
Zipo sababu nyingi ambazo zimekua chanzo cha ndoa nyingi za kipindi hiki kuvunjika au kuwa kwenye hali mbaya.... Me apa ntazungumzia mbili tu ambazo kwangu naona ndo chanzo haswaa..

1;UAMINIFU.... Hili ni tatizo kubwa toka vizazi vya nyuma bt limekua kubwa zaidi na tishio ktk kikazi hiki kutokana mifumo ya maisha tunayoishi kwa sasa.... Kukosekana kwa uaminifu kwenye ndo kunasababishwa na vitu vingi na miongoni vitu ivyo ni mabadiliko ya mitindo ya maisha kutoka kwenye mahusiano ya mwanzo kwenda kwenye ndoa... Mfano; Mwanaume au mwanamke alizoea kumuita mwenzie majina mazuri ya kimahaba wakati wa uchumba ila wanapokua kwenye ndoa majina hayo yanatoweka au huenda walizoea maisha flan ivi ya utani utani au kutoana out mara kwa mara bt wanapoingia kwny ndoa mambo yote hayo yanatoweka, matokea ya mambo hayo mara nyingi kwa ndoa za sasa huwa ni tatizo coz mmoja kati yao anaweza kuhisi labda mwenzie ana mtu mwngine ambaye anafanyia mambo hayo na pengine na yeye bila kujiridhisha kwa kumuuliza mwenzie matokeo yake anaweza kuamua kutafuta namna ya kutuliza nafsi yake nje na ndoa yake na hapo mwisho huwa na matokea yasiyokua mazuri.

2:NDOA ZA ULAZIMA.... Hii imekua kawaida sana kwa vijana wa kizazi chetu kuoana kwa sababu imetokea tu au imewalazimu iwe ivyo.... Waswahili wanasema "Ukimchunguza sana Nguruwe hauwezi kumla" ni kweli msimu huu unaweza kuwa na maana njema kabisa bt linapokuja swala ndoa huna budi kumchunguza nguruwe coz wakat mwingine si kila kila kitu ni mfano wa msemo huu... Historia ya ndoa nyingi zinazovunjika kwa sasa zinabebwa na jambo hili... Imekua kawaida kabisa kwa vijana kuoana bilia kufamiana vyema kutokana na hamu na shauku ya mioyo yao kwa kipindi kifupi sana na mwisho wanapopata nafasi ya kuwa pa1 kwa muda ndipo kila mmoja hujiona hayupo kwenye mikono salama kutokana na kuyabaini mapungufu ya mwenzie na hapi ndipo vurugu huanzia na kufikia hatua ya kutamani kuishi peke ake
 
Misifa, pasua kichwa na vipusa!!!! Wanawake ni tatizo kwa asilimia kubwa.
 
Uvumilivu ni kitu kikubwa sana kwenye ndoa. Pia akili ya kupambanua mambo. Ipo ndoa moja ambayo wenyewe hawaelewani kabisa. Mwanamke anajishusha na kila anapojishusha mwanaume anazidi kumuonea.
Ugomvi wenyewe hauna maana kabisa kwangu mimi. Mwanaume ni yule mtu anayependa kutumia mfumodume. Anamkandamiza mwenzake sana. Jambo hilo limempelekea hata ndugu na majirani kujisikia huruma. Ila mbele ya kadamnasi haonyeshi tabia hiyo. Anavizia wakati ambapo hakuna watu. Tabia ilipozidi ndipo hata ndugu na jamaa walipoona.
Kaka wa binti waliingilia ugomvi na kumwambia shemeji yao hatumii akili kabisa. Anapomnyanyasa binti wa watu anamletea madhara.
Cha ajabu binti amerudi kwa mumewe na sasa mateso anayopata ni hadi mbele za watu kisa jamaa anadai amedharauliwa.
Vitu vya aina hiyo vya kutumia akili tu vinafanya watu waishi kwa mateso! Hizi ndoa hapana kwa kweli.
 
Kitu muhimu ambacho kila mtu anapaswa kujua ni kwamba,''Ndoa sio kwa ajili ya kila mtu''.
 
Mkuuu ,, Watu wengi siku izi hawapitii ile hatua ya uchumba ...yaaaan kujuana ..

Uchumba unasaidia kujua madhaifu yamwenzako ,nini anapenda nann hapendi ,,ufanye nn asikasirike nahata style ya uombaji msamahaa n.k...siku izi hiyo haipo.

Unakuta namwanamke miezi 1-6 tayari ,ndoaa .....sawa matokeo yake nikasheshe balaaa yaaan nipatashika ,,nguo kuchanikaaaa...


LAKINI KAMA MMEKAA UCHUMBA WENU VIZURI NAKWAMUDA MZURI ,,MMEJUANA ,, JAMAN NAWAMBIENI NDOA NITAMU SANAAAAAAAAAAAA.
 
Hatuelewi nini maana ya ndoa. Hilo tu ndilo tatizo.
 
Back
Top Bottom