Kiukweli hiyo kampuni ya wachina kwa sasa inabore sana.
Mimi pia nina king'amuzi cha startimes, kwa siku kadhaa sasa TV yangu kwenye channel nyingi, aidha itaandika no srrvice na kwenye zile channel ambazo angalau zitakuwa zinaonekana, basi ni scratches kibao!
Hiyo kampuni wakati wanafunga mtambo wao hapo Makongo, si walituassure sisi wateja wao kuwa sasa tatizo la kutoonekana vizuri channel, kwa wanaotumia ving'amuzi vya startimes, itakuwa imefika mwisho.
Mbona sasa badala ya kuimprove, mambo ndiyo yamekuwa more worse, sisi wateja tunatuma salaam kwenu startlimes, hizi ni zama za free market, kama hamtataka kuboresha huduma yenu, sisi wateja hatutakuwa na option nyingine zaidi ya kuwakimbia na kuhamia kwenye ving'amuzi vingine.