BASHADA
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 513
- 148
Kipindi cha Hamza Kasongo, mwandishi wa Iringa na makamu wa IPC na mmiliki wa blogu ya francisgodwin ametoa ushahidi kuwa alikuwa akijaribu kupiga picha baada ya Mwangosi kuuawa, polisi wakamnyooshea bunduki akakimbia akapotelea porini msituni. Aliporudi akachukuliwa na dereva wake, akawa anafuatwa na magari mawili kila anapoenda, mwishowe akaingia uchochoro fulani akawapiga chenga alafu akapiga simu redioni kuwajulisha kuwa yuko mochuari ili kuwapoteza polisi ndo pona yake, huenda na yeye angekuwa marehemu.
Update: anasema alitokea msitu wa Sao Hill, dereva wake akamwambia wanakutafuta. Salama yako ondoa label zilizobandikwa kwenye ubavu wa gari ili wasijue kama gari la mwandishi wa habari, wakaondoka ndo wakaanza kufukuziwa. Wakiongeza mwendo jamaa wanaongeza, wakipunguza nao wanapunguza, wakiingia sehemu nao wanaingia. Bila shaka kuna jambo hapo wadau
Update: anasema alitokea msitu wa Sao Hill, dereva wake akamwambia wanakutafuta. Salama yako ondoa label zilizobandikwa kwenye ubavu wa gari ili wasijue kama gari la mwandishi wa habari, wakaondoka ndo wakaanza kufukuziwa. Wakiongeza mwendo jamaa wanaongeza, wakipunguza nao wanapunguza, wakiingia sehemu nao wanaingia. Bila shaka kuna jambo hapo wadau