Nafikiri siku hiyo walitumwa kuua waandishi wa habari. Next time sijui itakuwa nani.... tusipowadhibiti hawa watatufuata hata majumbani mwetu. Nasema tena na tena mbona mashahidi wako wengi tu tume ya nini?
Wananajaribu kuwatisha waandishi wa habari ili inapotokea wanafanya fujo katika mikutano ya CHADEMA waandishi wa habari wasiwe na ujasiri wa kuwapo eneo la tukio kuripoti udhalimu wao. Si mnafamu kuwa hata kinachowatia kiwewe polisi kwa sasa ni picha na video zinazochukuliwa ktk maeneo wanapojaribu kufanya ufedhuli wao? Nadhani wanawatisha wasiwe wanaripoti madudu na picha za polisi hao, ili wafanikishe mipango ya waume zao (ccm) na kuwachafua CHADEMA kuwa ndio wahusika.