Changamoto ya Internet inazidi kuathiri shughuli mbalimbali nchini

Changamoto ya Internet inazidi kuathiri shughuli mbalimbali nchini

tripof

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2024
Posts
853
Reaction score
1,147
Hali ya mtandao wa internet bado ni mbaya sana kiasi cha kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii kuathirika. Hii ni pamoja na Mabenki, Mahospitali, maduka, TRA, Umeme, Mashirika ya ndege, na maeneo mengineo.

Kwa uwekezaji na maeneo ya kiuchumi na kijamii hili liwe funzo kubwa kuwa tunahitaji mawimbi imara ya intenent wengine wanazungumzia starlink au uwekezaji wowote njia ya settelite visaidiae na mkonga vinginevyo tatizo lilikuwa la umeme limeisha linaingia la internet mbona hatuna vision ya maendeleo jamani ni kutesana tu.

Mitandao iko low/slow tufanyeje kazi za maendeleo, Nape na Mawaziri nendeni na kasi ya mama ya kutuletea maendeleo ya kweli.
 
Na inavyoonekana ni sisi tu ndiyo bado tuna hili tatizo kwa ukali sana. Why us? 😳

IMG-20240514-WA0052.jpg
 
Ndiyo maana nchi zilizoendelea nchi kubwa, hawajatupa shimoni matumizi ya simu za mezani zilizopo majumbani, maofisini, mabarabarani, mijini, vijijini, kituo cha Zimamoto na mashambani n.k

Walijua umuhimu wake lakini sisi tumeruka hatua hiyo na kudhani mobile phones zilizo smartphone zenye mitandao ya email ndiyo mtindo wa kisasa pekee wa mawasilisno ya kuaminika kumbe TTCL SIMU walitakiwa kuendelea kutandaza nyaya za simu za mezani kila pahala

1715692584431.png
 
Nyie mmewekeza kwenye UCHAWA hayo ndo Matunda yachumeni mkale kivulini mpande nguvu za kuandika MAPAMBIO!!!!
 
Na inavyoonekana ni sisi tu ndiyo bado tuna hili tatizo kwa ukali sana. Why us? 😳

View attachment 2989986
Kwa sababu TTCL iliambiwa iingie ubia na kampuni za mkongo, ikakataa kwa kusema inanunua cables za Huawei. Tukashindwa hata kufanya Contingency Planning. Elon Musk alitaka kutuunga StarLink, mpaka leo anapigwa danadana.

Wenzetu kama Wakenya waliwahi kuingia ubia na kuweka Contingency Planning.

Ni kati ya maamuzi ya kijinga kabisa kuwahi kutokea.
 
Tumezidiwa hadi na Malawi? Aibu gani hii?
Hii ndiyo status ya mpaka jana jioni na walikuwa hawaja-update bado. Leo sitashangaa kuona wenzetu wote wameshatatua tatizo isipokuwa sisi.

Inavyoonekana sisi, kama ilivyo kawaida yetu, hatuna miundombinu imara wala backup sababu ya urasimu, uzembe na hata upigaji. Na waziri anayehusika yupo tu anabwabwaja huko mitandaoni na "Mama ameagiza tulitatue hili tatizo". Utalitatuaje kama huna miundo mbinu imara wala back up plans? Kisa mama kasema? 😬😬😬
 
Nape ametia hasara kubwa
Sion sababu ya eye kuwepo ofisin
 
Ndiyo tatizo la maamuzi ya kitaalamu kufanywa na wanasiasa ,Elon Mask ndiyo ilikuwa backup ya fiber optic.

Kwenye kutoa huduma lazima uwe na backup ,sisi tunategemea njia moja tu kupata internet inabid tuchukue pia Satelite....Cha msingi huyo elon auze hisa na hao mabwanyenye yanaylinda ugali wao wachukue.
 
Kwa sababu TTCL iliambiwa iingie ubia na kampuni za mkongo, ikakataa kwa kusema inanunua cables za Huawei. Tukashindwa hata kufanya Contingency Planning. Elon Musk alitaka kutuunga StarLink, mpaka leo anapigwa danadana.

Wenzetu kama Wakenya waliwahi kuingia ubia na kuweka Contingency Planning.

Ni kati ya maamuzi ya kijinga kabisa kuwahi kutokea.
Ndiyo maana Wakenya, kwa kiasi kikubwa, tayari wameshatatua tatizo. Sisi ndiyo kwanza wanasiasa wanashindana kutoa matamko utafikiri matamko yao yanasaidia cho chote.

Starlink inasemekana ilishindikana maana akina Vodacom, Airtel, Tigo na wengineo wanaogopa kunyang'anywa (au tuseme kupunguziwa) ulaji wao. Na waziri husika walishamtia kibindoni (ni mtetezi wao mkuu!).

Kwa Tanzania hii ambapo karibu kila kitu huendeshwa kisivyotakiwa sababu ya ufisadi, uzembe na kutojali, hakuna kinachoshangaza.
 
Ndiyo maana nchi zilizoendelea nchi kubwa, hawajatupa shimoni matumizi ya simu za mezani zilizopo majumbani, maofisini, mabarabarani, mijini, vijijini, kituo cha Zimamoto na mashambani n.k

Walijua umuhimu wake lakini sisi tumeruka hatua hiyo na kudhani mobile phones zilizo smartphone zenye mitandao ya email ndiyo mtindo wa kisasa pekee wa mawasilisno ya kuaminika kumbe TTCL SIMU walitakiwa kuendelea kutandaza nyaya za simu za mezani kila pahala

View attachment 2990024
Wameshatupa Ila hawategemei manyaya , ndo tofauti ilipo ( transmission over the air)
 
Ndiyo tatizo la maamuzi ya kitaalamu kufanywa na wanasiasa ,Elon Mask ndiyo ilikuwa backup ya fiber optic.

Kwenye kutoa huduma lazima uwe na backup ,sisi tunategemea njia moja tu kupata internet inabid tuchukue pia Satelite....Cha msingi huyo elon auze hisa na hao mabwanyenye yanaylinda ugali wao wachukue.
Mama anaupiga mwingi
 
Back
Top Bottom