UCL
Member
- Aug 18, 2020
- 8
- 6
Wanaforum, Amani kwenu!
Ilani ya uchaguzi ni mwongozo unaobeba mambo yote yatakayotekelezwa na Chama husika kwa faida ya wananchi kwa kipindi cha miaka mitano (Tanzania). Kwa maneno mengine, Ilani ya uchaguzi ni dira itoayo mwelekeo na utaratibu wa kutekeleza ahadi za chama kwa wananchi.
Katika kipindi hiki cha kampeni, vyama vya siasa vina kazi moja tu ya kushindanisha Ilani zao kwa wananchi ili wachague Ilani inayowafaa. Hii ndiyo dhana halisi ya kuuza sera. Kuwashawishi wananchi wakuchague kwa sababu yako mambo umeahidi kuwatekelezea kwa faida ya maisha yao.
Cha kushangaza, baadhi ya Wagombea wamekuwa wakiuza sera zisizotekelezeka ili mradi tu wachaguliwe. Wanawaadaha wananchi kwa maneno matamumatamu na yenye kutia moyo. Wakishachaguliwa, hakuna wanachokifanya. Bahati mbaya sana wao hurejeana kuomba tena ridhaa ya wananchi ili waendelee kuiongoza Serikali na kuwatumikia wananchi haohao kwa awamu nyingine.
Swali:
Kwa sababu Chama kimefunga mkataba na wananchi na kwa upande wa wananchi wao wametimiza masharti ya mkataba kwa kukipa chama dhamana ya kuiongoza Serikali, inapotokea chama kwa upande wake kimeshindwa kutimiza masharti yaliyomo kwenye mkataba huo, nini kifanyike wadau?
Ilani ya uchaguzi ni mwongozo unaobeba mambo yote yatakayotekelezwa na Chama husika kwa faida ya wananchi kwa kipindi cha miaka mitano (Tanzania). Kwa maneno mengine, Ilani ya uchaguzi ni dira itoayo mwelekeo na utaratibu wa kutekeleza ahadi za chama kwa wananchi.
Katika kipindi hiki cha kampeni, vyama vya siasa vina kazi moja tu ya kushindanisha Ilani zao kwa wananchi ili wachague Ilani inayowafaa. Hii ndiyo dhana halisi ya kuuza sera. Kuwashawishi wananchi wakuchague kwa sababu yako mambo umeahidi kuwatekelezea kwa faida ya maisha yao.
Cha kushangaza, baadhi ya Wagombea wamekuwa wakiuza sera zisizotekelezeka ili mradi tu wachaguliwe. Wanawaadaha wananchi kwa maneno matamumatamu na yenye kutia moyo. Wakishachaguliwa, hakuna wanachokifanya. Bahati mbaya sana wao hurejeana kuomba tena ridhaa ya wananchi ili waendelee kuiongoza Serikali na kuwatumikia wananchi haohao kwa awamu nyingine.
Swali:
Kwa sababu Chama kimefunga mkataba na wananchi na kwa upande wa wananchi wao wametimiza masharti ya mkataba kwa kukipa chama dhamana ya kuiongoza Serikali, inapotokea chama kwa upande wake kimeshindwa kutimiza masharti yaliyomo kwenye mkataba huo, nini kifanyike wadau?