Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA) kimekanusha taarifa zinazomhusisha muuguzi na tukio la kumpasua mgonjwa nyumbani juu ya makochi mkoani Tabora, kikibainisha kuwa mhusika hana sifa wala taaluma ya uuguzi.
Katika taarifa yake kwa umma, TANNA imeeleza kushtushwa na taarifa iliyotolewa hivi karibuni na vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mitandao ya kijamii juu ya taarifa iliyotolewa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akielezea juu ya tukio la mtu anayedaiwa kuwa ni muuguzi aliyemchukua mgonjwa na kwenda kumfanyia upasuaji nyumbani kwake juu ya makochi. Chama hicho kimesema kimefanya ufuatiliaji wa haraka mkoani Tabora na kubaini ukweli tofauti.
Uchunguzi wa awali wa TANNA umebaini kuwa mhusika wa tukio hilo la hatari ni mtumishi wa Idara ya Afya katika Wilaya ya Urambo, anayefanya kazi katika Zahanati ya Kamsekwa. Hata hivyo, imebainika kuwa mhusika huyo anahudumu kwa nafasi ya Mhudumu wa Afya (Health Attendant) na si muuguzi kama ilivyoripotiwa awali.
Soma Mwigulu: Muuguzi Tabora aliyemfanyia mgonjwa upasuaji nyumbani kwake afukuzwe kazi, afikishwe kwenye mkono wa sheria na kufutiwa leseni
“Imethibitika kuwa mhusika aliyefanya kitendo hicho siyo muuguzi na hana sifa wala taaluma yoyote ya uuguzi… kutokana na utambulisho huo, tuhuma hizo hazihusiani na Muuguzi yeyote wala hazioneshi taswira ya utendaji wa Taaluma ya Uuguzi nchini”, imeeleza taarifa hiyo ya TANNA ikieleza kuwa nafasi ya Mhudumu wa Afya ni nafasi inayojitegemea kitaaluma kama ilivyo kwa madaktari na wauguzi wenyewe kwenye sekta ya afya.
Kufuatia mkanganyiko huo wa taarifa, TANNA imetoa wito kwa mamlaka zinazokusanya na kutoa taarifa kwa viongozi wa juu wa kitaifa kujiridhisha kwa kina kuhusu taaluma na nafasi za watuhumiwa kabla ya kuziweka hadharani. Chama hicho kimesisitiza kuwa kuripoti taarifa zisizo na usahihi wa kitaaluma kunadhalilisha wauguzi walio wengi wanaofanya kazi kwa weledi na uzalendo mkubwa.
TANNA imelaani vikali kitendo hicho ikikitaja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya utabibu na sheria za nchi, kwani kimehatarisha maisha ya mwananchi. Chama hicho kimehimiza mwajiri na mamlaka za kisheria kuchukua hatua stahiki dhidi ya mhusika huyo kwa mujibu wa sheria za nchi.
Aidha, chama hicho kimewasihi wauguzi wote nchini kuendelea kuzingatia miongozo ya utumishi wa umma na kuhakikisha huduma za afya zinatolewa katika maeneo rasmi pekee ili kulinda usalama wa wagonjwa
Katika taarifa yake kwa umma, TANNA imeeleza kushtushwa na taarifa iliyotolewa hivi karibuni na vyombo mbalimbali vya habari pamoja na mitandao ya kijamii juu ya taarifa iliyotolewa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba akielezea juu ya tukio la mtu anayedaiwa kuwa ni muuguzi aliyemchukua mgonjwa na kwenda kumfanyia upasuaji nyumbani kwake juu ya makochi. Chama hicho kimesema kimefanya ufuatiliaji wa haraka mkoani Tabora na kubaini ukweli tofauti.
Uchunguzi wa awali wa TANNA umebaini kuwa mhusika wa tukio hilo la hatari ni mtumishi wa Idara ya Afya katika Wilaya ya Urambo, anayefanya kazi katika Zahanati ya Kamsekwa. Hata hivyo, imebainika kuwa mhusika huyo anahudumu kwa nafasi ya Mhudumu wa Afya (Health Attendant) na si muuguzi kama ilivyoripotiwa awali.
Soma Mwigulu: Muuguzi Tabora aliyemfanyia mgonjwa upasuaji nyumbani kwake afukuzwe kazi, afikishwe kwenye mkono wa sheria na kufutiwa leseni
“Imethibitika kuwa mhusika aliyefanya kitendo hicho siyo muuguzi na hana sifa wala taaluma yoyote ya uuguzi… kutokana na utambulisho huo, tuhuma hizo hazihusiani na Muuguzi yeyote wala hazioneshi taswira ya utendaji wa Taaluma ya Uuguzi nchini”, imeeleza taarifa hiyo ya TANNA ikieleza kuwa nafasi ya Mhudumu wa Afya ni nafasi inayojitegemea kitaaluma kama ilivyo kwa madaktari na wauguzi wenyewe kwenye sekta ya afya.
Kufuatia mkanganyiko huo wa taarifa, TANNA imetoa wito kwa mamlaka zinazokusanya na kutoa taarifa kwa viongozi wa juu wa kitaifa kujiridhisha kwa kina kuhusu taaluma na nafasi za watuhumiwa kabla ya kuziweka hadharani. Chama hicho kimesisitiza kuwa kuripoti taarifa zisizo na usahihi wa kitaaluma kunadhalilisha wauguzi walio wengi wanaofanya kazi kwa weledi na uzalendo mkubwa.
TANNA imelaani vikali kitendo hicho ikikitaja kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya utabibu na sheria za nchi, kwani kimehatarisha maisha ya mwananchi. Chama hicho kimehimiza mwajiri na mamlaka za kisheria kuchukua hatua stahiki dhidi ya mhusika huyo kwa mujibu wa sheria za nchi.
Aidha, chama hicho kimewasihi wauguzi wote nchini kuendelea kuzingatia miongozo ya utumishi wa umma na kuhakikisha huduma za afya zinatolewa katika maeneo rasmi pekee ili kulinda usalama wa wagonjwa