Chama cha Kitaifa - A National Party

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,604
1,704
TANU kilikuwa ni chama cha Kitaifa. Kirefu chake cha Tanzania African National Union kilikuwa na maana ya 'Chama cha Kitaifa cha Muungano wa Waafrika'. Hakika Chama hiki kilikuwa na wanachama na viongozi kutoka kila pembe ya Tanzania/Afrika.

Suala hili la utaifa wa chama lilizingatiwa wakati tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Lakini cha ajabu vigezo vililegezwa maana badala ya kusema ili chama kisajiliwe lazima kiwe na wanachama kadhaa kutoka katika kila mkoa, sheria ikasema iwe ni mikoa kadhaa tu. Naamini kuna hitaji la kuirekebisha sheria hii.

Msiniulize kwa nini nimeleta uchambuzi huu wa kihistoria. Kilicho muhimu ni kujenga vyama vya kitaifa. Huu ndio wakati wa kuwa na chama cha kitaifa kinachosimamia demo-krasi-a.
 
TANU kilikuwa ni chama cha Kitaifa. Kirefu chake cha Tanzania African National Union kilikuwa na maana ya 'Chama cha Kitaifa cha Muungano wa Waafrika'. Hakika Chama hiki kilikuwa na wanachama na viongozi kutoka kila pembe ya Tanzania/Afrika.

Suala hili la utaifa wa chama lilizingatiwa wakati tunaingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Lakini cha ajabu vigezo vililegezwa maana badala ya kusema ili chama kisajiliwe lazima kiwe na wanachama kadhaa kutoka katika kila mkoa, sheria ikasema iwe ni mikoa kadhaa tu. Naamini kuna hitaji la kuirekebisha sheria hii.

Msiniulize kwa nini nimeleta uchambuzi huu wa kihistoria. Kilicho muhimu ni kujenga vyama vya kitaifa. Huu ndio wakati wa kuwa na chama cha kitaifa kinachosimamia demo-krasi-a.

Kwanini unajihami tusikuulize, tetea hoja yako bana
kuanzisha chama na kukijenga ni gharama inachukua muda mrefu sheria iko sawa
 
kuanzisha chama na kukijenga ni gharama inachukua muda mrefu sheria iko sawa

Hi sheria iko sawa kivipi? Umeisoma? Hebu angalia hiki kifungu:

10. Conditions for full registration
(1) No political party shall be qualified to be fully registered unless–


(a) it has first been provisionally registered;
(b) it has obtained not less than two hundred members who are qualified to be registered as voters for the purposes of parliamentary elections from each of at least ten Regions of the United Republic out of which at least two Regions are in Tanzania Zanzibar being one Region each from Zanzibar and Pemba;
(c) it has submitted the names of the national leadership of the party and such leadership draws its members from both Tanzania Zanzibar and Mainland Tanzania; and
(d) it has submitted to the Registrar the location of its head office within the United Republic and a postal address to which notices and other communications may be sent.


Wewe unaona hiyo sehemu (b) iko sawa tu? Tanzania ina mikoa 10? Au 22?
 
Back
Top Bottom