Chalinze: CCM yapunguza kasi, CHADEMA yakoleza

Chalinze: CCM yapunguza kasi, CHADEMA yakoleza

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Sijui sababu lakini najionea. Kwasasa CCM imepunguza mno kasi iliyoanza nayo katika kampeni zake za Ubunge hapa Chalinze. Mikutano yake sasa haihamasishi,haivutii,haishawishi.Imegeuka sehemu za kusalimiana na kutaniana.Hakuna sera labda hela. Mgombea,Ridhiwani Kikwete, sasa 'anarelax' bila wasiwasi.Nani amemdanganya kuwa tayari ameshajipatia ushindi???

CHADEMA wao wanaongeza kasi siku hadi siku. Wanapita vijijini na mitaani wakimnadi Mgombea wao Torongey ambaye sasa anazidi kupata nguvu na kusikilizwa. Anajinadi kama anayeomba na kutafut kweli. 'Makamanda' wa CHADEMA nao wanaitumia nafasi ya 'kujisahau' kwa CCM kuendelea kumuuza Mgombea wao.

Hadi muda huu, kimaoni CCM iko mbele.Lakini,kiuchaguzi na kikura bado ni 50/50. Kusuasua kwa CCM kwaweza kuonekana kama dharau kwa wananchi na wao wakaamua kugeukia upande mwingine. Kwakuwa siko vyema sana kiafya kwasasa, naishia hapa na mtazamo wangu huu.


Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Chalinze)
 
Siku moja watu wataelewa tu,utawala wa uonevu utakoma.
 
Sijui sababu lakini najionea. Kwasasa CCM imepunguza mno kasi iliyoanza nayo katika kampeni zake za Ubunge hapa Chalinze. Mikutano yake sasa haihamasishi,haivutii,haishawishi.Imegeuka sehemu za kusalimiana na kutaniana.Hakuna sera labda hela. Mgombea,Ridhiwani Kikwete, sasa 'anarelax' bila wasiwasi.Nani amemdanganya kuwa tayari ameshajipatia ushindi???

CHADEMA wao wanaongeza kasi siku hadi siku. Wanapita vijijini na mitaani wakimnadi Mgombea wao Torongey ambaye sasa anazidi kupata nguvu na kusikilizwa. Anajinadi kama anayeomba na kutafut kweli. 'Makamanda' wa CHADEMA nao wanaitumia nafasi ya 'kujisahau' kwa CCM kuendelea kumuuza Mgombea wao.

Hadi muda huu, kimaoni CCM iko mbele.Lakini,kiuchaguzi na kikura bado ni 50/50. Kusuasua kwa CCM kwaweza kuonekana kama dharau kwa wananchi na wao wakaamua kugeukia upande mwingine. Kwakuwa siko vyema sana kiafya kwasasa, naishia hapa na mtazamo wangu huu.


Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Chalinze)

Si kweli watu wa vijijini achana nao, wale sio wa kuwaamini!
 
Jamaa mna mioyo migumu nyie! Yaani mlivyo mnaweza hata kuishi hata motoni haswa yule macho kumchuzi pamoja na kikono!
 
Chadema hamna hoja na huko mnapoteza muda mavuno yenu itakua aibu tupu chama gani kisichokua na watu wastaarabu ccm ni mafisadi lkn wana nafuu kuliko chadema.
 
2005 baada ya watu kuwa na mawazo kama haya mgando et chaguo la Mungu,ccm waliiba kura kuliko uchaguzi wowote ,historia inaweza ikajirudia hapa.
 
Kwani Chadema haiwezi kushinda? watakaoamua ni wananchi wa Chalinze na siyo familia ya Kikwete
 
Chadema hamna hoja na huko mnapoteza muda mavuno yenu itakua aibu tupu chama gani kisichokua na watu wastaarabu ccm ni mafisadi lkn wana nafuu kuliko chadema.

hebu fafanua hapo kwenye neno USTAARABU?
 
We subiri waone mziki mzigo tukiukosa poa bado si mali yao?ila moto utawaka
 
Back
Top Bottom