Chakula cha Mama Ntilie na utamu wake

Chakula cha Mama Ntilie na utamu wake

Huwa wanapika KWA kutumia nyanya zilizooza na huwa wanaweka amira kwenye wali
 
Unakiona chakula kingi kinapopakuliwa hapo ufaham kuwa wali umechanganywa na hamira unaumuka kinoooma
Kifuatacho sasa ITV,,,tena ule wali binz
 
Kuna siku nilikuwa naweka tinted kwenye gari mitaa ya uswazi njaa ilikuwa inaniuma sana naikawauliza wana wanitafutie chimbo la mamalishe lishe misosi ya hatari. Nilipelekwa chimbo hilo yaani wali wa Nazi unanukia balaa kulikuwa na mboga ya majani ya kunde ilikuwa tamu sijawahi ona pia pilipili yao iliyokuwa katika mfumo kama wa chachandu mixer mbilimbi nilidata. Lawama nawapelekea mgambo wa City kwa kubomoa kile kibanda maana nilirudi nikakuta pamesafishwa mama lishe wote wametimuliwa. Mpaka leo pamoja ya kwamba nimeshawahi kula misosi mpk ya business class ya Emirates na KLM ila yule mamalishe alikonga roho yangu
 
ya leo kali mama, weka nusu....!!

maxresdefault.jpg
 
Kwa maisha ya Kitanzania hakuna mtu ambaye hajawahi kula chakula cha mtaani /vibanda hodi /uchochoroni au kwa jina maarufu 'Mama Ntilie'.

Bei yake huwa ni ya kawaida sana (pengine robo ya chakula cha hotelini) na huwa kinawekwa kingi sana kwa jina maarufu 'cha kushiba'.

Zifuatazo ni sifa au tabia za chakula cha mama ntilie:-

1. Ujazo wake ni mkubwa sana (cha kushiba)

2. Rosti yake (mchuzi wa nyama/samaki) huwa ni mzito sana unaovutia machoni. Masalu hufanya kazi yake.

3. Bei yake huwa inaanzia TZS 800.000 mpk TZS 1.5000 kwa sahani moja

4. Huwa kinagombaniwa sana

5. Bakuli na sahani huwa ni chache sana na huwazinasuuzwa tu na kuwekea chakula cha mlaji mwingine

6. Wapishi wengi huwa wanene

7. Mazingira huwa machafu sana. Ila chakula kitamu

8. Chakula hiki huisha mapema sana

Nini siri ya utamu wa vyakula ambavyo hupikwa sehemu chafuchafu. Hata Kitimoto nae anahusika!

Mimi kipindi naishi buguruni 2005/06 msosi ulikuwa 300 Tsh msela unashiba na tena ukishatia na yale maji ya Kandoro kudadadeki unashiba balaa.
 
Sasa kama pika yao tu huwa wanaipanua Miguu yao huku Magauni yao yakikunjwa hadi Mapajani halafu Masufuria yao nayo yakiwa katikati na hiyo Miguu yao kwanini Chakula chao kisiwe Kitamu? Tunashiba kwa vingi Mkuu We acha tu!
 
Ukizoea kwa mama n'ntilie unaweza usioe elfu 1500 mboga 3 wali kumwaga
aaagh mkuu wife ni Zaidi ya misosi ina maana mamalishe atakupa mbunye, kukufulia nguo, kukupa joto usiku, kukukumbusha kunywa dawa, kukuzalia watoto n.k. Mke ni taasisi sio chakula tu
 
Mtu alieshikwa tumbo la kuhara akiwa stendi ya mabasi huwa anasifia sana jinsi choo cha stendi kilivyomsitili.... uwezo wetu wa kujikuna umeishia hapo, hatuna jinsi ya kuviona vitamu regardless vinaandaliwa na nani au katika mazingira yapi.
 
Mwanza nina chocho moja, Mama ntilie wanapika jioni kwa kuwa mchana wanasumbuliwa na Mgambo.

Chakula ninachopata mchana kwa sh. 5,000/=
Ikifika jioni saa 2:30 usiku kwa Mama ntilie nakipata kwa 2,000/=

Samaki mzuri, ugali mzuri, wali ndiyo usiseme.

Nawakubali sana Mama ntilie, ukiwa vibaya economically ndiyo utaona umuhimu wao.
 
Ukizoea kwa mama n'ntilie unaweza usioe elfu 1500 mboga 3 wali kumwaga
aaagh mkuu wife ni Zaidi ya misosi ina maana mamalishe atakupa mbunye, kukufulia nguo, kukupa joto usiku, kukukumbusha kunywa dawa, kukuzalia watoto n.k. Mke ni taasisi sio chakula tu
 
Umesahau jambo moja mkuu chakula hupikwa mapema asbh kufika saa sita kishakua kiporo usiku ndio kiporo kabisa
 
Wakichambia yale maji ndio wanapikia ndo mana kitamu
 
Bei nafuu na wingi wa chakula,sababu ni tatu, hawalipi kodi kubwa, Ada ndogo ya maeneo ya Biashara, gharama ndogo ya usafi na uendeshaji.

Siyo hawalipi kodi kubwa. hawalipi kodi kabisa na wengi hawana ada ya maeneo ya biashara. Nenda Riveside darajani jioni uone walivyojipanga na vyakula vyao. hadi wali wa buku unapatikana na ni wa kushiba kabisa.
 
Mimi sijawahi kula kwa mama ntilie kwani Nina kinyaa sana, wakitoka chooni hawanawi wanaendelea tu kupika mikono imebeba kinyesi halafu utakuta anashika nyanya anakatakata, ndiyo maana mnasema mchuzi ni mzito halafu mtamu kumbe mnakula mavi, wakati mwingine wanashika tambala la kudekia kula wakati bila kunawa mikono kwa maji na sabuni wanaendelea kushika vyakula, wengine mbaya zaidi wana watoto wachanga kutwa wakiwatawaza watoto mavi halafu hawanawi mikono yao kwa maji yanayotitirika na sabuni

Wewe hujawahi kula kwa mamantilie kwa sababu umetoka famila tajiri au ya kifisadi. lakini wanzania karibu wote wamekula kwa mama ntilie. hadi Maofisa wa serikali wanakula kwa mama Ntilie katika zama hizi za vyuma kulegea.
 
Bora hao mama ntilie wanaopikia pachafu tunawaona nendeni kwenye majiko ya hizo hoteli kubwa mnazoziamini mjionee mtakaa kimy hupika usiku mnene bila kunawa hata uso
 
Back
Top Bottom