GE2025 CHADEMA yaungana na kanisa la Katoliki katika maombi ya Kitaifa

GE2025 CHADEMA yaungana na kanisa la Katoliki katika maombi ya Kitaifa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania wote kushiriki maombi ya Novena Takatifu yanayofanyika chini ya Kanisa Katoliki, ambayo yanahitimishwa tarehe 23 Agosti 2025, kwa lengo la kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.

Katika taarifa kwa umma iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Tanganyika), John Wegesa Heche siku ya Ijumma, chama hicho kimewataka wanachama wake na Watanzania wote kwa ujumla kushirikiana na waumini wa Kanisa Katoliki katika maombi hayo ya kitaifa.

Soma pia: Rais TEC atangaza maombi ya kufunga kuombea haki na amani katika uchaguzi mkuu

“Tukitambua kuwa tarehe 23 Agosti ndio siku ya kuhitmisha maombi haya, Chadema inawaomba Watanzania wote tuungane na waumini wa Kanisa Katoliki, katika maombi ya Novena Takatifu tarehe 23 Agosti 2025, katika kuombea Taifa letu juu ya haki na amani huku tukijua kama kitabu Kitakatifu Biblia inavyosema; Isaya 32:17: "Na kazi ya haki itakuwa ni amani; na matunda ya haki yatakuwa utulivu na tumaini daima”, amesema Heche.

Aidha, Heche amerejea historia ya mapambano ya kisiasa yaliyosimamiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akieleza kuwa Nyerere alihusisha hata nguvu za Mungu katika kudai uhuru wa Tanganyika. Amekumbusha changamoto za kisiasa zilizojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, ikiwemo za mwaka 2019, 2020 na 2024, ambapo chama hicho kimesema kulikuwa na ukiukwaji wa utu na haki za kidemokrasia.

“Kati ya mwaka 1955 hadi 1959 Mwalimu J. K Nyerere alianza kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru wa kisiasa dhidi ya Mkoloni Mwingereza. Aliwaambia Watanganyika kuwa tutamdai Mkoloni Mwingereza atuachie uhuru wetu. Kama atakataa tutaenda Umoja wa Mataifa nao wasipotukubalia tutaenda kulalamika kwa Mungu”.

Kwa mujibu wa Heche, chama hicho kinaamini kuwa maombi ya pamoja yatawajengea Watanzania ujasiri, hekima na mshikamano, akisema: “huu ni wakati wa kuungana kama familia moja ya Watanzania mbele za Mungu, tukimuomba atufungulie njia ya haki, uhuru, na kuheshimu utu wa kila mmoja wetu”.
Screenshot_20250822-200237.png
Screenshot_20250822-200318.png
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania wote kushiriki maombi ya Novena Takatifu yanayofanyika chini ya Kanisa Katoliki, ambayo yanahitimishwa tarehe 23 Agosti 2025, kwa lengo la kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.

Katika taarifa kwa umma iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Tanganyika), John Wegesa Heche siku ya Ijumma, chama hicho kimewataka wanachama wake na Watanzania wote kwa ujumla kushirikiana na waumini wa Kanisa Katoliki katika maombi hayo ya kitaifa.

Soma pia: Rais TEC atangaza maombi ya kufunga kuombea haki na amani katika uchaguzi mkuu

View attachment 3448991

“Tukitambua kuwa tarehe 23 Agosti ndio siku ya kuhitmisha maombi haya, Chadema inawaomba Watanzania wote tuungane na waumini wa Kanisa Katoliki, katika maombi ya Novena Takatifu tarehe 23 Agosti 2025, katika kuombea Taifa letu juu ya haki na amani huku tukijua kama kitabu Kitakatifu Biblia inavyosema; Isaya 32:17: "Na kazi ya haki itakuwa ni amani; na matunda ya haki yatakuwa utulivu na tumaini daima”, amesema Heche.

Aidha, Heche amerejea historia ya mapambano ya kisiasa yaliyosimamiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akieleza kuwa Nyerere alihusisha hata nguvu za Mungu katika kudai uhuru wa Tanganyika. Amekumbusha changamoto za kisiasa zilizojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, ikiwemo za mwaka 2019, 2020 na 2024, ambapo chama hicho kimesema kulikuwa na ukiukwaji wa utu na haki za kidemokrasia.

“Kati ya mwaka 1955 hadi 1959 Mwalimu J. K Nyerere alianza kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru wa kisiasa dhidi ya Mkoloni Mwingereza. Aliwaambia Watanganyika kuwa tutamdai Mkoloni Mwingereza atuachie uhuru wetu. Kama atakataa tutaenda Umoja wa Mataifa nao wasipotukubalia tutaenda kulalamika kwa Mungu”.

Kwa mujibu wa Heche, chama hicho kinaamini kuwa maombi ya pamoja yatawajengea Watanzania ujasiri, hekima na mshikamano, akisema: “huu ni wakati wa kuungana kama familia moja ya Watanzania mbele za Mungu, tukimuomba atufungulie njia ya haki, uhuru, na kuheshimu utu wa kila mmoja wetu”.
Devil worshipers wa buku saba watakuja kutukana hapa mda sio mrefu!!!
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania wote kushiriki maombi ya Novena Takatifu yanayofanyika chini ya Kanisa Katoliki, ambayo yanahitimishwa tarehe 23 Agosti 2025, kwa lengo la kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.

Katika taarifa kwa umma iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Tanganyika), John Wegesa Heche siku ya Ijumma, chama hicho kimewataka wanachama wake na Watanzania wote kwa ujumla kushirikiana na waumini wa Kanisa Katoliki katika maombi hayo ya kitaifa.

Soma pia: Rais TEC atangaza maombi ya kufunga kuombea haki na amani katika uchaguzi mkuu

View attachment 3448991

“Tukitambua kuwa tarehe 23 Agosti ndio siku ya kuhitmisha maombi haya, Chadema inawaomba Watanzania wote tuungane na waumini wa Kanisa Katoliki, katika maombi ya Novena Takatifu tarehe 23 Agosti 2025, katika kuombea Taifa letu juu ya haki na amani huku tukijua kama kitabu Kitakatifu Biblia inavyosema; Isaya 32:17: "Na kazi ya haki itakuwa ni amani; na matunda ya haki yatakuwa utulivu na tumaini daima”, amesema Heche.

Aidha, Heche amerejea historia ya mapambano ya kisiasa yaliyosimamiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akieleza kuwa Nyerere alihusisha hata nguvu za Mungu katika kudai uhuru wa Tanganyika. Amekumbusha changamoto za kisiasa zilizojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, ikiwemo za mwaka 2019, 2020 na 2024, ambapo chama hicho kimesema kulikuwa na ukiukwaji wa utu na haki za kidemokrasia.

“Kati ya mwaka 1955 hadi 1959 Mwalimu J. K Nyerere alianza kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru wa kisiasa dhidi ya Mkoloni Mwingereza. Aliwaambia Watanganyika kuwa tutamdai Mkoloni Mwingereza atuachie uhuru wetu. Kama atakataa tutaenda Umoja wa Mataifa nao wasipotukubalia tutaenda kulalamika kwa Mungu”.

Kwa mujibu wa Heche, chama hicho kinaamini kuwa maombi ya pamoja yatawajengea Watanzania ujasiri, hekima na mshikamano, akisema: “huu ni wakati wa kuungana kama familia moja ya Watanzania mbele za Mungu, tukimuomba atufungulie njia ya haki, uhuru, na kuheshimu utu wa kila mmoja wetu”.
Ni jambo jema kumwomba mungu
 
Wakatoliki wote tukon kwenye maombi kama tulivyoelekezwa bila kujali Chama

Chakandumuz SASA hawana agenda

Hata domokaya wamemsahau kabisa
 
wakati wa maombi ukiisha, tuchukue hatua kuhakikisha tunajinasua na hizi changamoto tunazopitia.
Sala na kazi.
Maana kama ni kuomba, tumeomba sana.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa wito kwa Watanzania wote kushiriki maombi ya Novena Takatifu yanayofanyika chini ya Kanisa Katoliki, ambayo yanahitimishwa tarehe 23 Agosti 2025, kwa lengo la kuliombea taifa amani, haki na mshikamano wa kitaifa.

Katika taarifa kwa umma iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA (Tanganyika), John Wegesa Heche siku ya Ijumma, chama hicho kimewataka wanachama wake na Watanzania wote kwa ujumla kushirikiana na waumini wa Kanisa Katoliki katika maombi hayo ya kitaifa.

Soma pia: Rais TEC atangaza maombi ya kufunga kuombea haki na amani katika uchaguzi mkuu

View attachment 3448991

“Tukitambua kuwa tarehe 23 Agosti ndio siku ya kuhitmisha maombi haya, Chadema inawaomba Watanzania wote tuungane na waumini wa Kanisa Katoliki, katika maombi ya Novena Takatifu tarehe 23 Agosti 2025, katika kuombea Taifa letu juu ya haki na amani huku tukijua kama kitabu Kitakatifu Biblia inavyosema; Isaya 32:17: "Na kazi ya haki itakuwa ni amani; na matunda ya haki yatakuwa utulivu na tumaini daima”, amesema Heche.

Aidha, Heche amerejea historia ya mapambano ya kisiasa yaliyosimamiwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, akieleza kuwa Nyerere alihusisha hata nguvu za Mungu katika kudai uhuru wa Tanganyika. Amekumbusha changamoto za kisiasa zilizojitokeza kwenye chaguzi zilizopita, ikiwemo za mwaka 2019, 2020 na 2024, ambapo chama hicho kimesema kulikuwa na ukiukwaji wa utu na haki za kidemokrasia.

“Kati ya mwaka 1955 hadi 1959 Mwalimu J. K Nyerere alianza kuwahamasisha Watanganyika kudai uhuru wa kisiasa dhidi ya Mkoloni Mwingereza. Aliwaambia Watanganyika kuwa tutamdai Mkoloni Mwingereza atuachie uhuru wetu. Kama atakataa tutaenda Umoja wa Mataifa nao wasipotukubalia tutaenda kulalamika kwa Mungu”.

Kwa mujibu wa Heche, chama hicho kinaamini kuwa maombi ya pamoja yatawajengea Watanzania ujasiri, hekima na mshikamano, akisema: “huu ni wakati wa kuungana kama familia moja ya Watanzania mbele za Mungu, tukimuomba atufungulie njia ya haki, uhuru, na kuheshimu utu wa kila mmoja wetu”.
Hapa ndo wanakoseaga. Wakibwagwa kwenye sandulu wanalalamiko mar oooh wameibiwa. Kumbe hawajui wao ndo wanajimaliza wenyewe. Hivi chama kimekosa kabosa big brains?
 
Heche kafeli kwenye hili big time
Hapa ndo wanakoseaga. Wakibwagwa kwenye sandulu wanalalamiko mar oooh wameibiwa. Kumbe hawajui wao ndo wanajimaliza wenyewe. Hivi chama kimekosa kabosa
 
Hapa ndo wanakoseaga. Wakibwagwa kwenye sandulu wanalalamiko mar oooh wameibiwa. Kumbe hawajui wao ndo wanajimaliza wenyewe. Hivi chama kimekosa kabosa big brains?
wewe mwenye big brain upo wapi
 
Heche kafeli kwenye hili big time
Nakutana na mtu wa kwanza mwenye akili katika hii mada. Wengine wote mpaka Sasa ni takataka tupu.

Kimsingi inafahamika kuwa kanisa Katoliki na chadema lao Moja awamu hii; kuhakikisha mama hatawali kwa amani. Mungu ni wetu sote, atamlinda mama yetu huyu amiiiiiina!
 
Chama de mapadri never ever forever kuongoza nchi
 
Nakutana na mtu wa kwanza mwenye akili katika hii mada. Wengine wote mpaka Sasa ni takataka tupu.

Kimsingi inafahamika kuwa kanisa Katoliki na chadema lao Moja awamu hii; kuhakikisha mama hatawali kwa amani. Mungu ni wetu sote, atamlinda mama yetu huyu amiiiiiina!
Usiniweka kwenye ujinga wako mimi ni mtu nasimamia haki nakosoa bila kujali chama katoliki kawaida kufunga Novena wala sio jambo jipya. Katoliki ni taasisi hipo kwa ajili ya kusimamia haki. Magufuli alipigwa spana na kanisa alipigwa waraka wa pasaka kuhusu utekaji na corona. Magufuli alifika kipindi amejenga kanisa chato kwake ndani lilitakiwa lizinduliwe na Askofu wa katoliki akagoma Askofu wa Ngara ndo mpaka chato alifungiwa passport ya kusafiri huyu Mama ana kwa kipindi ambacho tulikua tunaelekea haikua na ulazima kufungia kanisa la Gwajima. Mama ni raisi wa nchi yeye angempuuza Gwajima na kelele zake bila hata kufunga kanisa sasa tunaenda kwenye uchaguzi. Lazima ujue namna ya kufanya hesabu za siasa Mama angejua tunaelekea kwenye Uchaguzi akapuuza kelele za Gwajima bila kufunga kanisa. Sijui washauri wake
 
Usiniweka kwenye ujinga wako mimi ni mtu nasimamia haki nakosoa bila kujali chama katoliki kawaida kufunga Novena wala sio jambo jipya. Katoliki ni taasisi hipo kwa ajili ya kusimamia haki. Magufuli alipigwa spana na kanisa alipigwa waraka wa pasaka kuhusu utekaji na corona. Magufuli alifika kipindi amejenga kanisa chato kwake ndani lilitakiwa lizinduliwe na Askofu wa katoliki akagoma Askofu wa Ngara ndo mpaka chato alifungiwa passport ya kusafiri huyu Mama ana kwa kipindi ambacho tulikua tunaelekea haikua na ulazima kufungia kanisa la Gwajima. Mama ni raisi wa nchi yeye angempuuza Gwajima na kelele zake bila hata kufunga kanisa sasa tunaenda kwenye uchaguzi. Lazima ujue namna ya kufanya hesabu za siasa Mama angejua tunaelekea kwenye Uchaguzi akapuuza kelele za Gwajima bila kufunga kanisa. Sijui washauri wake
Pole sana
 
TAARIFA KWA UMMA

WARAKA WA WITO WA KUUNGANA NA KANISA KATOLIKI KATIKA SIKU YA KUHITIMISHA MAOMBI YA KULIOMBEA TAIFA LA TANZANIA – AGOSTI 23, 2025

Ndugu Watanzania wenzangu,

Ninawasalimu na kuwatakia amani.

Katika safari ya taifa letu ya kudai haki, demokrasia, na mabadiliko ya kweli, tunatambua umuhimu wa imani na mshikamano wa kiroho. Chadema inafahamu kuwa tangu tarehe 15 Agosti 2025 hadi 23 Agosti 2025, ambayo ni siku ya kuhitimisha maombi, waumini wa Kanisa Katoliki wamekuwa wakifanya maombi ya Novena kuliombea Taifa letu kwa ajili ya amani na haki.

Wanachama na viongozi wetu ambao pia ni waumini wa Kanisa Katoliki, kwa uaminifu wamejiunga katika maombi haya, na chama kimewahimiza kushiriki kikamilifu, tukiheshimu na kuamini maneno haya kutoka katika Biblia, 2 Mambo ya Nyakati 7:14:

"Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kuziacha njia zao mbaya; basi nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao."

Tukitambua kwamba tarehe 23 Agosti ni siku ya kuhitimisha maombi haya, Chadema inawaomba Watanzania wote kuungana na waumini wa Kanisa Katoliki katika maombi ya Novena Takatifu, kuombea Taifa letu juu ya Haki na Amani, tukijua maneno ya Biblia, Isaya 32:17:

"Na kazi ya haki itakuwa ni amani; na matunda ya haki yatakuwa utulivu na tumaini daima."

Kumbuka kwamba tangu mwaka 1955 hadi 1959, Mwalimu J. K. Nyerere alianza kuhamasisha Watanganyika kudai uhuru wa kisiasa dhidi ya ukoloni wa Mwingereza. Aliwaambia Watanganyika: “Tutamdai Mkoloni Mwingereza atuachie uhuru wetu. Kama atakataa, tutaenda Umoja wa Mataifa, na kama bado hatutakubaliwa, tutaenda kumlilia Mungu.”

Mwalimu Nyerere aliongoza mapambano hayo, akikabiliana na kesi za uchochezi, hadi kufanikisha uhuru wa Taifa letu mwaka 1961. Sasa Tanzania ipo katika jitihada za kufanikisha uchaguzi wa haki na huru wa vyama vingi, tukikumbuka changamoto zilizojitokeza katika uchaguzi wa 2019, 2020 na 2024, ambapo haki za msingi za kidemokrasia na binadamu zilikataliwa.

Hivyo, hatuwezi kudai haki pekee yetu; tunahitaji Mungu atupe nguvu za kiroho, akili, maarifa, na uthabiti. Mapambano yetu ni ya haki, na tunayo imani kuwa Mungu atakuwa upande wetu.

Ninawasihi Watanzania wote tuliombee taifa letu liwe mikononi mwa Mungu, tukimwomba atupe:

Hekima na ujasiri wa wananchi katika kudai na kupigania haki na mabadiliko msingi yanayohitajika kwa mustakabali wa taifa.

Amani ya kweli inayojengwa juu ya haki.

Umoja wa wananchi wote, bila kujali dini au itikadi.


Huu ni wakati wa kuungana kama familia moja ya Watanzania mbele za Mungu, tukimuomba atufungulie njia ya haki, uhuru, na kuheshimu utu wa kila mmoja wetu.

Kwa heshima ya Mungu, ninawaomba Watanzania, hasa wanachama wa Chadema, kesho tarehe 23 Agosti 2025, nendeni kwenye ibada na mshiriki maombi haya kwa wingi, tukijumuika na waumini wa Kanisa Katoliki popote walipo. Nina imani kuwa Mungu atatusikia na kutupa nguvu na ujasiri wa kusimamia haki ya taifa letu.

Kwa Pamoja Tuliombe:
"Haki huinua Taifa, bali dhambi ni aibu kwa watu wote." (Mithali 14:34)

John Wegesa Heche
Makamu Mwenyekiti, Tanganyika
22 Agosti 2025
Screenshot_20250822-200237.png

Screenshot_20250822-200318.png
 
Back
Top Bottom