GE2025 CHADEMA yatoa tamko kuhusu sakata la Timu ya Yanga kuchangia Harambee ya CCM

GE2025 CHADEMA yatoa tamko kuhusu sakata la Timu ya Yanga kuchangia Harambee ya CCM

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka Klabu ya Yanga kujiepusha na Siasa na kurejesha Shilingi milioni 100 zinazodaiwa kuchangia kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia GSM Foundation.

Kupitia taarifa iliyotolewa Agosti 15, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi, Brenda Rupia, CHADEMA imesema kitendo cha Yanga kuhusishwa na mchango huo ni kuingiza michezo kwenye siasa, jambo linalokiuka kanuni za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) zinazokataza vilabu kujihusisha na siasa

CHADEMA imesema michezo inapaswa kuunganisha watu wa itikadi na mitazamo tofauti, na si kuwa chombo cha kugawa wananchi. Chama hicho kimeongeza kuwa hatua ya Yanga kusaidia chama kimoja cha siasa ni kuwadhalilisha mashabiki na wanachama wasio na itikadi sawa

Aidha, chama hicho kimewataka viongozi wa Yanga kujitathmini iwapo wana uhalali wa kuongoza taasisi inayokusudiwa kuunganisha Watanzania wote bila kujali tofauti zao za kisiasa.





1755259295701.png


1755259346319.png
 
Tone tone vipi kwani ... hela zote mmepiga mvinyo, wote tumeshuhudia Lema katika ile commercia ya tone amevimba na chupa la Alize huku akijishebedua. acheni ulalamishi Chadomo.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeishutumu Klabu ya Yanga kwa kile kinachodaiwa kuwa mchango wa Shilingi milioni 100 kusaidia kampeni za Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiutaja kama kitendo cha kukiuka kanuni za michezo na kuwagawa wanachama wake.

Katika taarifa yake ya Agosti 15, 2025, CHADEMA kupitia Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi Brenda Rupia, imesema maelezo ya Yanga yaliyotolewa Agosti 14, 2025 kwamba fedha hizo zilitolewa na mdhamini wao GSM kupitia taasisi ya GSM Foundation, yanakinzana na kauli ya awali ya Rais wa klabu hiyo, Mhandisi Hersi Said, aliyenukuliwa akisema Yanga imechangia CCM milioni 100 na GSM bilioni 10.

Soma pia: Hersi itenganishe Yanga na CCM mbali, Kumbuka Neutrality phrase

Screenshot 2025-08-15 052420.png

Chadema kimesema historia ya Yanga kama klabu iliyoasisiwa wakati wa harakati za kudai uhuru inapaswa kuilazimisha kubaki huru kisiasa na kulinda mshikamano wa mashabiki wake wenye itikadi tofauti, badala ya kuunga mkono chama kimoja.

“Kitendo cha Yanga kutumia fedha za wanachama wake ambao wengine sio wanachama wala mashabiki wa CCM, kuzipeleka kukisaidia chama kimoja (CCM) ili kiendelee kubaki madarakani ni kuwadharau wanachama wake wanaoamini kwenye vyama vingine”, taarifa hiyo imesema.
Chama hicho kimeituhumu Yanga kutumia fedha za wanachama wake, akiwemo wasiounga mkono CCM, kwa manufaa ya chama hicho tawala, jambo linalodaiwa pia kukiuka Ibara za 4, 12 na 17 za kanuni za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) zinazokataza vilabu na mashirikisho kujihusisha na siasa.

CHADEMA imetoa wito kwa Yanga kurudisha fedha hizo kwenye mfuko wa klabu, kuomba radhi kwa umma au kutangaza wazi kuwa ni tawi la CCM. Pia imewataka viongozi wa klabu hiyo kujitathmini iwapo wanastahili kuendelea kuongoza taasisi inayopaswa kuwa ishara ya mshikamano wa kitaifa.
 
Mimi ni MWANANCHI KINDAKINDAKI lakini suala la kuchangia chama cha siasa Kwa klabu yetu HAPANA HAPANA HAPANA.
 
Yanga wangefanya kuchangia vyama vyote milioni mia mia, ili waweke usawa na si chama kimoja. Hapo wamekosea sana...wale wengine acha wachangiane wezi kwa wezi. Hizi taasisi zingewaingizia kimya kimya vyama ambavyo vinashiriki uchaguzi...kwa usawa maana hii nchi ni ya vyama vingi na si chama kimoja
 
Kama mnashindwa tu kutofautisha kati ya GSM na Young Africans Sports Club bado mnajiita akili kubwa? FIFA sio wajinga. Wanajua TFF kuna usajili wa Young Africans Sports Club na sio GSM. Pigeni kelele lakini hakuna FIFA itafanya kwa Yanga.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeitaka Klabu ya Yanga kujiepusha na Siasa na kurejesha Shilingi milioni 100 zinazodaiwa kuchangia kampeni za Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia GSM Foundation.

Kupitia taarifa iliyotolewa Agosti 15, 2025 na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi, Brenda Rupia, CHADEMA imesema kitendo cha Yanga kuhusishwa na mchango huo ni kuingiza michezo kwenye siasa, jambo linalokiuka kanuni za Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) zinazokataza vilabu kujihusisha na siasa

CHADEMA imesema michezo inapaswa kuunganisha watu wa itikadi na mitazamo tofauti, na si kuwa chombo cha kugawa wananchi. Chama hicho kimeongeza kuwa hatua ya Yanga kusaidia chama kimoja cha siasa ni kuwadhalilisha mashabiki na wanachama wasio na itikadi sawa

Aidha, chama hicho kimewataka viongozi wa Yanga kujitathmini iwapo wana uhalali wa kuongoza taasisi inayokusudiwa kuunganisha Watanzania wote bila kujali tofauti zao za kisiasa.





CHADEMA nasi tunachosha.. sasa ili naro tunaendelea kulibeba mwezi mzima huku wenzetu wakifanya kampeini
 
Back
Top Bottom