Chadema wilayani Kasulu kunafuka Moshi

Chadema wilayani Kasulu kunafuka Moshi

ISMAIL MKIMBIZI

Senior Member
Joined
Jan 13, 2013
Posts
192
Reaction score
23
Hakika ni kweli CHADEMA Kasulu kunafuka moshi na wakati wowote moto utalipuka. Mwenyekiti wa CHADEMA Kasulu BW Rajabu Bujoro amekuwa akifanya maamuzi yake binafsi kwa matakwa yake bila kufuata taratibu za kikatiba.

Ni ukweli usiopingika, mwenyekiti huyo hatoi Demokrasia ndani ya chama, mfano tazama aliwahi kuteua wagombea udiwani mwaka 2010 kwa mapenzi yake mwenyewe bila kufuata taratibu zozote. Aliwateua makada wawili kutoka CCM kazi ambayo sio ya kwake ambapo kwa kawaida kikatiba wenye mamlaka ya uteuzi wa wagombea kata na jimbo nafasi za udiwani na ubunge huteuliwa na Kamati Tendaji ya Jimbo husika.

Aliwateua makada hao wa CCM ambao ni Bw Mwononyi wa Kabanga kugombea kata ya Msambara na Bw Bomoa kugombea kata ya Kasulu mjini kitu ambacho kilipelekea CHADEMA kushindwa vibaya sana katika nafasi hizo.
Baadaye aliyekuwa kada wa NCCR MAGEUZI Bw. Haruna Kwasakwasa alihamia CHADEMA akamteua kuwa katibu wa chama bila kufuata taratibu za kikatiba nafasi nyeti ambayo sio ya kumpatia mtu baki ambaye hajaiva KI - ITIKADI ZA CHADEMA na hajakitumikia chama.

Kwa kuwa Bw Kwasasa amekalia kiti muhimu na uwezo wake ni mdogo na hajaiva kiitikadi za CHADEMA amekuwa akiendesha mambo ovyo ovyo ikiwa ni pamoja na kutengeneza mifarakano baina ya viongozi na wanachama. Na hii sio siri amekuwa akiropoka yeye na mwenyekiti hadharani akipiga vita baadhi ya wanachama na viongozi.

Tarehe 18.12.2012 Jimbo liliomba kibali katika kituo cha polisi cha wilaya Kasulu ili kufanya mkutano wa hadhara tarehe 22.12.2012 wakakubaliwa. Tarehe 19.12.2012 Jimbo wakatoa taarifa kwa barua kwa uongozi wa ngazi ya wilaya kuwataarifu kuwa kutakuwa na mkutano wa hadhara tarehe 22.12.2012 na mgeni rasmi atakuwa mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Mkoa Kigoma Bw. Jafari Kasisiko. Barua aliipokea Katibu wilaya Bw Haruna Kwasakwasa.

Maandalizi hayo yalifanywa kikamilifu na Jimbo, ajabu na kweli mwenyekiti Bujoro na katibu wake Haruna Kwasakwasa walifanya juhudi za kuzuia mkutano huo usifanyike. Tarehe 21.12.2012 walikimbilia kituo cha polisi wilaya kutoa taarifa ili mkutano uzuiliwe usifanyike, ambapo Mkuu wa Polisi Kasulu aliwaandikia barua Jimbo wafike kituo cha polisi 22.12.2012 saaa 03:00 asubuhi.

Jimbo waliitikia wito wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jimbo Bw Pindu, akifuatana na katibu wa Jimbo Bw. Lukas , Katibu Mwenezi wa Jimbo Bw. Kaijage, Kamanda wa Vijana Bw. Masoud Bigangika pamoja na Katibu wa Baraza la Wazee Bw. Juma Vuruga. Upande wapili wa walalamikaji alikuwa ni Mwenyekiti wa CHADEMA wilaya Kasulu na Katibu wake Bw. Kwasakwasa.

Baada ya vuta ni kuvute mjadala ulifikia mahali ukategemea hekima za Mkuu wa Polisi Kasulu aliyekuwa akisaidiwa na Mkuu wa Upelelezi kushauri mkutano ufanyike na tofauti nyingine zikajadiriwe baadaye katika vikao vya ndani vilivyo halali kikatiba. Mkutano ulifanyika lakini cha ajabu Bw Bujoro na Bw Kwasakwasa hawakuhudhuria japokuwa walialikwa na badala yake walionekana wakilandalanda mitaani wakisikilizia kwa mbali.

Amaa kweli ukistaajabu ya MUSA utaona ya FILAUNI. Tatizo kubwa Bw Bujoro huwa hashauriki. Aliwahi kutamka mwenyewe kwa kauli ya kichochezi juu ya uchomaji wa makanisa. Akihojiwa alisema "... makanisani sio mahali patakatifu, wanaruhusu mabinti kuingia wakiwa uchi ... hivyo ni a halali yachomwe moto.." Aliendelea kuhojiwa ni vipi kiongozi wa chama kutoa matamshi kama hayo huoni ni kosa? Alijibu kuwa anatetea imani yake ya kiisilam.

Moja ya wafanyabiashara waliokuwapo KAHAWANI alimwambia kama anataka kutetea imani yake aachie kiti aende akawe Imamu au Shehe wa msikiti kwa kuwa CHADEMA haina UDINI, UKABILA, RANGI wala JINSI. Sijui Bw. Bujoro kichwa chake kina nini kiasi cha kutojua atamke nini miongoni mwa wanajamii ambapo kuna watu wenye imani tofauti na mitazamo tofauti. Alipoambiwa kuwa amefanya kosa kubwa na afute kauli yake alisema hajakosea kwa kuwa amelisema KAHAWANI na sio JUKWAANI.
 
kama amekshifu kanisa huyu amelaaniwa chama kitammulika! tuhuma zake wakilisha makao makuu kwa hatua zaidi!
 
Mwendo wa chadema ni mzuri sana kiongozi akikiuka katba ya chama nkufukuzwa tu ili mtu akija mwingine ajuwe style ileile kuwa nikikosea utaratbu napigwa chini,naomba hii iendelee ili tujenge utamaduni wa kuwa wazalendo hasa kutumika kwenye uongozi kwa manufa ya umma.
 
Ulichoongea ni kweli mkuu,,mi mwenyewe baada ya kumaliza degree yangu SUA na kurudi kazini kwangu kahama ila nikaomba likizo na kuja nyumbani kimobwa,,nikawa naongea na jamaa zangu hapo kasulu mjini na kuwaambia wategemee 2015 nitagombea kupitia CHADEMA wakanieleza cha msingi kama unania kweli we onana na BUJORO tu,,sasa nikatafakari kugombea ubunge na bujoro wapi na wapi???
Lakini bujoro sishangai kwa hayo yote kwa sababu hana elimu yoyote na chadema najua walimuweka kwa kuwa jamaa alikuwa -mpinzani kwelikweli kipindi cha sanzugwanko wakiwa NCCR japo elimu ndiyo inamtupa mkono,hana uelewa wa mabo coz hata kujifunza kusoma na kuandika alifundishwa na mwalimu mmoja aliyekuwa anamuuzia duka lake miaka ya 2000 wakati ajira za ualimu zilisitishwa kwa muda.
NA HII NDIYO CHANGAMOTO NAMBA MOJA YA CHAMA CHETU YA KUKOSA WASOMI WENGI WAELEWA WA SERA ZA VYAMA NDANI YA NCHI YETU.
 
huu ndio muda wa kusafisha nyumba na kuondoa uchafu wote kama huu kujiweka tayari kupokea majukumu makubwa ya kuongoza dola.
 
Ni kweli mkuu,kiujumla uongozi wa chadema ngazi za wilaya na mikoa haujatulia, kuna taarifa zisizorasmi kuwa kuna baadhi ya viongozi ngazi za wilaya wa chadema wanashirikiana na watu wa ccm,mfano kule kusini wilayani MBINGA mkoani Ruvuma mwenyeki wilaya wa cdm hutoa siri za kwenye vikao kwa wapinzani wao ccm. Chadema kama kweli wanataka kuongoza nchi inabidi wapange vizuri safu zao kuanzia taifa mapaka mtaa na kuondoa masalia wote wanaofanya kazi za ccm!
 
Kama katukana dini rasmi ya CHAMA, basi afukuzwe!
 
Nyie ni wazushi tu, mnaleta tuhuma za uongo ili kujinufaisha, bujoro ameanza siasa za kuijenga chadema mm nikiwa mdogo sana hapo mwenge shule ya msingi, nakumbumbuka alivyokuwa anakamatwa na polisi na kupandisha mlimani mzegamzega wakati huo ofsi za chadema zikiwa barabara ya kigoma, huyo mzee msimsumbue kwa tamaa zenu za madaraka.
Huyo masoud mnaemuita kamanda wa vijana hata darasa la saba hakumaliza, shule alikuwa mtoro namba moja eti leo hii ndo mwenyekiti wa vijana,
 
Bujoro jamaa wa Ruhita ana tuhuma zake nyingi tu, japokuwa alikuwa anatupa lifti tukiwa tunaenda shuleni Mubondo lakini tulikuwa tunamwogopa kishenzi. Jamaa kwa matusi na dharau ni banda. Halafu nasikia alikatazwa kukanyaga DSM, kuna hujuma laiifanya mitaa ya Buguruni, na ndo mwanzo wa kufulia kwake.
 
Bujoro jamaa wa Ruhita ana tuhuma zake nyingi tu, japokuwa alikuwa anatupa lifti tukiwa tunaenda shuleni Mubondo lakini tulikuwa tunamwogopa kishenzi. Jamaa kwa matusi na dharau ni banda. Halafu nasikia alikatazwa kukanyaga DSM, kuna hujuma laiifanya mitaa ya Buguruni, na ndo mwanzo wa kufulia kwake.

Huu ni umbea uliokithiri, buguruni ww unadhani ni ndogo km murusi kiasi cha mtu kukimbilia kasulu? nyie akina Masoud shule yenyewe tena ya msingi imewaashinda na ss mnataka kugeuza chadema km ndo kimbilio lenu la kutoka kimaisha, mlitakiwa msome
 
Hii ni thread ya pili ndani ya week moja humu jf ya kuleta uzushi kuhusu bujoro usio na kichwa wala miguu, jamani jf sio sehemu ya majungu na umbea, mambo hayo pelekeni fb
 
Hii ni thread ya pili ndani ya week moja humu jf ya kuleta uzushi kuhusu bujoro usio na kichwa wala miguu, jamani jf sio sehemu ya majungu na umbea, mambo hayo pelekeni fb

bila shaka utakuwa unalipwa na huyu mjamaa. ni kwamba mahali hapa ni mahali pa kutafakari, kama imekugusa basi unajirekebisha kupitia link hii. lengo ni kuwa na jamii ambayo ni responsible kwa viongozi na wananchi pia. hivyo tuhuma za namna hiyo zinapotolewa, siyo kukimbilia kukanisha, bali tafakari na uchukue hatua.

Bujoro anasifika kwa kuwa na lugha za dharau na matusi, mwulize yeyote wa kasulu atakwambia.
 
Join Date : 13th January 2013

Posts : 1
Rep Power : 0

Likes Received 0
Likes Given 0



JF imekuwa eneo la CHADEMA kutoa madukuduku yao badala ya kutumia vikao!
 
Ni kanisa lipi hilo linaloruhusu mabinti kuingia uchi!!? Asitake kupotosha umma, na hata kama ingekuwa hivyo je uhalali wa kuchoma kanisa wanautoa wapi? Huko misikitini wanapoingia wachawi na majini ndio patakatifu sana?!! Shwain wahed!
 
Haya malalamiko yako ingekuwa vizuri ungeyapeleka Makao Makuu ya Chadema pale Kinondoni.
 
Ni kanisa lipi hilo linaloruhusu mabinti kuingia uchi!!? Asitake kupotosha umma, na hata kama ingekuwa hivyo je uhalali wa kuchoma kanisa wanautoa wapi? Huko misikitini wanapoingia wachawi na majini ndio patakatifu sana?!! Shwain wahed!

Ndugu CHUMACHAKAVU hapa ni mahari pa watu wanaofikiria kwa kina sio wakurupukaji (Home of Great thinkers). Tatizo la uchomaji wa makanisa kaliongea yeye Bujoro kama Bujoro na sio swala kama unavyochanganya waumini wote kwa kusema misikitini kuna majini, wachawi na ndiyo pasipo patakatifu. Nijuavyo mimi Misikitini Makanisani pote ni mahali patakatifu sana tu, naomba ufute mara moja kauli yako ihusishayo masuala ya kidini na uchache wa hoja za kisiasa za muhusika Bujoro kwa mapungufu yake kimaadili, hekima na Imani. Hapa kinachozungumziwa ni hoja za kisiasa kwa faida ya CHADEMA na jamii kwa ujumla ambayo inaamini Uisilamu na Ukristo ni dini safi.
 
Ndugu CHUMACHAKAVU hapa ni mahari pa watu wanaofikiria kwa kina sio wakurupukaji (Home of Great thinkers). Tatizo la uchomaji wa makanisa kaliongea yeye Bujoro kama Bujoro na sio swala kama unavyochanganya waumini wote kwa kusema misikitini kuna majini, wachawi na ndiyo pasipo patakatifu. Nijuavyo mimi Misikitini Makanisani pote ni mahali patakatifu sana tu, naomba ufute mara moja kauli yako ihusishayo masuala ya kidini na uchache wa hoja za kisiasa za muhusika Bujoro kwa mapungufu yake kimaadili, hekima na Imani. Hapa kinachozungumziwa ni hoja za kisiasa kwa faida ya CHADEMA na jamii kwa ujumla ambayo inaamini Uisilamu na Ukristo ni dini safi.
1. kakudanganya nani hapa ni sehemu ya great thinkers only! ni fyongo ngapi zimetemwa,zinatemwa na zitatemwa ndani ya jf? au wewe ni mgeni humu? hicho ni kibwagizo tu cha jf lakini hakiwezi kufilter aina ya members wanao-join humu, nilichokisema ndicho ninachokiamini and you have no right to force me to believe otherwise but you can advise me if you think you have strong points to convince me!

2. sifuti kauli, usifananishe hapa na bungeni.

3. Una uhakika gani kama shehe ponda au shehe ilunga au hata rais kikwete wanaamini kama ukristo ni dini safi? AU una uhakika gani kama mimi au mch. mtikila au askofu malasusa tunaamini kama uislam ni dini safi? usijifanye hujui tatizo la udini lililoigubika jamii yetu sasa kutokana mbegu ya udini-siasa iliyopandwa na jk na chama chake na sasa tunavuna matunda yake!! si kweli kama jamii kwa ujumla inaamini hivyo!
 
Back
Top Bottom