nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
12 APRIL 2012
Na Raphael Okello, Bunda
CHAMA cha Demokrasia na Mae n d e l e o (CHADEMA) kimesisitiza kuwepo kwa serikali ya majimbo ambapo kimewaomba wananchi kuzingatia suala hilo watakapotoa maoni wakati wa mchakato wa uandikaji wa Katiba Mpya.
Akiwahutubia mamia ya wananchi mjini Bunda mkoani Mara hivi karibuni Mbunge
wa Jimbo la Nyamagana Bw. Ezekiel Wenje aliwataka Watanzania kuingiza katika Katiba Mpya ijayo utawala wa majimbo kwa kuwa ndio njia pekee itakayowawezesha wananchikufaidi uwepo wa rasilimali ya nchi.
"Hatuwezi kufaidi rasilimali ya nchi kama mfuko wa taifa utaendelea kuwa mmoja...kwa kuwa wapo viongozi wajanja wanaotumia vibaya mgao huo ambapo fedha nyingi huishia katika mfuko wao huku wananchi wakitaabika," alisema Bw. Wenje.
Alisema zipo kanda ambazo zina rasilimali nyingi lakini hazina maendeleo ambapo alitoa mfano kwa Kanda ya Ziwa ambapo alisema kanda hiyo inamiliki rasilimali nyingi ya taifa ikiwa ni pamoja na rasilimali watu, madini,ziwa, wanyamapori, samaki na zao la pamba lakini kanda hiyo bado iko nyuma katika huduma za jamii na kwamba haina hata Chuo Kikuu kimoja cha Serikali.
Aliwataka wakazi wa Kanda ya Ziwa na kanda zingine kuhakikisha kuwa ajenda hiyo inakuwa ni ya kikatiba na si ya chama cha siasa kwa kuwa inagusa utaifa.
"Idadi ya Watanzania inakadiriwa kufikia milioni 45 na kati ya hao milioni 15 wanatoka kanda ya ziwa...na katika nchi hii mgombea yeyote wa kiti cha urais lazima atafute kupata ukubali kutoka Kanda ya Ziwa ili apate uhakika wa kushinda," alisema Bw. Wenje.
Kwa mjibu wa Bw. Wenje kupitia mgawanyo wa mapato ya rasilimali katika serikali ya majimbo ni asilimia 20 ya mapato yote ndio itakayowasilishwa katika mfuko wa pamoja wa taifa ili kufidia majimbo yenye rasilimali kidogo na shughuli za jumla za umoja wa kitaifa.
Na Raphael Okello, Bunda
CHAMA cha Demokrasia na Mae n d e l e o (CHADEMA) kimesisitiza kuwepo kwa serikali ya majimbo ambapo kimewaomba wananchi kuzingatia suala hilo watakapotoa maoni wakati wa mchakato wa uandikaji wa Katiba Mpya.
Akiwahutubia mamia ya wananchi mjini Bunda mkoani Mara hivi karibuni Mbunge
wa Jimbo la Nyamagana Bw. Ezekiel Wenje aliwataka Watanzania kuingiza katika Katiba Mpya ijayo utawala wa majimbo kwa kuwa ndio njia pekee itakayowawezesha wananchikufaidi uwepo wa rasilimali ya nchi.
"Hatuwezi kufaidi rasilimali ya nchi kama mfuko wa taifa utaendelea kuwa mmoja...kwa kuwa wapo viongozi wajanja wanaotumia vibaya mgao huo ambapo fedha nyingi huishia katika mfuko wao huku wananchi wakitaabika," alisema Bw. Wenje.
Alisema zipo kanda ambazo zina rasilimali nyingi lakini hazina maendeleo ambapo alitoa mfano kwa Kanda ya Ziwa ambapo alisema kanda hiyo inamiliki rasilimali nyingi ya taifa ikiwa ni pamoja na rasilimali watu, madini,ziwa, wanyamapori, samaki na zao la pamba lakini kanda hiyo bado iko nyuma katika huduma za jamii na kwamba haina hata Chuo Kikuu kimoja cha Serikali.
Aliwataka wakazi wa Kanda ya Ziwa na kanda zingine kuhakikisha kuwa ajenda hiyo inakuwa ni ya kikatiba na si ya chama cha siasa kwa kuwa inagusa utaifa.
"Idadi ya Watanzania inakadiriwa kufikia milioni 45 na kati ya hao milioni 15 wanatoka kanda ya ziwa...na katika nchi hii mgombea yeyote wa kiti cha urais lazima atafute kupata ukubali kutoka Kanda ya Ziwa ili apate uhakika wa kushinda," alisema Bw. Wenje.
Kwa mjibu wa Bw. Wenje kupitia mgawanyo wa mapato ya rasilimali katika serikali ya majimbo ni asilimia 20 ya mapato yote ndio itakayowasilishwa katika mfuko wa pamoja wa taifa ili kufidia majimbo yenye rasilimali kidogo na shughuli za jumla za umoja wa kitaifa.