CHADEMA wapokea msaada wa milioni 400

CHADEMA wapokea msaada wa milioni 400

nashauri,mikataba yote iwe wazi na isiwe ni siri,uwe ni mkataba baina ya serikali na serikali,serikali na chama,serikali na mtu binafsi ama chama na chama.
hii itasaidia kuelewa nini mikataba inahitaji na nini tunatakiwa kulipa.
 
Safari hii Slaa sijui atajikopesha shilingi ngapi!

Bora anayejikopesha pesa za chama kuliko wanaogawana kodi letu. Shilling billion 3.5 za safari za Rais zinaliwa na hakuna mtu anayefikishwa mahakamani, wanaficha nini???
 
Watu wanatokwa jasho kwenye majukwaa wakihutubia, wamezeeka lakini bado wanataka kuwa Marais na wako tayari hata kufanya lolote ili waendelee kuwa viongozi wakuu cha chama kwa sababu ya pesa kama hizi.

Siyo ajabu hata wake zao wako tayari kupigana kufa na kupona ili waendelee kupata pesa kama hizi.

SIASA NI BIASHARA BANA.
 
silaha kubwa ya chadema matusi, akili zao hazifikiri zaidi ya hapo
 
acha umbumbu kijana, Sabodo ametoa msaada mara ngapi wakawekeana mkataba?
Umeona zilipoelekea?

Haya sabado alitoa millon 400 kujenga chuo cha kilelea viongozi na vijana wa CHADEMA pale kibaha ..fedha zilitolewa mwaka 2010 hicho chuo umekiona?

Na zile za kwenu mkuu Taswira si mnanunulia kadi za wapiga kura na kulipoa mamluki wa kupiga kura gharama za malazi? Ngoma droo!!! Hii ya wa denishi ni tofauti mkuu, mikataba ya scandinavian countries si ya kuchezea unavyofikiri wewe.
 
Zile pesa za EPA ziliwafikia wanaCCM wote? Pesa za GreenBank nazo je? Meremeta, IPTL nazo pia wewe zilikufikia?

Mkuu vipik2 ngoja tuone kama na zile za kaa mbali na nyara za taifa kama zitawafikia wote!! Ha ha !! Sembuse hizi za mikataba fake ya wawekezaji toka pande za dunia!!! Kuna mingine imesainiwa majuzi yaani kweli sasa wachina wameamua kuja kivingine maana vita ni kati ya Marekani na China kwa sasa!! Kila upande unamega kwa staili yake!! Je yote hii itafikiwa walengwa watanzania? Kama walikuwa wanajali majority mbona umaskini uko pale pale? Hongera CDM kwa kuweka mkataba wazi na kuwa kazi yake ni mradi wa Capacity building kwa vijana!!! Wasije tena mahasimu waanze kuuliza eti visima vya maji viko wapi wakati mkataba unalenga mafunzo!! Akili zao ndogo mkuu. Wasamehe bure.
 
cHADEMA BWANA KINAPENDWA HADI ULAYA, YAANI WALE CCM B WAKIONA HIVYO HAWAAMINI MACHO YAO!
 
acha umbumbu kijana, Sabodo ametoa msaada mara ngapi wakawekeana mkataba?
Umeona zilipoelekea?

Haya sabado alitoa millon 400 kujenga chuo cha kilelea viongozi na vijana wa CHADEMA pale kibaha ..fedha zilitolewa mwaka 2010 hicho chuo umekiona?

mburula mburula mburula mburula mburula...................................
 
CCM imeshapewa mabilioni, lakini haijawahi kuweka hadharani hata sh. 1. "Madai mengine ni kwamba mfanyabiashara Ali Albwardy, ambaye ndiye mmiliki wa Kilimanjaro-Kempinski, “alimwezesha” Kikwete kwa kiasi cha dola milioni moja za Kimarekani (sawa na Sh. 1.6 bilioni), kwa ajili ya shughuli za kutafuta urais mwaka huo." au fuatilia Link hii Rais Jakaya Kikwete aanikwa | Gazeti la MwanaHalisi. LAKINI JAMAA HAKUWEKA HADHARANI HATA THUMNI HADI KAUMBULIWA NA WATAFITI. Haki ya nani nimelimisi MWANAHALISI
 
Ni fedha za kuwanoa vijana, wanawake Zinatoka Denmark, zitasambaa kila kona Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezidi kuongezewa uwezo,baada ya ‘kumwagiwa'Sh. milioni 400 na Chama cha Conservative People's (CPP) cha nchini Denmark. Fedha hizo zimetolewa na chama hicho kwa ajili ya kuwezesha programu ya mafunzo itakayotolewa kwa vijana na wanawake zaidi ya 30,000 wa Chadema ili kuwajengea uwezo wa kisiasa kupitia mafunzo yatakayotolewa na wataalamu wa Chadema na wa kutokaDenmark. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, mafunzo hayo yatatolewa kwa vijana 9,000 na wanawake 9,000 katika awamu ya kwanza. Dk. Slaa alisema awamu ya kwanza ya programu hiyo itatekelezwa kati ya Machi-Desemba,mwaka huu na ya pili itakuwa kuanzia mwakani.

Makubaliano ya ushirikiano wa uendeshaji wa programu hiyo yalitiwa saini katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika MakaoMakuu ya Chadema,jijini Dar es Salaam jana. Yalisainiwa na Dk. Slaa kwa upande wa Chadema, na Mratibu wa Miradi wa CCP, Rolf Aagaard-Svendsen, kwa niaba ya chama chake. Utiaji saini mkataba huo ulishuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Chadema, akiwamo Mwenyekiti wa Baraza la Vijana (Bavicha), John Heche na Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chama hicho, ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum, Naomi Kaihula.

Wengine ni Katibu Mtendaji Ofisi ya Katibu Mkuu wa Chadema, Victor Kimesera;Mkurugenzi wa Organaizesheni na Mafunzo, Benson Kigaila na Ofisa Mwandamizi wa Habari na Uenezi,Erasto Tumbo. Wengine ni Mkurugenziwa Halmashauri na Masuala ya Bunge wa Chama hicho, John Mrema; na Mbunge wa zamani wa Denmark, ambaye ni mwanachama wa CCP, Helle Sjelle.

Dk. Slaa alisema kimsingi, mkataba huo unalenga maeneo mawili; ya vijana kwa maana ya Bavicha na wanawake kwa maana ya awacha. Alisema kinachotaka kufanyika kupitia msaada huo ni kujenga mfumo wa kuwawezesha viongozi wote wa Bavicha na Bawacha kuanzia ngazi ya taifa, kanda na jimbo.

Alisema mafunzo makubwa kama hayo, ambayo yanashuka hadi katika ngazi ya jimbo,hayajawahi kufanyika katika historia ya uhai wa Chadema. "Na kwa ujumla wake katika nchi nzima,tunalenga msaada huu kuwafunza viongozi vijana wapatao 9,000 na zaidi, na akina mama viongozi wa Bawacha wapatao 9,000 na mamia vilevile," alisema Dk. Slaa na kuongeza: "Kwa hiyo ni mpango mkubwa, ambao
unaanza Machi hii hii na utaenda mpaka mwishoni mwa Desemba.

Awamu ya pili itaanza mwaka kesho." lisema Chadema imekuwa ikituhumiwa kuwa imekuwa ikipokea fedha kutoka nje ya nchi kwa lengo la kuitisha maandamano ya kuipinga serikali. Dk. Slaa alisema tuhuma hizo zimekuwa zikienezwa na baadhi ya maofisa wa serikali, ambao wanawajua. Alisema maofisa hao wamekuwa wakifuatilia nyendo za Chadema na baadhi ya viongozi wake, akiwamo yeye kwa nia mbaya ya kukihujumu chama hicho. "Waendelee kutuhujumu. Maana wananizunguka kila siku hapa na tunawajua," alisema Dk. Slaa.

Hata hivyo, alisema tofauti na madai hayo,Chadema na CCP ni wanachama wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Duniani (IDU), ambao lengo lake kuu ni kuhakikisha ustawi wa demokrasia na mfumo wa vyama vingi duniani. Kutokana na hali hiyo,alisema fedha hizo hazikutolewa kwa lengo lingine zaidi ya kuhakikisha ustawi wa demokrasia nchini. Pia alikanusha madai potofu ambayo yamekuwa yakitolewa na baadhi ya watu wanaoihusisha Chadema na ugaidi, akisema mkataba huo umefanyika wazi na kwa kufuata maadiliyote.

Mratibu wa Miradi wa CCP, Rolf alisema wamefurahishwa na utendaji wa Chadema katika kuzungumzia matatizo yanayowakabili wananchi. Alisema kwa utendaji huo mzuri wa Chadema ndiyo maana wameamua kuiunga mkono kwa kuwasaidia fedha hizo.

Rolf alisema msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya Denmark ya kuvisaidia vyama vya siasa vya nchi zinazoendelea. Naye Mwenyekiti wa Bavicha, Heche alisema msaada huo ni fursa kwao ya kufundisha vijana na kuwaandaa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao. "Maana vijijini wamekuwa wakitishiwa kwa sababu hawajui haki zao," alisema Heche na kuongeza: "Programu hii itatusaidia kupata wagombea kuanzia ngazi ya serikali ya mtaa na Uchaguzi Mkuu ujao." Novemba 17, mwaka juzi, Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde, pamoja na mambo mengine, alidai Chadema imekuwa ikitoa vitisho vya kuandamana na kwamba, wapo tayari
kufa kwa ajili ya katiba kutokana na ahadi ya fedha walizopewa na Ujerumani.

Lusinde alisema hayo wakati akichangia Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2011, bungeni, mjini Dodoma. Pia Agosti 12, mwaka jana, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alikaririwa akidai kuwa anao ushahidi kwamba Chadema imekuwa ikiwahadaa wananchi kwa kuwachangisha fedha, huku ikipokea mabilioni ya Shilingi kwa wafadhili kutoka nje.

Nape pia alidai kuwa upo uwezekano wa Chadema kupewa fedha hizo kwa mikataba yenye masharti ya kuiweka nchi rehani. Vilevile, alidai kuwa Chadema inawalaghai wananchi, ina viongozi wasio waaminifu na kwamba iko tayari kuuza nchi kwa uroho wa madaraka. Alitoa kauli hizo wakati Chadema kilipokuwa kinachangisha fedha kutoka kwa wanachama wake kwa ajili ya operesheni ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C).

Kufuatia kauli hizo, Bodi ya Wadhamini wa Chadema iliagiza wanasheria kumwandikia barua Nape kumtaka kukiomba radhi chama hicho. Baadaye, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika,alikaririwa akisema kuwa tayari Nape ameshaandikiwa barua ya kisheria Agosti 24, mwaka jana ya kumtaka aombe radhi na kulipa fidia ya Sh.bilioni 3 kwa matamshi hayo aliyoyaita kuwa ni ya uzushi na uongo.

CHANZO: NIPASHE
 
mbona hela kidogo hiyo?. ccm uchaguzi wa arumeru kikao kimoja walitumia mil 600. mia
 
Kuwanoa kitu gan kilichobutu?
Kwanin vijana na wanawake?
Mashart ya pesa hizo kutolewa au Dernmark wanatoa bure tu?
 
kweli chadema kinapendwa, hadi wazungu wanakikubali
 
​Mkuu, unge-edit basi kuifanya habari isomeke vizuri badala ya kuiacha imekaa kama utenzi.
 
Back
Top Bottom