Manasse
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 352
- 241
Kila siku tukiamka tunapata habari mpya na tunaona matamko ya CHADEMA juu ya kudai kwamba uongozi wa Rais Magufuli sio mzuri haufuati misingi ya utawala bora.
Jambo la kujiuliza ni kwamba, CHADEMA wao wangefanya nini kama wangeshika dola maana kila kukicha hakuna jema kwao.
Kabla ya Mh. Lowassa kuhamia CDM alisikika akisema "Serikali hii inahitaji mtu mwenye maamuzi magumu" ebu tujiulize maamuzi magumu ni yapi na yanafanywaje?
Rais Magufuli alipoingia madarakani tunaona maamuzi magumu aloyafanya ambapo kuanzia awamu ya 2 hadi ya 4 hakuna rais aloyafanya.
1. Kung'oa uongozi wa taasisi mbali mbali kama bandari, TRA, etc.
2. Kuondoa wafanyakazi hewa serikalini.
3. Kuhimiza na kulazimisha kisheria kodi ilipwe na wale wote walokwepa kodi.
4. Mafisadi papa ambao walokuwa wakiibia serikali kupelekwa mahakamani.
5. Wazembe kazini kufukuzwa na si kuhamishwa kama awali.
6. Kuhamia Dodoma (mchakato unaendelea)
Jambo la kujiuliza sisi watanzania.
1. Kama CDM wangeshika dola, ni mambo yapi tofauti na haya ambayo wangefanya ili watanzania tuone kwamba wanatetea maslahi ya taifa.
2. CDM leo wanatetea wafanyabiashara, (jambo jema) lakini wanasema kwamba "Wafanyabiashara wanafunga biashara zao na kuhofia mitaji yao (wanashindwa kufanya biashara zao)."
3. Kuna sheria gani mpya ambayo imepitishwa na bunge inawabana wafanyabiashara baada ya Rais Magufuli kushika dola.
4. Kama leo umefunga biashara yako kwa miezi 8 tu au mwezi mmoja tu tangu mwaka wa fedha uanze, jiulize, wewe ulikuwa mfanyabiashara au mkwepa kodi?
5. Sasa kwanini CHADEMA wanatetea uozo huu?
Hoja za CHADEMA kuwaaminisha watanzania:
CHADEMA wameibuka na hoja ya udikteta lakini kimsingi si kwamba Rais Magufuli anafanya udikteta bali hiyo ni aina ya uongozi ambayo alikuwanayo tangu akiwa waziri na aina hiyo ya uongozi ndiyo ilimfanya mpaka Mh.Mbowe (M/kiti wa kudumu CDM) amsifu Rais Magufuli kwa utendaji wake (jimboni hai) akiwa waziri wa ujenzi lakini leo anamkataa kisa kamshika pabaya anashindwa kupumua.
Udikteta wa CHADEMA.
1. Ni vyema pia watanzania tukajiuliza, kwanini kila anayekuja CHADEMA kama mgombea urais anaishia kuwa katibu mkuu badala ya Mwenyekiti?
2. Mh.Mbowe anazaidi ya miaka15 ya uwenyekiti CHADEMA, je hivyo ndivyo katiba yao isemavyo au ndio kubaka demokrasia?
Maamuzi magumu.
1. Swali>
Maamuzi magumu yangefanywa vipi bila kutumia amri na maelekezo?
2. Swali>
CHADEMA, maamuzi yenu magumu mngeyafanya kwa mtindo gani?
3. Swali>
Mh.Lowassa aliposema nchi hii ilipofikia inahitaji maamuzi magunu, alikuwa anamaanisha nini?
Jambo la kushangaza:
CHADEMA badala ya kuunga mkono maamuzi haya, badala yake wanapinga uongozi mzima wa Rais Magufuli kana kwamba yale walokuwa wakiyadai tangu miaka yote hayajafanyika.
Kudhihirika unafiki wa CHADEMA:
1. Msomi Kubenea ambaye sasa ni mbunge wa ubungo (CDM) aliitumia elimu yake vyema sana kuandika na kuwaelimisha watanzania juu ya madudu alofanya Mh.Lowassa akiwa Waziri Mkuu na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa kuwaaminisha watanzania.
Sasa mh.Lowassa amejiunga CDM, viongozi wale wale wasomi na wanaotetea maslahi ya taifa tena waloshinikiza Mh. Lowassa apelekwe mahakamani, leo wamekana usomi wao kwa njaa zao (wasaka tonge) wanamsafisha Mh. Lowassa tumwone msafi na sisi watanzania tunaojiita wasomi tunakubali hili.
2. Dkt. Slaa naye alizinguka nchi nzima kutangaza ufisadi wa Mh. Lowassa na hili liliwafanya CDM waonekane kuwa chama bora sana Tanzania na kinaweza kushika dola lakini baada ya maamuzi ya mwenye chama (Mh.Mbowe_M/kiti wa kudumu wa CHADEMA) kutoa amri Mh. Lowassa simama hapa, Dkt. slaa akajitoa CDM.
CHADEMA yapoteza dira.
Kutokana na utendaji mzuri wa Rais Magufuli, CHADEMA wamejikuta katika wakati mgumu kiasi cha kufanya mpango wa kukihamisha kinyesi (ref= Dkt slaa) walichokitwaa awali ili wakirejeshe CCM jambo ambalo limekuwa gumu sana maana watanzania wanyonge, sasa wamehuishwa na utendaji mzuri wa Rais Magufuli.
CHADEMA wamekuwa na hoja ambazo hazina kabisa mashiko hivyo basi wamejikuta wakiyengeneza kila aina ya hoja kuwaaminisha watanzania kwamba utendaji wa Rais Magufuli ni mbaya lakini cha ajabu, CHADEMA wamejikuta wanaungwa mkono na watu wachache wenye maslahi ya kifisadi ambao ndio walikuwa kwakwepakodi mahili Tanzania.
Mh.Mbowe ni miongoni mwa wafanyabiashara Tz na kama mnavyofahamu, Tz watu wengi walikuwa wanakwepa kodi lakini baada ya Rais Magufuli kushika dola, wanaostahili kulipa kodi wanalipa bila kukwepa.
Nini CHADEMA mfanye.
1. Acheni siasa za uchochezi na kumuandama Rais Magufuli kwa utendaji wake, angalieni wapi mtaisaidia Tz kwa kujenga na kukosoa kwa nia njema, mkifanya hivi watanzania watawakubali sana.
2. Nendeni majimboni mwenu chocheeni miradi ya maendeleo, leteni sheria mpya kuishauri serikali kwa nia njema, sio kuzunguka kwa nia ya kufanya maandamano badala ya watu kufanya kazi.
3. Fufueni kero za watanzania kama mlivyokuwa mkifanya awali ili mshirikiane na serikali kuleta maendeleo?
Nb: Before u find the direction, u should know first where u are going.
Jambo la kujiuliza ni kwamba, CHADEMA wao wangefanya nini kama wangeshika dola maana kila kukicha hakuna jema kwao.
Kabla ya Mh. Lowassa kuhamia CDM alisikika akisema "Serikali hii inahitaji mtu mwenye maamuzi magumu" ebu tujiulize maamuzi magumu ni yapi na yanafanywaje?
Rais Magufuli alipoingia madarakani tunaona maamuzi magumu aloyafanya ambapo kuanzia awamu ya 2 hadi ya 4 hakuna rais aloyafanya.
1. Kung'oa uongozi wa taasisi mbali mbali kama bandari, TRA, etc.
2. Kuondoa wafanyakazi hewa serikalini.
3. Kuhimiza na kulazimisha kisheria kodi ilipwe na wale wote walokwepa kodi.
4. Mafisadi papa ambao walokuwa wakiibia serikali kupelekwa mahakamani.
5. Wazembe kazini kufukuzwa na si kuhamishwa kama awali.
6. Kuhamia Dodoma (mchakato unaendelea)
Jambo la kujiuliza sisi watanzania.
1. Kama CDM wangeshika dola, ni mambo yapi tofauti na haya ambayo wangefanya ili watanzania tuone kwamba wanatetea maslahi ya taifa.
2. CDM leo wanatetea wafanyabiashara, (jambo jema) lakini wanasema kwamba "Wafanyabiashara wanafunga biashara zao na kuhofia mitaji yao (wanashindwa kufanya biashara zao)."
3. Kuna sheria gani mpya ambayo imepitishwa na bunge inawabana wafanyabiashara baada ya Rais Magufuli kushika dola.
4. Kama leo umefunga biashara yako kwa miezi 8 tu au mwezi mmoja tu tangu mwaka wa fedha uanze, jiulize, wewe ulikuwa mfanyabiashara au mkwepa kodi?
5. Sasa kwanini CHADEMA wanatetea uozo huu?
Hoja za CHADEMA kuwaaminisha watanzania:
CHADEMA wameibuka na hoja ya udikteta lakini kimsingi si kwamba Rais Magufuli anafanya udikteta bali hiyo ni aina ya uongozi ambayo alikuwanayo tangu akiwa waziri na aina hiyo ya uongozi ndiyo ilimfanya mpaka Mh.Mbowe (M/kiti wa kudumu CDM) amsifu Rais Magufuli kwa utendaji wake (jimboni hai) akiwa waziri wa ujenzi lakini leo anamkataa kisa kamshika pabaya anashindwa kupumua.
Udikteta wa CHADEMA.
1. Ni vyema pia watanzania tukajiuliza, kwanini kila anayekuja CHADEMA kama mgombea urais anaishia kuwa katibu mkuu badala ya Mwenyekiti?
2. Mh.Mbowe anazaidi ya miaka15 ya uwenyekiti CHADEMA, je hivyo ndivyo katiba yao isemavyo au ndio kubaka demokrasia?
Maamuzi magumu.
1. Swali>
Maamuzi magumu yangefanywa vipi bila kutumia amri na maelekezo?
2. Swali>
CHADEMA, maamuzi yenu magumu mngeyafanya kwa mtindo gani?
3. Swali>
Mh.Lowassa aliposema nchi hii ilipofikia inahitaji maamuzi magunu, alikuwa anamaanisha nini?
Jambo la kushangaza:
CHADEMA badala ya kuunga mkono maamuzi haya, badala yake wanapinga uongozi mzima wa Rais Magufuli kana kwamba yale walokuwa wakiyadai tangu miaka yote hayajafanyika.
Kudhihirika unafiki wa CHADEMA:
1. Msomi Kubenea ambaye sasa ni mbunge wa ubungo (CDM) aliitumia elimu yake vyema sana kuandika na kuwaelimisha watanzania juu ya madudu alofanya Mh.Lowassa akiwa Waziri Mkuu na kwa kiasi kikubwa alifanikiwa kuwaaminisha watanzania.
Sasa mh.Lowassa amejiunga CDM, viongozi wale wale wasomi na wanaotetea maslahi ya taifa tena waloshinikiza Mh. Lowassa apelekwe mahakamani, leo wamekana usomi wao kwa njaa zao (wasaka tonge) wanamsafisha Mh. Lowassa tumwone msafi na sisi watanzania tunaojiita wasomi tunakubali hili.
2. Dkt. Slaa naye alizinguka nchi nzima kutangaza ufisadi wa Mh. Lowassa na hili liliwafanya CDM waonekane kuwa chama bora sana Tanzania na kinaweza kushika dola lakini baada ya maamuzi ya mwenye chama (Mh.Mbowe_M/kiti wa kudumu wa CHADEMA) kutoa amri Mh. Lowassa simama hapa, Dkt. slaa akajitoa CDM.
CHADEMA yapoteza dira.
Kutokana na utendaji mzuri wa Rais Magufuli, CHADEMA wamejikuta katika wakati mgumu kiasi cha kufanya mpango wa kukihamisha kinyesi (ref= Dkt slaa) walichokitwaa awali ili wakirejeshe CCM jambo ambalo limekuwa gumu sana maana watanzania wanyonge, sasa wamehuishwa na utendaji mzuri wa Rais Magufuli.
CHADEMA wamekuwa na hoja ambazo hazina kabisa mashiko hivyo basi wamejikuta wakiyengeneza kila aina ya hoja kuwaaminisha watanzania kwamba utendaji wa Rais Magufuli ni mbaya lakini cha ajabu, CHADEMA wamejikuta wanaungwa mkono na watu wachache wenye maslahi ya kifisadi ambao ndio walikuwa kwakwepakodi mahili Tanzania.
Mh.Mbowe ni miongoni mwa wafanyabiashara Tz na kama mnavyofahamu, Tz watu wengi walikuwa wanakwepa kodi lakini baada ya Rais Magufuli kushika dola, wanaostahili kulipa kodi wanalipa bila kukwepa.
Nini CHADEMA mfanye.
1. Acheni siasa za uchochezi na kumuandama Rais Magufuli kwa utendaji wake, angalieni wapi mtaisaidia Tz kwa kujenga na kukosoa kwa nia njema, mkifanya hivi watanzania watawakubali sana.
2. Nendeni majimboni mwenu chocheeni miradi ya maendeleo, leteni sheria mpya kuishauri serikali kwa nia njema, sio kuzunguka kwa nia ya kufanya maandamano badala ya watu kufanya kazi.
3. Fufueni kero za watanzania kama mlivyokuwa mkifanya awali ili mshirikiane na serikali kuleta maendeleo?
Nb: Before u find the direction, u should know first where u are going.