CHADEMA wamemsaidia Rais Samia?

CHADEMA wamemsaidia Rais Samia?

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,320
Reaction score
117,613
Kama mnakumbuka Magufuli enzi zake aliwahi kuongea hadharani.

'msini drive'.. mnakumbuka?

Tumewahi jiuliza alikuwa anawaambia kina nani??..kina nani Wana jeuri ya kum drive Rais? Hadi Magufuli aongee kwa style ya kulalamika hadharani?

Bottom line lazima tukubali kuna 'power behind power' ambazo sometimes ni more powerful than the power we see ..

Sasa hapa tunarudi kwa Chadema walikuwa Wana utamaduni mrefu wa kuheshimu hizi 'power behind power'..na walifaidika nazo sana.

Mnakumbuka sakata la bugs wakati ule wa Dr Slaa?Nani walimwambia chumba chake kina bugs?..nyaraka mbalimbali walizokuwa wanapewa wanaibuka nazo?

Kina Zitto hadi wanaokolewa wasikamatwe....kina Lipumba nk.

Kiukweli hii kitu tunaita 'the system' huwa ni nadra Sana kumsaliti Rais anaewasikiliza.....kama walikuwa Wana doubt kama Samia atawasikiliza na Samia amesha prove kuwa anawasikiliza ..basi kwa vyovyote vile Chadema walipaswa na wao kufanya kazi kwa karibu na 'hawa watu' kama zamani.

Je, walipewa go ahead ya kuandaa maaandamano nchi nzima ya kudai katiba?..au walijiamulia wenyewe?..

Chadema hawajui "the system " wasingeruhusu kabisa Rais mpya ayumbishwe ambae ndo kwanza wanahitaji kumsoma na kujua watafanyaje nae kazi apewe nafasi?

Chadema hawajui "the system " priority Yao ya kwanza kabisa nchini ni Amani na Utulivu?

Chadema hawajui "the system" sio Tu Wana jukumu la usalama lakini wao ndo best "proffesionals " kabisa wenye jukumu pia la kujua exactly wananchi wako na mood ipi na wanataka nini kwa sasa?..na vipi Rais akishauriwa vizuri anaweza cheza na upepo kupenyeza agenda za muhimu?

Weaknesses za Samia zilifahamika na system walihitaji Rais azifanyie kazi baadhi ya weaknesses ili iwe rahisi kwa next time ...bahati mbaya Sana Chadema wameenda kuingia mtego mwepesi sana
Hatimae wamemsaidia Samia in the time being.

Samia kwanza Mwanamke.
Pili mzanzibari
Tatu hakuchaguliwa yeye
Nne Outsider ..hakuwa nguli wa siasa za CCM ....

Unaweza ongeza zingine nyingi ..but ilipoanza kuonekana tumepata Rais ambae kila 'mtu anataka kumtikisa na kudeka deka'..
The system walihitaji Rais atoe reaction ya haraka .. message iwe very clear.

"Msilete mchezo"..tutawashughulikia mkijaribu kutikisa nchi.

Sasa why Chadema waliingia huu mtego?

Mbona Mzee Warioba anapambania katiba bila kutishia vurugu??..

Samia ameongeza credit now
Watu wa System now wanajua angalau tuna mtu tukihitaji 'maamuzi magumu'
Hataogopa.... regardless ya mabalozi watasemaje ...mradi jukumu la kwanza kabisa kusimamia usalama wa Taifa halifanyiwi compromise ....

As long as Samia anaenda Sawa na 'the system' ..na Chadema wanafanya siasa zao mbali kabisa na system hakuna ambacho watapata.

Watapewa agenda kama walivyopewa
"Free Mbowe agenda"..ya kuwa keep busy hadi hapo The system watakapo ona sasa ni wakati sahihi kuwepo na mijadala ya katiba mpya.

System wasingeruhusu Rais ambae bado hajapata Ile 'political legitimacy 'abadili katiba... Constitutional legitimacy sio political legitimacy.

Kwa sasa the system wataenda na Samia hadi hapo ambapo ana political legitimacy na mazingira yanaruhusu kuanza kujadili katiba mpya na sio kwenda na upepo wa mitandaoni.

Kama Magufuli alilalama wanam drive.

Chadema walifikiri ni jambo rahisi Rais kwenda against the system?

Hasa wakati akifanya Jambo mnaenda kupiga makelele 'mama anaupiga mwingi'.

Rais anazidi kuonekana anafata Mitandao badala ya kusikiliza ushauri wa "the proffesionals".

Mnazidi kumuonesha ana weakness badala ya kumjenga...mpaka alipowachukulia hatua Chadema now.

Kaanza kuonekana sio that weak.

Ikibidi kufanya 'unpopular decisions'.. atafanya....hiko ni kitu kikubwa mno kwa system.

Swali langu kwa Chadema ..the system mnawasikiliza?Mtaweza kwenda against them kama hata Rais hawezi?
 
Kosa lao ni kama la jamii yetu kumuona Mwanamke ni dhaifu ili hali sio ukweli, yule ni Mwanamke kimaumbile lakini Mwenye Mamlaka ya Juu kuliko yeyote Nchini, Wao walivyoona Jinsia yake na upole wake wakafikiri ni Mwanya wao wa kupata political Milage kupitia Agenda ya Katiba, Miaka 5 walikuwa wametulia tulii na wengine walikimbia, Wamemzingua Mama na Yeye kaamua awazingue kuwakumbusha kuwa Yeye kabla ya Kumuita Mama ni Rais afu majina mengine ndo yatafuata.

kuna Wanaume na Wanawake wengi bila kujali imani zao dini, siasa, Elimu na Majukumu wanajitoa kuhakikisha Ofisi kubwa kwa taifa letu haipotezi Heshima yake kwa Taifa letu na Nchi nyengine, wanatumia nguvu zao, maarifa na hata rasilimali zao binafsi kulinda heshima ya Taasisi ya Urais, Chadema walitaka Kumtikisa Rais sio Mama
 
Samia atalazimika kumpongeza gaidi wa Zambia.
Hata Lungu alikuwa Rais kutoka Opposition. Sasa hivi Hichilema siyo mpinzani tena, ni Rais wa Zambia kwahiyo usishangae marafiki ,ake watakuwa watawala kina Samia, Kagame, Uhuru na siyo kina Zitto tena.

Kwani yukoje sasa hivi Rais wa Malawi, mlokole na Rais kutoka Opposition ?

Alisemaje siku ya mazishi ya ?Magufuli pale Dodoma ?

In short wanasiasa wote wanafanana na mahitaji yao yanafanana. Wananchi ni Mitaji tu.

Punguzeni kuendeshwa kwa mihemko na kuabudu watu ili muuone uhalisia.

Halafu msitdgemew sana jumyiya za kimataifa kwasababu hazijawahi kusaidia, ndioaana kina Museven na Kagame wanadunda kabisa.

Tena sasa hivi Tanzania tuna Rais mwanamke, mambo ya Beijing ambaye kwa kawaida wanawake huwa wana upendeleo fulani usitegemee pressure yoyote ya maana.
 
System yenyewe utopolo hakuna maendeleo hakuna ajira bado wanafunzi wanakaa chini bado Mambo vululu Kuna maana gani kua na system isio tenda haki hata kuwahurumia wakulima wanaotulisha?

Mimi naona bado tz tunacheza hatuko siriasi na mstakabali wa taifa hili...ni lini tutapata maendeleo? Hivi Hawaumii Hali ilivyo mbaya hawajui kweli katiba italeta haki na kuvifanya vyombo vyote vya usalama kutenda haki?
 
Team kuupiga mwingi mnamtetea sana huyu mama,Ajabu anayofanya KWA Sasa MNAAMINI kuna watu nyuma(system) ila KWA JPM hamkuamini/hamuamini kama kulikua na watu nyuma.

Niwakumbushe tu,mbowe aliwahi sema JPM anatekeleza Sera za uchaguzi wa Chadema mwanzo kabisaaa alivyoingia JPM.Je hao systems walikuwepo na kumuendesha jpm?

Binafsi naona mnatapatapa tu baada ya nyimbo zenu na mapambio ya mwanzo.

Cc TEAM MAMA ANAUPIGA MWINGI/MSOGA TROOPS/CHADEMA/ACT/WANAHARAKATI UCHWARA.


Sisi ndo wazalendo pekee tulobaki,no chama kutetea ovu lolote,NO TEAM CHAWA KUPATA TEUZI.
mnaweza tuita Sukuma gang mkipenda.

KAZI ISIYO NA MBELE WALA NYUMA IENDELEE!
 
Hata Lungu alikuwa Rais kutoka Opposition. Sasa hivi Hichilema siyo mpinzani tena, ni Rais wa Zambia kwahiyo usishangae marafiki ,ake watakuwa watawala kina Samia, Kagame, Uhuru na siyo kina Zitto tena...
Moja ya kosa kubwa kulifanya kwa hao jamaa ni kuwashauri jema kwao,au kuahimiza watumie akili,utaonekana msaliti tu.
 
Mbona unaandika kwa kulalama namna hii ? Ndio the so called SYSTEM wamekutuma ? One thing you should know for sure DICTATORSHIP have definitive end ! Angalia historia duniani ! Ujue CCM DICTORSHIP will finally crumble ! And sooner than later ! We are in the digitally connected world not giving a sh** to outdated so called systems.
Tatizo sio udikteta wa CCM bali ninyi mnaouwezesha, na mfano hai ni huu kwenye comment yako. Badala ya kutafakari analysis hii bora kabisa, unakurupuka kumtuhumu mtoa mada kuwa "katumwa na system." Same thing happening on social media, Prof Shivji, nguli wa sheria huyu, alipotoa maoni yake kuhusu katiba mpya, akadhihakiwa kuwa amezeeka vibaya, anataka u-DC.

The system doesn't give a sh*t about you not giving a sh*t. Because, again kama ilivyozoeleka mitandaoni, anonymous people can't do sh*t except kutukana wakiamini hakuna atakaewabaini. Real changes are brought about by real people, not clowns hiding behind fake IDs.
 
Tatizo sio udikteta wa CCM bali ninyi mnaouwezesha, na mfano hai ni huu kwenye comment yako. Badala ya kutafakari analysis hii bora kabisa, unakurupuka kumtuhumu mtoa mada kuwa "katumwa na system." Same thing happening on social media, Prof Shivji, nguli wa sheria huyu, alipotoa maoni yake kuhusu katiba mpya, akadhihakiwa kuwa amezeeka vibaya, anataka u-DC.

The system doesn't give a sh*t about you not giving a sh*t. Because, again kama ilivyozoeleka mitandaoni, anonymous people can't do sh*t except kutukana wakiamini hakuna atakaewabaini. Real changes are brought about by real people, not clowns hiding behind fake IDs.
Na wewe umefanya alichofanya kwahyo mko sawa!
 
Swali langu kwa Chadema ..the system mnawasikiliza?Mtaweza kwenda against them kama hata Rais hawezi?
Hakuna system hapa bongo kama JPM aliweza kumtimua Top wa usalama na kubadili vitengo kibao sidhani kama kuna mtu zaidi ya Rais. Hta samia akiamua anaunda mfumo wake tu ndani ya mfumo na hakuna kitu "the professionals" watamfanya.

Hivi kweli hiyo system imeona solution ni kumpa mtu ugaidi mbona kipindi cha Dr.Slaa maandamano yalianza siku ya kwanza tu toka JK anakuwa reelected na bado akawaita ikulu wayamalize?? Kwani hao SYSTEM hawakujua JK ni unpopular? Mbona bado waliruhusu ashambuliwe na upinzani na akubali demands zao??

Kama SYSTEM wameona suluhu ni jino kwa jino badala ya kuwaita mezani wapinzani "kuwatuliza"basi tina SYSTEM mbovu zaidi duniani.

Kenya pametulia baada ya RAO kuitwa mezani katulizwa na sahvi husikii choko choko au maandamano ya upinzani. Mbona simple tu waite Upinzani ikulu waeleze vision zako na wao wakupe expectation zao. Then utafakari uwaambie nipeni mwaka nifanye kazi na upinzani uwe passive. In turn kuonyesha solidarity hta kina Mbatia wangepewa post kubwa za kimaamuzi hku reforms za kisiasa zikifanyika taratibu.

Trust me kufikia 2025 angeshinda kwa kishindo hta ingekuwepo tume huru na siasa zingekuwa safi sio za kuwindana. Ila mnapotumia nguvu watu wana sympathise na upinzani mind you bado team JPM inalialia hadi leo so kufikia 2025 huyo mama hama political base ya kushinda.

SYSTEM kama ndio imeshaurid direct approach basi imemuingiza chaka. Kufikia mwakani approval ratings zitashuka
 
Tatizo sio udikteta wa CCM bali ninyi mnaouwezesha, na mfano hai ni huu kwenye comment yako. Badala ya kutafakari analysis hii bora kabisa, unakurupuka kumtuhumu mtoa mada kuwa "katumwa na system." Same thing happening on social media, Prof Shivji, nguli wa sheria huyu, alipotoa maoni yake kuhusu katiba mpya, akadhihakiwa kuwa amezeeka vibaya, anataka u-DC.

The system doesn't give a sh*t about you not giving a sh*t. Because, again kama ilivyozoeleka mitandaoni, anonymous people can't do sh*t except kutukana wakiamini hakuna atakaewabaini. Real changes are brought about by real people, not clowns hiding behind fake IDs.
Funny enough unayetoa ushauri huu upo A million miles kutoka ground zero then unatukana waliopo nyuma ya fake ID?? kwani sisi sio real people au members wa JF ni BOTS?? Kampeni za upinzani nchi nzima zilikua adressed kwa fake IDs au watu??

Back to topic..... Najua mnataka upinzani uwe moderate lakini Mbatia na Maalim walifanya hivyo kwa JPM waliambulia nini?? Upinzani ulikua unamsifia sana Mama zile 100 days za kwanza na walifanya mikutano ya ndani pekee ssa ni kosa gani wamefanya mpka wapate retaliation?? Mbona Neutrals kma kina zitto na wenyewe wanalialia licha ya kujipendekeza zanzibar??

Hakunaga system hapa TZ Rais ndio sauti ya mwisho.... Otherwise JPM wangemcontain toka siku ya kwanza. Mtu kaharibu mifumo yote vile then unadai eti kuna SYSTEM!! haya mambo yako walau Rwanda hapo ila sio Tz hii ambayo Mwenyekiti ndio sauti ya mwisho. Ana uwezo wa kuunda jeshi ndani ya jeshi na hakuna kitu mnaweza mfanya!! Mkimzingua anaita mercenaries kumzunguka and no sh**t the so called SYSTEM can do!!
 
Back
Top Bottom