Chadema mmekuwa wakosoaji wazuri wa kero mbalimbali zinazoikabili jamii yetu. Mmekuwa msitari wa mbele katika kupambana na masuala ya ufisadi, hili ni jambo jema lakini msiishie hapo tunatarajia kuwasikia katika masuala mengine pengine muhimu zaidi kuliko hicho mnachokiita "ukombozi" ambayo ni dhana mfu kwani nchi hii ilishajikomboa tangu 1961 na haijatawaliwa tena, what is the essence of your liberation crusade?
1. Chadema hamsikiki mkihamasisha vijana kufanya kazi badala yake mnawapotezea muda mwingi kwa kuwashirikisha kwenye mikutano na maandamano yasiyo na tija. Hivyo mnachangia tatizo la ajira nchini(disguised unemployment)
2. Chadema hamjaishauri serikali ipasavyo namna ya kushughulikia kero za madaktari na walimu. Na hamjajitokeza hadharani kushawishi madaktari wasitishe mgomo wakati mazungumzo kati yao na serikali yakiendelea.
3. Mnachangishana kugharamia mikutano na maandamano kwanini hata maramoja hamjaelekeza hamasa ya michango
katika kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo kama ujenzi wa visima au majosho.
4. Nia yenu njema ya kumhudumia mtanzania iko wapi? ikiwa hamuonyeshi umakini katika mipango na mikakati yenu ya kumnasua mtanzania katika lindi la umasikini(rejea madudu kwenye bajeti ya upinzani).
5. Ni ipi ajenda yenu ya kiuchumi kwani mikutano na maandamano hayawezi kuwapatia watanzania huduma za afya na elimu, barabara na miundombinu mingine.
1. Chadema hamsikiki mkihamasisha vijana kufanya kazi badala yake mnawapotezea muda mwingi kwa kuwashirikisha kwenye mikutano na maandamano yasiyo na tija. Hivyo mnachangia tatizo la ajira nchini(disguised unemployment)
2. Chadema hamjaishauri serikali ipasavyo namna ya kushughulikia kero za madaktari na walimu. Na hamjajitokeza hadharani kushawishi madaktari wasitishe mgomo wakati mazungumzo kati yao na serikali yakiendelea.
3. Mnachangishana kugharamia mikutano na maandamano kwanini hata maramoja hamjaelekeza hamasa ya michango
katika kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo kama ujenzi wa visima au majosho.
4. Nia yenu njema ya kumhudumia mtanzania iko wapi? ikiwa hamuonyeshi umakini katika mipango na mikakati yenu ya kumnasua mtanzania katika lindi la umasikini(rejea madudu kwenye bajeti ya upinzani).
5. Ni ipi ajenda yenu ya kiuchumi kwani mikutano na maandamano hayawezi kuwapatia watanzania huduma za afya na elimu, barabara na miundombinu mingine.