Usiwe MTUMWA wa historiaZitto kama akikubali kufanya hivo nitamuona hamnazo kabisa. Kwa jinsi walivyomnanga kipindi kile afu Leo watake kuungana nae tena.?
Zitto usikubali kufanya huo ujinga hao wote walitaka upotee lakini ulipambana kiume sana hadi leo hii heshima imeanza kurudi.
Mh. Zitto jaribu ila muungano wetu uwe wa kuachiana majimbo na urais basi.Usiwe MTUMWA wa historia
huu ni ushauri mzuri na Viongozi tunatafakari
Shikamoo Muheshimiwa.Usiwe MTUMWA wa historia
huu ni ushauri mzuri na Viongozi tunatafakari
Vyama vya upinzani hata wakijngana au ikawekwa Tume ya Uchaguzi kutoka Mbinguni, kamwe hawatashinda Uchaguzi Mkuu mwaka huu, labda 2025. Sababu ziko wazi kwani mwenye macho anaona na mwenye masikio anasikia.ACT ina nguvu mkuu. Kilichopunguza spidi ya ACT ni hili janga la corona ila ni chama ambacho kinakuja juu sana
Na ni chama ambacho kitakuja kuwa tishio sana kwa CCM endapo strategies fulani fulani wakizitumia..
Waungane na NCCR mageuziMpaka sasa kuna idadi kubwa ya Wabunge walioondoka CHADEMA kwa sababu mbalimbali. Lakini ni ukweli ulio wazi kabisa mpaka sasa chama kinadhoofu (Ikumbukwe kuondoka kwa hao wabunge haimaanishi kuwa wanaondoka na wanachama ila inasababisha sintofahamu kwa wanachama).
Unganiko lenu na ACT WAZALENDO ndio suluhu ya kukiokoa chama kisizame. Nina uhakika awamu ya 2020-2025 ndio itakuwa kuchakaa rasmi kwa CHADEMA na kuundwa chama kingine kikuu cha upinzani.
NCCR Mageuzi haiwezi kuwa tishio kwa CHADEMA. Mbatia hana ushawishi katika siasa za Tanzania ukilinganisha na Zitto Kabwe.
Siasa za upinzani zinahitaji muunganiko wa Lissu, Zitto na Maalim Seif. Hawa naweza kusema ndio wanaobeba upinzani kwa sasa. Mbowe ana siasa za matukio (kwenye ukweli tuseme).
Hii "combination" ya ZItto na Lissu ni hatari maana ni watu ambao wanajua kuanzisha hoja na kuisimamia na wana ushawishi mkubwa sana.
Mpaka sasa CHADEMA ishajua wasaliti wao ni akina nani. Zitto hakuwa msaliti na ndio maana hata alipofukuzwa CHADEMA alipoteza ubunge na hakuhamia CCM akaenda kuanzisha chama na huko akapita ubunge tena kwa kuhama jimbo (kitu ambacho Mbatia hawezi; alipigwa mtama na Mdee Kawe akaenda kwa Lyatonga Vunjo-Nguvu ya UKAWA ndio ikamuweka pale alipo). Hawa wengine mliowafukuza uanachama wamerudi CCM moja kwa moja.
Ushauri wangu achaneni na kujiona ndio mnaimarika bali fahamuni ya kuwa chama kinakufa na suluhu ni kuungana na ACT-Wazalendo hata kama hamtachukua dola lakini mtajiongezea idadi ya viti bungeni na hivyo kuipunguza monopoly ya CCM bungeni.
Achaneni na propaganda za kina Yericko wao siku zote wanamuona ZItto ndio adui namba moja wa CHADEMA. Unganeni na ACT mlete upinzani kwa CCM tofauti na hapo hiyo October mtapata wakati mgumu na mnaweza hata msipate wabunge (Sio kwa sababu watapigia kura CCM bali morale ya wanachama wenu itapungua sana na uwezekano wa wanachama wenu kutopiga kura ukawa mkubwa kutokana na kile kinachoendelea sasa).
Nawasilisha!
Upo sahihi mkuu.tume huru kwa ccm hawawezi kuruhusu wapo tayari kwenda motoni kuliko kukubali tume huruAcha kushawishi watu wasipige kura mkuu, Kupambana ni muhimu kivyovyote vile.
Fahamu hili kuwa haitatokea kamwe CCM kuweka tume huru. Ni kupambana nao tu mpaka kieleweke
Unafikiria hizo nyengine ni nyepesi mkuu?
Endeleeni kujidanganyaAkiondoka Mbowe, kama bado yupo chama kipo imara
Cdm itabakia cdm tu hizo taarabu zenu kaimbie lumumba kwenu kwenye mkesha wa kuiaga coronaAkiondoka Mbowe, kama bado yupo chama kipo imara
Mbowe hana impact yoyote kwa CHADEMA awepo au asiwepo hana madhara.
Ukweli ni kwamba kwa sasa CHADEMA akiondoka Lissu basi chama kimekwisha.
Wanaweza kukubaliana kila kitu lkn lazima washindane linapokuja suala la uenyekiti
Chombo cha kuzama siku zote huwa hakina usukani!
Watatapatapa mwishowe wataungana hadi na CCM,ACT yenyewe ni Zanzibar tu bara imesimamia mguu mmoja kama jini.
Naunga Mkono Hoja