Ukwelimtupu
Member
- Nov 21, 2011
- 36
- 13
CHADEMA na vyama washirika wanaounda UKAWA wamejikuta kwenye wakati mgumu wa kukosa ajenda baada ya Rais John Pombe Magufuli kuanza kutekeleza ahadi ambazo alizitoa kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA na vyama washirika wamekuwa wakipeta sana kwa kuibua madudu ya CCM kama rushwa na ufisadi, uzembe serikalini, uongozi mbovu, ahadi zisizotekelezeka na mambo mengi ya ovyo yalikuwa yakitendeka serikalini. Rais Magufuli kwa kiasi flani ameweza kuwashughulikia baadhi ya wala rushwa na mafisadi na kuwatumbua watumishi hewa na kusimamia serikali yake namna ambayo Watanzania hatujawahi kushuhudia kwenye awamu ya 2,3 na 4.
Ni kweli kwamba mambo ambayo yalikipa CHADEMA sifa ni kukemea rushwa na ufisadi serikalini, uongozi mbovu, ahadi hewa za CCM na kushindwa kwa serikali ya CCM kuzitumia vyema rasmali za nchi kwa manufaa ya Watanzania. Mambo haya kwa sasa ndiyo anayoyashughulikia rais Magufuli. Usugu wa matatizo haya umepungua na kuyafanya yasiwe "hot news" kisiasa na CHADEMA kushindwa kuyatumia matatizo haya kama ajenda kwenye mijadala yao. Hivyo CHADEMA/UKAWA wamejikuta hawana ajenda ya kuwafanya wasikike magazetini, redioni, TV na vijiweni.
Vipi kuhusu udikteta? CHADEMA/UKAWA walikuwa wakimnadi Mhe Lowassa kama kiongozi ambaye ataipeleka Tanzania mchakamchaka na kuondoa uzembe serikalini na kuwatumikia watanzania, kukuza uchumi na kuondoa umaskini Tanzania. Kwa tafsiri yangu mchakamchaka ni kutovumilia mambo ya ovyo kama uzembe, wafanyakazi hewa, shule bila madawati, kipindupindu, maandamano yasiyokuwa na tija, rushwa na ufisadi, kutotekeleza ahadi za serikali, ukwepaji kodi, uporaji ardhi, serikali kubaki Dar japo makao makuu yake ni Dodoma na mambo mengine mengi. Sasa inakuwaje CHADEMA wanalalamika pale ambapo Rais Magufuli anaipeleka Tanzania mchakamchaka?
RAI YANGU KWA CHADEMA: Inapaswa CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA wajitathmini na kujipanga upya. Kama chama cha upinzani misingi yake ni ipi? Ni matatizo yapi yanaikabili Tanzania na wana njia zipi mbadala za kuyatatua matatizo haya? Ili chama kiendelee kubaki hai na kisikike (kisiwe 'dormant') je ni hoja zipi zenye mashiko zitumiwe kuikosoa serikali?
Ni kweli kwamba mambo ambayo yalikipa CHADEMA sifa ni kukemea rushwa na ufisadi serikalini, uongozi mbovu, ahadi hewa za CCM na kushindwa kwa serikali ya CCM kuzitumia vyema rasmali za nchi kwa manufaa ya Watanzania. Mambo haya kwa sasa ndiyo anayoyashughulikia rais Magufuli. Usugu wa matatizo haya umepungua na kuyafanya yasiwe "hot news" kisiasa na CHADEMA kushindwa kuyatumia matatizo haya kama ajenda kwenye mijadala yao. Hivyo CHADEMA/UKAWA wamejikuta hawana ajenda ya kuwafanya wasikike magazetini, redioni, TV na vijiweni.
Vipi kuhusu udikteta? CHADEMA/UKAWA walikuwa wakimnadi Mhe Lowassa kama kiongozi ambaye ataipeleka Tanzania mchakamchaka na kuondoa uzembe serikalini na kuwatumikia watanzania, kukuza uchumi na kuondoa umaskini Tanzania. Kwa tafsiri yangu mchakamchaka ni kutovumilia mambo ya ovyo kama uzembe, wafanyakazi hewa, shule bila madawati, kipindupindu, maandamano yasiyokuwa na tija, rushwa na ufisadi, kutotekeleza ahadi za serikali, ukwepaji kodi, uporaji ardhi, serikali kubaki Dar japo makao makuu yake ni Dodoma na mambo mengine mengi. Sasa inakuwaje CHADEMA wanalalamika pale ambapo Rais Magufuli anaipeleka Tanzania mchakamchaka?
RAI YANGU KWA CHADEMA: Inapaswa CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA wajitathmini na kujipanga upya. Kama chama cha upinzani misingi yake ni ipi? Ni matatizo yapi yanaikabili Tanzania na wana njia zipi mbadala za kuyatatua matatizo haya? Ili chama kiendelee kubaki hai na kisikike (kisiwe 'dormant') je ni hoja zipi zenye mashiko zitumiwe kuikosoa serikali?