CHADEMA/UKAWA wamehaha

Ukwelimtupu

Member
Nov 21, 2011
36
13
CHADEMA na vyama washirika wanaounda UKAWA wamejikuta kwenye wakati mgumu wa kukosa ajenda baada ya Rais John Pombe Magufuli kuanza kutekeleza ahadi ambazo alizitoa kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA na vyama washirika wamekuwa wakipeta sana kwa kuibua madudu ya CCM kama rushwa na ufisadi, uzembe serikalini, uongozi mbovu, ahadi zisizotekelezeka na mambo mengi ya ovyo yalikuwa yakitendeka serikalini. Rais Magufuli kwa kiasi flani ameweza kuwashughulikia baadhi ya wala rushwa na mafisadi na kuwatumbua watumishi hewa na kusimamia serikali yake namna ambayo Watanzania hatujawahi kushuhudia kwenye awamu ya 2,3 na 4.

Ni kweli kwamba mambo ambayo yalikipa CHADEMA sifa ni kukemea rushwa na ufisadi serikalini, uongozi mbovu, ahadi hewa za CCM na kushindwa kwa serikali ya CCM kuzitumia vyema rasmali za nchi kwa manufaa ya Watanzania. Mambo haya kwa sasa ndiyo anayoyashughulikia rais Magufuli. Usugu wa matatizo haya umepungua na kuyafanya yasiwe "hot news" kisiasa na CHADEMA kushindwa kuyatumia matatizo haya kama ajenda kwenye mijadala yao. Hivyo CHADEMA/UKAWA wamejikuta hawana ajenda ya kuwafanya wasikike magazetini, redioni, TV na vijiweni.

Vipi kuhusu udikteta? CHADEMA/UKAWA walikuwa wakimnadi Mhe Lowassa kama kiongozi ambaye ataipeleka Tanzania mchakamchaka na kuondoa uzembe serikalini na kuwatumikia watanzania, kukuza uchumi na kuondoa umaskini Tanzania. Kwa tafsiri yangu mchakamchaka ni kutovumilia mambo ya ovyo kama uzembe, wafanyakazi hewa, shule bila madawati, kipindupindu, maandamano yasiyokuwa na tija, rushwa na ufisadi, kutotekeleza ahadi za serikali, ukwepaji kodi, uporaji ardhi, serikali kubaki Dar japo makao makuu yake ni Dodoma na mambo mengine mengi. Sasa inakuwaje CHADEMA wanalalamika pale ambapo Rais Magufuli anaipeleka Tanzania mchakamchaka?

RAI YANGU KWA CHADEMA: Inapaswa CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA wajitathmini na kujipanga upya. Kama chama cha upinzani misingi yake ni ipi? Ni matatizo yapi yanaikabili Tanzania na wana njia zipi mbadala za kuyatatua matatizo haya? Ili chama kiendelee kubaki hai na kisikike (kisiwe 'dormant') je ni hoja zipi zenye mashiko zitumiwe kuikosoa serikali?
 
Wajitathmini how wakati hata hamtaki wasikike popote bungeni, mikutatano mnaifanyia mizengwe, hata vyombo vya habari haziruhusiwi kutoa hoja zao labda kidogo magazeti.
Sasa hapo ulitaka wafanyeje ?! Wafanye fujo ndio ujue wana hoja ?!

Tumia hekima kabla ya kutoa hoja
 
Unapoiacha Akili yako iendeshwe na wenye kuharibu taswira ya family yako, Basi hupaswi kulaumu Wale wanaokucheka na kukukosoa
 
Huyu jamaa amegundua kuwa ili apate riziki yake ni kumsifia tu asiyejaribiwa na asiyekosolewa, hata mimi nitakuwa namsifia tu huyu malaika wetu maana amemzidi hata yesu aliyejaribiwa ili nisione cha mtemakuni
 
Huyu jamaa amegundua kuwa ili apate riziki yake ni kumsifia tu malaika asiyejaribiwa na asiyekosolewa, hata mimi nitakuwa namsifia tu huyu malaika wetu maana amemzidi hata yesu aliyejaribiwa ili nisione cha mtemakuni

Kwa hiyo kwa uelewa wako unaona natetea riziki yangu? Tatizo kubwa la baadhi ya wanachama wa CHADEMA ni kupinga hata kile kisichopingika. Hivi inakuingia akilini pale ambapo mtu anakerwa na hatua anazozichukua JPM kuhakikisha kwamba kodi stahiki inalipwa serikalini? Wewe binafsi unauonaje utendaji wa JPM?
 
CHADEMA na vyama washirika wanaounda UKAWA wamejikuta kwenye wakati mgumu wa kukosa ajenda baada ya Rais John Pombe Magufuli kuanza kutekeleza ahadi ambazo alizitoa kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA na vyama washirika wamekuwa wakipeta sana kwa kuibua madudu ya CCM kama rushwa na ufisadi, uzembe serikalini, uongozi mbovu, ahadi zisizotekelezeka na mambo mengi ya ovyo yalikuwa yakitendeka serikalini. Rais Magufuli kwa kiasi flani ameweza kuwashughulikia baadhi ya wala rushwa na mafisadi na kuwatumbua watumishi hewa na kusimamia serikali yake namna ambayo Watanzania hatujawahi kushuhudia kwenye awamu ya 2,3 na 4.

Ni kweli kwamba mambo ambayo yalikipa CHADEMA sifa ni kukemea rushwa na ufisadi serikalini, uongozi mbovu, ahadi hewa za CCM na kushindwa kwa serikali ya CCM kuzitumia vyema rasmali za nchi kwa manufaa ya Watanzania. Mambo haya kwa sasa ndiyo anayoyashughulikia rais Magufuli. Usugu wa matatizo haya umepungua na kuyafanya yasiwe "hot news" kisiasa na CHADEMA kushindwa kuyatumia matatizo haya kama ajenda kwenye mijadala yao. Hivyo CHADEMA/UKAWA wamejikuta hawana ajenda ya kuwafanya wasikike magazetini, redioni, TV na vijiweni.

Vipi kuhusu udikteta? CHADEMA/UKAWA walikuwa wakimnadi Mhe Lowassa kama kiongozi ambaye ataipeleka Tanzania mchakamchaka na kuondoa uzembe serikalini na kuwatumikia watanzania, kukuza uchumi na kuondoa umaskini Tanzania. Kwa tafsiri yangu mchakamchaka ni kutovumilia mambo ya ovyo kama uzembe, wafanyakazi hewa, shule bila madawati, kipindupindu, maandamano yasiyokuwa na tija, rushwa na ufisadi, kutotekeleza ahadi za serikali, ukwepaji kodi, uporaji ardhi, serikali kubaki Dar japo makao makuu yake ni Dodoma na mambo mengine mengi. Sasa inakuwaje CHADEMA wanalalamika pale ambapo Rais Magufuli anaipeleka Tanzania mchakamchaka?

RAI YANGU KWA CHADEMA: Inapaswa CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA wajitathmini na kujipanga upya. Kama chama cha upinzani misingi yake ni ipi? Ni matatizo yapi yanaikabili Tanzania na wana njia zipi mbadala za kuyatatua matatizo haya? Ili chama kiendelee kubaki hai na kisikike (kisiwe 'dormant') je ni hoja zipi zenye mashiko zitumiwe kuikosoa serikali?

Unahitaji maombi mkuuu amini nakwambia hama matambiko
 
Chadema bila Lowassa ndiyo ilikuwa CHADEMA, hii ya sasa wanajaribu kutusahailisha kuwa hawana FISADI ndani kwao. Ni upuuzi tu wanaoalalamikia.
 
Kwa hiyo kwa uelewa wako unaona natetea riziki yangu? Tatizo kubwa la baadhi ya wanachama wa CHADEMA ni kupinga hata kile kisichopingika. Hivi inakuingia akilini pale ambapo mtu anakerwa na hatua anazozichukua JPM kuhakikisha kwamba kodi stahiki inalipwa serikalini? Wewe binafsi unauonaje utendaji wa JPM?
Mwacha huu hakuna watakalaosema CHADEMA la kuwaumiza wana CCM na wanaomuunga mkono Magufuli zaidi ya MATUSI. Magufuli kawamaliza.
 
Huyu jamaa amegundua kuwa ili apate riziki yake ni kumsifia tu malaika asiyejaribiwa na asiyekosolewa, hata mimi nitakuwa namsifia tu huyu malaika wetu maana amemzidi hata yesu aliyejaribiwa ili nisione cha mtemakuni
Chadema hoja hamna tena, ndiyo umeandika nini sasa?
 
Mtoa mada nimeona nisikuache hivihivi coz naona una uhelewa hafifu sana ni hivi hayo yote anayofanya JPM ni matunda ya kuwepo upinzani kwahivo basi ili nchi iendelee tunahitaji wapinzani wenye nguvu pengine kuliko CHADEMA
 
CHADEMA na vyama washirika wanaounda UKAWA wamejikuta kwenye wakati mgumu wa kukosa ajenda baada ya Rais John Pombe Magufuli kuanza kutekeleza ahadi ambazo alizitoa kwenye kampeni za uchaguzi wa mwaka 2015. CHADEMA na vyama washirika wamekuwa wakipeta sana kwa kuibua madudu ya CCM kama rushwa na ufisadi, uzembe serikalini, uongozi mbovu, ahadi zisizotekelezeka na mambo mengi ya ovyo yalikuwa yakitendeka serikalini. Rais Magufuli kwa kiasi flani ameweza kuwashughulikia baadhi ya wala rushwa na mafisadi na kuwatumbua watumishi hewa na kusimamia serikali yake namna ambayo Watanzania hatujawahi kushuhudia kwenye awamu ya 2,3 na 4.

Ni kweli kwamba mambo ambayo yalikipa CHADEMA sifa ni kukemea rushwa na ufisadi serikalini, uongozi mbovu, ahadi hewa za CCM na kushindwa kwa serikali ya CCM kuzitumia vyema rasmali za nchi kwa manufaa ya Watanzania. Mambo haya kwa sasa ndiyo anayoyashughulikia rais Magufuli. Usugu wa matatizo haya umepungua na kuyafanya yasiwe "hot news" kisiasa na CHADEMA kushindwa kuyatumia matatizo haya kama ajenda kwenye mijadala yao. Hivyo CHADEMA/UKAWA wamejikuta hawana ajenda ya kuwafanya wasikike magazetini, redioni, TV na vijiweni.

Vipi kuhusu udikteta? CHADEMA/UKAWA walikuwa wakimnadi Mhe Lowassa kama kiongozi ambaye ataipeleka Tanzania mchakamchaka na kuondoa uzembe serikalini na kuwatumikia watanzania, kukuza uchumi na kuondoa umaskini Tanzania. Kwa tafsiri yangu mchakamchaka ni kutovumilia mambo ya ovyo kama uzembe, wafanyakazi hewa, shule bila madawati, kipindupindu, maandamano yasiyokuwa na tija, rushwa na ufisadi, kutotekeleza ahadi za serikali, ukwepaji kodi, uporaji ardhi, serikali kubaki Dar japo makao makuu yake ni Dodoma na mambo mengine mengi. Sasa inakuwaje CHADEMA wanalalamika pale ambapo Rais Magufuli anaipeleka Tanzania mchakamchaka?

RAI YANGU KWA CHADEMA: Inapaswa CHADEMA na vyama washirika wa UKAWA wajitathmini na kujipanga upya. Kama chama cha upinzani misingi yake ni ipi? Ni matatizo yapi yanaikabili Tanzania na wana njia zipi mbadala za kuyatatua matatizo haya? Ili chama kiendelee kubaki hai na kisikike (kisiwe 'dormant') je ni hoja zipi zenye mashiko zitumiwe kuikosoa serikali?
Umefika mwisho wa kufikiri auu?
 
Back
Top Bottom