CHADEMA, UKAWA, muacheni Lowassa aongoze kampeni yake

CHADEMA, UKAWA, muacheni Lowassa aongoze kampeni yake

Anheuser

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2011
Posts
1,944
Reaction score
665
Uongozi CHADEMA, UKAWA, na wadau wa upinzani. Kama mmemualika Lowassa kusaidia kuiangusha C.C.M. basi ni kwa sababu ameonyesha dalili za mafanikio, na hiyo yote inatokana na mikakati yake ya siku nyingi pamoja na timu yake, ujumbe wake kwa umma, historia na mvuto wake kwa jamii.

Kama ndie yeye mnaetegemea kumpa abebe bendera basi muacheni Lowassa awe Lowassa, ikiwa ni pamoja na kumuacha ku control his message. Huu mpango wa Mwenyekiti na wasemaji wa chama kila asubuhi wanatoka na matamko kuhusu Dr. Slaa sijui Mnyika tuwaombee kwa Mungu sijui wamefanya lile na hili, wamesusa, hawajala, hawarudi nyumbani, that is extremely crippling to the Lowassa campaign. Mnamwondoa mgombea wenu kwenye national conversation badala ya kumuachia ukumbi.Mmeshampokea, mmeshampokea, hayo ni maji chini ya daraja.

Wengine wame focus kwenye "kwa nini havai gwanda," well, labda timu yake imeamua strategically kum project kama national leader, huwezi kwenda kwenye national election na magwanda ya chama kimoja. Kushinda uchaguzi Lowassa atahitaji kura za wapenda C.C.M. pia. Hii si kampeni ya CHADEMA, ni kampeni ya Lowassa, image ya CHADEMA is badly tainted right now, mwacheni mgombea ajinasibu kwa utashi wake mwenyewe. Kina Mbowe sogeeni pembeni kwa sasa tafadhalini, waacheni wakina Apson Mwang'onda wa run the campaign. Rai yangu kwa Lowassa, kwa sasa anzisha ofisi ya makao makuu ya kampeni mbali na Mtaa wa Ufipa.
 
Nafikiri baada ya kupitishwa leo EL atambulishwe mikoani na huko azungumze yeye mwenyewe na hotuba zake zisiguse swala la Slaa.
 
Anheuser

Hadi october mtaishiwa cha kusema
 
Last edited by a moderator:
Anheuser

Mnadhani mtatutoa kwenye reli, thubuuutu!
 
Last edited by a moderator:
Nimegundua sio wote wanaotoa ushaur kwa Ukawa ni wana ukawa wengine ni magamba dam dam.

Huo ndio mpango mkakati wa ccm kutaka kuivuruga ukawa,ila wamechemka kwani ukawa kuna watu vile vile.
 
Duuu..............Huu mwaka wa tabu. SITAPIGA KURA YA URAIS!!!!!
 
Wewe utakuwa mgonjwa, ni sawa na mgeni aje kwako umuachie majukumu yote
 
Japo sina uhakika kàma mtoa mada yupo Team Lowassa ila aliyoyaongea yana ukweli kiasi flani,hata mimi nililiona hili,na ninaamini hatà wana mikakati wa kampeni wa Dr Magufuli wameuona huu upenyo na wanautumia sasa.Habari za kila siku zinazomhusu Dr Slaa zinamwondoa Lowassa ambaye ndiye mgombea mtarajiwa wa UKAWA katika front pages na headlines za media kila siku,this was supposed to be UKAWA moment and they have failed to take advantage of it, Ila kuhusu ujumbe hilo linahitaji collaborative efforts.
Lastly Dr Slaa bado ni muhimu sana katika kampeni,kuna wale ambao wanaitwa sceptical voters ambao bado wana mashaka na uadilifu wa Lowassa,Dr Slaa ndio sauti pekee ya kuaminika ndani ya CHADEMA itakayoweza kuwalainisha hawa wapiga kura,mwingine simwoni.
 
Japo sina uhakika kàma mtoa mada yupo Team Lowassa ila aliyoyaongea yana ukweli kiasi flani,hata mimi nililiona hili,na ninaamini hatà wana mikakati wa kampeni wa Dr Magufuli wameuona huu upenyo na wanautumia sasa.Habari za kila siku zinazomhusu Dr Slaa zinamwondoa Lowassa ambaye ndiye mgombea mtarajiwa wa UKAWA katika front pages na headlines za media kila siku,this was supposed to be UKAWA moment and they have failed to take advantage of it, Ila kuhusu ujumbe hilo linahitaji collaborative efforts.
Lastly Dr Slaa bado ni muhimu sana katika kampeni,kuna wale ambao wanaitwa sceptical voters ambao bado wana mashaka na uadilifu wa Lowassa,Dr Slaa ndio sauti pekee ya kuaminika ndani ya CHADEMA itakayoweza kuwalainisha hawa wapiga kura,mwingine simwoni.

Enedeleeni kujidanganya maana ukawa ina silaa ,za kutisha kila kiongozi ndani ya ukawa ni tishio kwa ccm
 
Nimegundua sio wote wanaotoa ushaur kwa Ukawa ni wana ukawa wengine ni magamba dam dam.

Hapana mmefanya upuuzi huwezi kumkaribisha fisadi ukabaki salama hiyo , mmeua chama na matumaini ya wengi
 
Lowassa kainunua CHADEMA kwa billion kadhaa. Halafu kapewa chama na nyongeza ya discount ya vyama vya cuf, nccr
 
Ata mi naunga mkono huyu slaa kuntajataja kila saa sio issue apotezewe anaturudisha nyuma
 
Back
Top Bottom