Heshima yenu wanaJf! Chama cha Demokrasia na Maendeleo Sumbwanga mjini kimekanusha upotoshaji uliofanywa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Rukwa bw Matete kuwa bw Godfrey Shayo iliyekihama Chama hicho na kujiunga na CCM alikuwa mwenyekiti wa CHADEMA wilaya. Taarifa za uhakika toka ofisi ya CHADEMA Sumbawanga mjini ni kuwa bw Shayo alishawahi kushika wadhifa wa mwenyekiti wa baraza la Vijana BAVICHA Sumbawanga mjini tena siyo wilaya nzima ya Sumbawanga kwani wilaya ya Sumbawanga ina wenyeviti wawili wa BAVICHA akiwepo wa Sumbawanga mjini na Sumbawanga vijijini. Kumbukumbu zinaonesha kuwa katika kipindi cha uongozi wa bw Shayo kama mwenyekiti wa BAVICHA Sumbawanga mjini alibainika kuwa mdanganyifu kwa kutumia mamlaka yake kuchangisha pesa toka kwa wafadhiri na kuzichakachua. Kwa mjibu wa Katibu wa CHADEMA wilaya bw Kasikila upo ushahidi uliyomtia bw Shayo hatiani wa kuchangisha kiasi cha Tsh 48,000/ na kuzitafuna, ni kwa ubadhirifu huo ndo kikao rasmi cha BAVICHA Sumbawanga mjini cha tarehe 16/07/2011 kiliamua kwa manufaa ya chama na kwa kauli moja kumvua uongozi bw Shayo baada ya kupoteza sifa za kuwa kiongozi. Mhutasari wa kikao cha kutokuwa na Imani na Bw Shayo. Tazama kiambatanisho nimeambatanisha na makala hii.
Katika hafla kubwa yenye sura ya kimkoa iliyoandaliwa na CCM Mkoa wa Rukwa kwa ajili ya kumkaribisha bw Shayo CCM na kurushwa na Sumbwanga Tv, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Rukwa bw Matete alikaririwa akitamka kwa ujasiri mkubwa kuwa bw Shayo ametokea CHADEMA kama mwenyekiti wa wilaya na kuongezea kuwa zaidi ya kuwa mwenyekiti wa wilaya Sumbawanga pia alikuwa akiongoza wilaya ya Nkasi kwa wadhifa huo huo, Taarifa sahihi ni kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Sumbwanga ni bw Godfrey Katata, na mwenyekiti wa sasa wa BAVICHA tangu tar 18/07/2011 ni bw Conwell Kakwaya, kwa mjibu wa mjumbe wa Baraza la vijana CHADEMA taifa mkoa wa Rukwa bw Frank Joseph Fumpa huu ni upotoshaji wa hali ya juu kwani bw Shayo baada ya kuvuliwa uongozi alibaki akitapatapa mara baada ya kukosa platform CHADEMA na kwa maana hiyo ndiyo maana akaona ni bora ahamie CCM, rekodi sahihi ni kuwa bw Shayo amehamia CCM kama mwanachama wa kawaida wa CHADEMA tena mwanachama mwenye doa au kovu la utaperi. CCM wanapongezwa kwa kuandaa hafla kubwa iliyohudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyaya, wakuu wa wilaya, wabunge, watendaji wakuu wa mkoa, na halmashauri zote za mkoa, (Mpanda, Nkasi, Sumbawanga vijiji na Manispaa) kwa ajili ya kumkaribisha bw Shayo, lakini wajue si sahihi sana kufanya hivyo kwa sasa kwani kutokana na hali mbaya ya maisha wanayokabiliwa wanarukwa ni fedheha kwa CCM na Serikali kwa ujumla. Ikumbukwe kuwa mkoa wa Rukwa una wenyeji wanaotegemea kilimo lakini kwa sasa pamoja na kuwepo na sera ya kilimo kwanza wakulima wanashindwa kununua pembejeo, kwa sasa mfuko wa mbolea Sumbwanga ni 50 elfu @ kilo 50 (mbolea ya Ruzuku) na mbolea y a kuuzwa tu kwa kawada ni shilingi 82 elfu hadi 90 elfu, barabara ni mbovu hazitumiki kwasasa, mafuta ni shida siku ya x mas lita moja ya mafuta ya petroli ilifikia shilingi elfu 7. Namuomba Stella Manyanya ayafanyie kazi haya na si propaganda za kisiasa, ni vema kama ana nia ya kuendeleza mkoa hizo awaachie wakina Tambwe Hiza
CHADEMA Sumbawanga mjini imekanusha pia upotoshaji mwingine kuwa bw Shayo ameihama CHADEMA eti kwa sababu ya ukabila na udini, upotoshaji huo unajibainisha kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, viongozi wa madhehebu ya kikristo walijiingiza katika kampeni makanisani kwa kumpinga mgombea wa CCM bw AESHI kwa kuwa ni muumini wa kiislam, hoja hii inahitimishwa kwa kusema kuwa CHADEMA Sumbwanga ni chama cha wakristo, Hoja hii si sahihi na kwamba udini Sumbwanga mjini haupo kwa vyama vyote viwili yaani CCM na CHADEMA. Chachu ya udini Sumbawanga iliingizwa kwa wapiga kura katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka jana na viongozi wa kampeni wa CCM bw Matete( mwenyekiti CCM mkoa),bw Tungombe (katibu mwenezi wilaya), bw Aeshi (mgombea wa ubunge), na wengineo. Hali ilikuwa mbaya sana pale bw Aeshi mgombea wa ubunge CCM alipoishiwa sera kwa wapiga kura na kujinadi katika mikutano kadhaa ya hadhara yeye kama YESU, na kumwita Kikwete MUNGU na Madiwani ROHO MTAKATIFU, jambo hili lilionekana kama fedheha na dharau kubwa kwa wakristo, kanisa katoriki lilitoa onyo kali kwa bw Aeshi na kutoa ujumbe wa kuombwa msamaha kwa dharau hiyo, jambo ambalo halikuwezekana, hali iliendelea kuharibiwa zaidi pale bw Matete kutumia advantage ya yeye kusoma seminari na mapadre wa kikatoriki na kuwa karibu nao kwa muda na kutumia mikutano ya kampeni kuwaita mapadre wahuni na wazinzi na kuwa yeye anawafahamu vizuri. Kauli hizi alizipata mh Pinda na kuwaamuru wahusika waombe msamaha kwa makanisa, kwa bahati mbaya hawa kufanya hivyo. Mh Pinda aliamua mwenyewe kuja Sumbawanga kuongea na viongozi wa dini wa kikristo kadhaa na kuamua mwenyewe kuapanda jukwaani katika uwanja wa Rukwa high school na kueleza yote kwa kujaribu kumtetea bw Aeshi kwa kusema alikuwa alijaribu kuomba kura kwa kutumia mafiga matatu akajisahau akatamka YESU,MUNGU na ROHO MTAKATIFU, lakini Pinda alikiri kuwa ni kosa kubwa na hasa kwa Aeshi ambaye si dhehebu hilo, mwishowe mh Pinda aliomba msamaha kwa niaba ya CCM na wote waliohusika.Mh Pinda aliondoka, lakini bado wahusika hawakukoma na hadi sasa kama ilivyoelezwa na bw Shayo bado hoja hii iko katika kauli za viongozi wa CCM mkoa. CHADEMA Sumbawanga mjini inatamka kuwa haihusiki kwa hili la udini, CHADEMA iko imara na itaendelea kuwa imara zaidi Sumbawanga mjini. Naomba kuwasilisha wakuu.
Katika hafla kubwa yenye sura ya kimkoa iliyoandaliwa na CCM Mkoa wa Rukwa kwa ajili ya kumkaribisha bw Shayo CCM na kurushwa na Sumbwanga Tv, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Rukwa bw Matete alikaririwa akitamka kwa ujasiri mkubwa kuwa bw Shayo ametokea CHADEMA kama mwenyekiti wa wilaya na kuongezea kuwa zaidi ya kuwa mwenyekiti wa wilaya Sumbawanga pia alikuwa akiongoza wilaya ya Nkasi kwa wadhifa huo huo, Taarifa sahihi ni kuwa mwenyekiti wa CHADEMA Sumbwanga ni bw Godfrey Katata, na mwenyekiti wa sasa wa BAVICHA tangu tar 18/07/2011 ni bw Conwell Kakwaya, kwa mjibu wa mjumbe wa Baraza la vijana CHADEMA taifa mkoa wa Rukwa bw Frank Joseph Fumpa huu ni upotoshaji wa hali ya juu kwani bw Shayo baada ya kuvuliwa uongozi alibaki akitapatapa mara baada ya kukosa platform CHADEMA na kwa maana hiyo ndiyo maana akaona ni bora ahamie CCM, rekodi sahihi ni kuwa bw Shayo amehamia CCM kama mwanachama wa kawaida wa CHADEMA tena mwanachama mwenye doa au kovu la utaperi. CCM wanapongezwa kwa kuandaa hafla kubwa iliyohudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Stella Manyaya, wakuu wa wilaya, wabunge, watendaji wakuu wa mkoa, na halmashauri zote za mkoa, (Mpanda, Nkasi, Sumbawanga vijiji na Manispaa) kwa ajili ya kumkaribisha bw Shayo, lakini wajue si sahihi sana kufanya hivyo kwa sasa kwani kutokana na hali mbaya ya maisha wanayokabiliwa wanarukwa ni fedheha kwa CCM na Serikali kwa ujumla. Ikumbukwe kuwa mkoa wa Rukwa una wenyeji wanaotegemea kilimo lakini kwa sasa pamoja na kuwepo na sera ya kilimo kwanza wakulima wanashindwa kununua pembejeo, kwa sasa mfuko wa mbolea Sumbwanga ni 50 elfu @ kilo 50 (mbolea ya Ruzuku) na mbolea y a kuuzwa tu kwa kawada ni shilingi 82 elfu hadi 90 elfu, barabara ni mbovu hazitumiki kwasasa, mafuta ni shida siku ya x mas lita moja ya mafuta ya petroli ilifikia shilingi elfu 7. Namuomba Stella Manyanya ayafanyie kazi haya na si propaganda za kisiasa, ni vema kama ana nia ya kuendeleza mkoa hizo awaachie wakina Tambwe Hiza
CHADEMA Sumbawanga mjini imekanusha pia upotoshaji mwingine kuwa bw Shayo ameihama CHADEMA eti kwa sababu ya ukabila na udini, upotoshaji huo unajibainisha kuwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, viongozi wa madhehebu ya kikristo walijiingiza katika kampeni makanisani kwa kumpinga mgombea wa CCM bw AESHI kwa kuwa ni muumini wa kiislam, hoja hii inahitimishwa kwa kusema kuwa CHADEMA Sumbwanga ni chama cha wakristo, Hoja hii si sahihi na kwamba udini Sumbwanga mjini haupo kwa vyama vyote viwili yaani CCM na CHADEMA. Chachu ya udini Sumbawanga iliingizwa kwa wapiga kura katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka jana na viongozi wa kampeni wa CCM bw Matete( mwenyekiti CCM mkoa),bw Tungombe (katibu mwenezi wilaya), bw Aeshi (mgombea wa ubunge), na wengineo. Hali ilikuwa mbaya sana pale bw Aeshi mgombea wa ubunge CCM alipoishiwa sera kwa wapiga kura na kujinadi katika mikutano kadhaa ya hadhara yeye kama YESU, na kumwita Kikwete MUNGU na Madiwani ROHO MTAKATIFU, jambo hili lilionekana kama fedheha na dharau kubwa kwa wakristo, kanisa katoriki lilitoa onyo kali kwa bw Aeshi na kutoa ujumbe wa kuombwa msamaha kwa dharau hiyo, jambo ambalo halikuwezekana, hali iliendelea kuharibiwa zaidi pale bw Matete kutumia advantage ya yeye kusoma seminari na mapadre wa kikatoriki na kuwa karibu nao kwa muda na kutumia mikutano ya kampeni kuwaita mapadre wahuni na wazinzi na kuwa yeye anawafahamu vizuri. Kauli hizi alizipata mh Pinda na kuwaamuru wahusika waombe msamaha kwa makanisa, kwa bahati mbaya hawa kufanya hivyo. Mh Pinda aliamua mwenyewe kuja Sumbawanga kuongea na viongozi wa dini wa kikristo kadhaa na kuamua mwenyewe kuapanda jukwaani katika uwanja wa Rukwa high school na kueleza yote kwa kujaribu kumtetea bw Aeshi kwa kusema alikuwa alijaribu kuomba kura kwa kutumia mafiga matatu akajisahau akatamka YESU,MUNGU na ROHO MTAKATIFU, lakini Pinda alikiri kuwa ni kosa kubwa na hasa kwa Aeshi ambaye si dhehebu hilo, mwishowe mh Pinda aliomba msamaha kwa niaba ya CCM na wote waliohusika.Mh Pinda aliondoka, lakini bado wahusika hawakukoma na hadi sasa kama ilivyoelezwa na bw Shayo bado hoja hii iko katika kauli za viongozi wa CCM mkoa. CHADEMA Sumbawanga mjini inatamka kuwa haihusiki kwa hili la udini, CHADEMA iko imara na itaendelea kuwa imara zaidi Sumbawanga mjini. Naomba kuwasilisha wakuu.