Chadema should not apologize!


Du Du Du!!!
Mkuu MgSalon. that was a vitriolic and classic attack on a fellow JF Member.
No wonder your mighty pen has made a acid attack with an intent to downsize MMKJJ.
However lets agree on one thing,politics as politics, handles all matters on shifting sands, public opinion is what matters.
I never fail to put my stand clear, that I am a CCM member, though not a coconut!
That CCM has walloped CDM hands down, whether legally or not, is there for all to see and comment.

Wakuu siasa ni mchezo wa kuigiza na asiyelitambua hilo basi hajui anafanya nini.MMKJJ is very articulate in explaining his position in whatever political scenario.
What I take my hat off for him is his right sense of judging the shifting political sands and public opinion.
Lets face it, CDM had a good case for the Constitutional Reforms pressure that it mounted.
However now everything seems to be in shambles and there is no leadership of national credibility, we are left to hear of the squabbles within this party centering on Zitto and his cronies.
CDM lazima mkubali kuwa sasa hivi mnacheza mchezo ambao bado hamjauzoea as compared to CCM, and the public is taking note.
 


Acha personal attack za kijinga. MMM katoa hoja yake, wewe km hukubaliani nayo basi ijibu thread yake sio kumchana mtu. Ukijibu hoja jibu kama mwana JF kwa mtazamo wako na usijibu kama Kiongozi wa Chama.Think critically, think more than usual, acha jazba.
 
To be honest Mwanakijiji is right about one thing, CHADEMA hawa ni watu waku improvise to as they go along.. And when you support people like that, one thing is certain... uncertainty and in many occasions this is coupled with disappointment and disillusionment ...

But what the hell, maybe the man has multiple personality disorder and this entire thread is just him talking to himself, turns out JF is a psyc ward.. ROFLMAO!
 
mheshimiwa MGsalon naona hukuilewa topic ya Mwanakijiji kabisa. Ilikuwa ni sitire....yaani alikuwa anaonyesha kuwa, CHADEMA hawatakiwi kumkubali rais sasa baada ya kupita katika mambo yote haya yaliyotokea.

inakuwa haileti maana, kumkataa rais, kukataa matokeo, kutoka nje ya bunge, halafu mwishowe tunakubali....MMM anasema, kumtambua rais sasa hivi, ni sawa na kukubali kuwa mtazamo wa kwanza wa kuchakachuliwa ulikuwa ni kosa....na kama lilikuwa kosa na sasa wameamua kukubali, basi waombe na msamaha kabisa tujue moja.

Nadhani umemuelewa sasa!
 
..Mnamsakama bure Mwanakijiji. Labda kainzi kake kalipotea njia...badala ya kwenda kwenye kikao cha CDM kakaingia kwenye kikao cha akina Makamba.

Ile post yake kama ingekuwa kweli CDM wangekuja na habari ya kutambua matokeo na kumtambua Rais basi alikuwa yuko right kabisa. Lakini kwakuwa imekuwa ni kinyume chake, yeye mwenyewe MMM apime kama anapaswa kuomba radhi ama la. Yes, kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake kuhusu jambo lolote. lakini hana haki ya kupotosha!!!

Nina mnukuu Dr. Slaa kwenye Tanzania Daima la leo tar. 14, Desemba "Msimamo wa CMD wa kutomtambua rais Kikwete kuwa rais halali wa Tanzania haujabadilika"
 

Hivi mwanakijiji ni nani? Ni mtu au taasisi
 
Hivi mwanakijiji ni nani? Ni mtu au taasisi

Na mimi nashangaa. Ila sisi wa kuja hapa JF tunamjua kama EXTRA senior member. He has supporters at JF than any other person. Ila leo kaja na mpya. Yaani CDM kukubali yaishe hataki. We are peaceful people and as far as I am concerned that is what CDM stands for. Not violence!
 


I can understand but the alternative is absolutely unsafe path!
 
Jamani, mtu hana haki ya kubadili mawazo yake?
U want him to be static eeh, jamani!!
These chadema fanatics whose vision and reasoning are clouded!!
U are blindly in love with bwana zenu Slaa na Mbowe?!!!
 

Shida yangu karibu na uchaguzi mwjj alitutoa wasi wasi kabisa kuwa wizi hauwezekani kwa jinsi mfumo wa upigaji wa kura ulivyo. Lakini baadaye tumejionea mambo tofauti kabisa. Mimi nikaandika humu kumuomba kwanza atuombe radhi maana alitupa matumaini ya uongo. Ukweli ni kuwa wizi ulikuwepo. Sasa sijui antetea lipi, wizi ulikuwepo au haukuwepo?

 

kwa hiyo hapa kuna mtumwa wa mbowe na mtumwa wa mwanakijiji, kazi kweli kweli, haya na mtumwa wa zitto kabwe tunamngoja ajitokeze, bila kuwasahau watumwa wa mkwele. Yangu macho.
 
am among those who believed mkuu mzee mwanakijiji is among few great thinkers who believe in the liberal and democratic modus operandi of governing this country. i was so astonished as a great thinker to learn that the honoured mkuu is a believe in the party disciplinary procedures!
 
jamani, mtu hana haki ya kubadili mawazo yake?
U want him to be static eeh, jamani!!
These chadema fanatics whose vision and reasoning are clouded!!
U are blindly in love with bwana zenu slaa na mbowe?!!!


na wewe bwana wako makamba na mkwere? Ficha upumbavu wako, usifiche hekima yako.
 
ZeMarcopolo,
Narudia tena, hakuna mahali popote Chadema imebadili msimamo wake na kusema kuwa Kura hazijaibiwa au kuchakachuliwa. Taarifa niliyotoa jana kwa TBC ilieleza wazi kuwa Kamati Kuu, ilipokea na kujadili na kuridhia mapendekezo yote yaliyowasilishwa na Sekretariat ya Chama kuwa Chadema imekataa matokeo ya Uchaguzi kutokana na irregularities 15. Chadema inaamini kuwa iwapo Katiba ya nchi isingelikuwa imezuia kuhoji matokeo ya uchaguzi Mkuu wa Rais mahakamani, matokeo hayo yangeliweza kubatilishwa. Kwa vile Katiba inakataza kuhoji matokeo kuhojiwa mahakamani, basi japo Kikwete's Presidency ni Lawful it is Illegitimate. Chadema ilitumia maneno ya kiingereza kuonyesha tofuati kubwa kati ya maneno hayo mawili. Huo ndio msimamo wa Chadema toka mwanzo na haijawahi kuyumba, japo maneno ya kiswahili yamekuwa yakipewa tafsiri tofauti na watu mbalimbali. Ni kwa msingi huo, Kamati Kuu ikasisitiza " Kuundwa kwa Tume Huru" kuchunguza Dosari " Irregularities" hizo kubwa katika uchaguzi. Nasisitiza, Chadema ni Chama ambacho toka mwanzo ilisisitiza kuwa "Haiko Tayari kuingia Ikulu kwa kumwaga Damu ya Watanzania". Inawezekana wanaopenda na kufurahia vurugu, Chadema haiko tayari kwa hali hiyo. Tunasukumwa sana na wapenzi na wanachame wetu kutoka mitaani na kuandamana, na ndicho pia wanachotaka ndugu zetu akina Mwanakijiji. Maandamano, (ya amani au ya kushinikiza), kwa watu wanaojua mchakato wa demokrasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kushindikana. Pili, ili Tanzania isiingie katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kwa Katiba na Sheria mbovu kama tuliyonayo leo, Chadema inasisitiza upatikanaji wa Katiba mpya, Shirikishi na ya Wananchi.Upatakanaji wa Katiba hii utakuwa na mchakato, na kama Serikali haitaki, basi Chadema kwa kushirikiana na wadau na watu mbalimbali wakiwemo wananchi itatutumia njia zote zinazoweza kuipatia nchi Katiba ya Wananchi. Yote haya ni mchakato, na kwa mtu yeyote anayoamini kuwa mchakato huchukua muda, basi atakuwa mvumilivu. Hakuna sababu ya kutumia lugha kali, kukashifiana na kutukanana japo jamvi letu ni mahali ambapo "we dare to speak". Tukivumiliana na kuheshimiana tutafika salama bandarini. Tukikurupuka tunaweza pia tusifikie lengo tunalotaka. Hekima na busara vikitawala na kuongoza matunda yatakuwa mazuri kwa Taifa letu. Taifa ni letu tukiibomoa hatuna pengine pa kwenda, labda tukiamua kulowea penginepo. Tukikurupuka tunaweza kuwaumiza wanaohusika na wasiohusika. Uvumilivu na Busara daima huvuta heri.
 
Duh Kidhungu kinatugonga! Hadi aibu ukisoma wabongo wanapochangia kwa kimombo, too many misplaced words!
Wengi tunavunja kwani siye siyo native speakers... wewe pia sidhani kama uko fluent kivile. Kizungu ni lugha ya tatu kama siyo ya nne kwa wengi wetu.
 
E bana eehh!! Ivo weye una akili zakwako au za kuazima? Kwanini huyu mzee ni nani kwako? Ukifuata mtu kwa hiari kisha ukapotea unalaumu?
 
Wajameni someni article ya MM vizuri mtaelewa ana maana gani sio mnakurupuka tu na kutoa majibu. Mwanzisha mada 'go read the article very carefully take ur time no rush then fikia suluhisho.' I bet mtazamo wako utakuwa tofauti na unavyofikiri sasa.
 
Dr. Slaa umesema "crystal clear". Hakuna nyongeza.
Haya Mwanakijiji et al mjitokeze hapa haraka na kuomba radhi.
 

Dr. Slaa umesema vyema kabisa na binafsi naamini huo ndio msimamo sahihi wa kidhamira na kisiasa. Hauna utata. Lakini, hadi hivi sasa hamjaenda kwa wananchi waliowaomba kura na kuwaambia msimamo huu. Mmeacha vyombo vya habari viutafssiri kwa wananchi. Mwezi mmoja na nusu baada ya uchaguzi bado hamjaweza kwenda kukutana na wananchi kama uongozi mzima wa taifa au wewe kama mgombea wao uliyebeba matumaini yao kwenda na kukutana nao na kuzungumza nao na kuwaambia nnini msimamo wa chama.

Lakini, msimamo wa kusema "ni illegitimate presidency" ni msimamo ambao CCM watawalazimisha wabunge wa Chadema kubadili ili wasema kuwa ni legitimate president kwa sababu "kachaguliwa" na "katangazwa"; je uongozi mzima wa CHadema unakubaliana kuwa ni illegitimate presidency? Je viongozi wengine wa Chadema wako tayari kutake that public position?

Ndio maana hoja ya ngu ya "Chadema must apologize" msingi wake ni kuhama katika hii position ambayo umeiarticulate hapa. Mkihama tu hapa ni lazima msamaha uje. Thats what I'm saying. Lakini, ni muhimu zaidi kwa nyinyi viongozi ( siyo mmoja mmoja) kukutana na wananchi na kuufafanua huu msimamo ili wananchii nao wajue msimamo huu wauelewe na bila ya shaka waufanye kuwa ni msimamo wao vile vile.

Nashukuru kwa ufafanuzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…