CHADEMA, nini sasa kwenda mbele?

CHADEMA, nini sasa kwenda mbele?

The good thing is "jamaa sasa hivi anatembea na AC, kwa hiyo 2 years to come hatoboi"
 
Tunasubiri utujengee shule, ulituahidi kabla hujaenda kuwa Yaya huko canada
Utasubiri! Ili nikunufaishe wewe or! Mimi siyo yaya kenge wewe.
 
Eti viongozi wasomi! Huko ccm mnaongozwa na wasomi wepi? Au hao madokta na majaji waliosombwa kuiba kura ndio wasomi? Au kina Bashiru wasioweza kuyaishi maneno na mafundisho waliyokuwa wanawafundisha watoto wetu?

Kwa taarifa yako na wengine wenye uelewa wa aina yako, Mbowe haendi kokote, he is there to stay ili akiongoze chama! Haya ni mapito na yapo ili chama na wanachama waimarike kiitikadi. Hakuna Cha viti maalumu Wala maridhiano Bali mapambano juu ya haki na usawa na demokrasia.

Mbowe na safu take ya uongozi pamoja na wanachama wa cdm wapo imara kuliko wakati mwingine wowote! Na dunia mzima wanajua upuuzi wa ccm na serikali yake ndio maana mnaweweseka baada ya kuona mmefanya utopolo! CDM haitetereki ipo imara!
 
Basi na hivyo vikwazo vije tuone kama ni kweli hatutaathirika!Wakisema tu tujinunulie ARV wenyewe tutatafutana!Huyo China ambaye tunajidai naye yeye anachangia kiduchu sana kwenye bajeti yetu tegemezi!EU na US wakisema wakate mrija basi ujue bajeti itakuwa na hali ngumu kutekelezeka ukizingatia mikopo mikubwa mikubwa tuliyonayo ambayo kila mwaka tunatenga fungu kulipa!
Vikwazo vikifanya hali ya watu kuwa mbaya huenda serikali ikajirudi na kuacha demokrasia itamalaki!Na hapo ndipo upinzani utanufaika kwa haki kutendeka kwenye chaguzi na utekelezaji wa majukumu yao ya kisiasa!
Kwa unavyojua wewe, tangu Magu aingie mpaka leo ni kiasi gani cha bajeti ya serikali inachangiwa na wafadhili???
 
Na nadhani kama tutawekewa vikwazo basi na iwe hivyo ili wote tuumie pengine akili zitaturudi na kuwa watu!.
 
Hiyo ni ahadi wanatoa.

Katika hiyo ahadi yao ya 40%, ni kiasi gani hasa wamempa Magu unavyofikiria????

Unafikiri jeuri ya Magu ya kusema kila anapofanya jambo ni kwa pesa zetu wenyewe ni nini????
 
Hiyo ni ahadi wanatoa.

Katika hiyo ahadi yao ya 40%, ni kiasi gani hasa wamempa Magu unavyofikiria????

Unafikiri jeuri ya Magu ya kusema kila anapofanya jambo ni kwa pesa zetu wenyewe ni nini????
Huwa anawadanganya huyo Magu!Husomi hata alama za nyakati?Wewe unadhani kwanini waziri wa mambo ya nje kateuliwa mapema?Hujui Magu anapenda sifa majukwaani huku nyuma pazia anatuma wasaidizi wake kuweka mambo sawa?

World bank na IMF walipogoma kutoa pesa kisa sheria ya Takwimu iliyokuwa imepitishwa na bunge baada ya serikali kupeleka muswada,kwanini serikali ya Magufuli ikaurudisha Muswada bungeni kufanya marekebisho ili isikose pesa za World bank na IMF?Kama JPM ana jeuri kwanini alitii masharti na kurudisha Muswada?

Fikirieni sio mnaandika tu,hao jamaa wakisema tuanze kujitegemea kununua ARV,hali itakuwaje?Mnajua gharama za hizo dawa?
 
Waanze kwa kuomba radhi wananchi walivyotengeneza makaratasi feki ya kura na kuzitumia kufanya hadaa eti wamekamata kura feki. .
 
Kwa maelezo uliyotoa hapa, najiuliza hasa umuhimu wa CHADEMA utakuwa upi kwetu sisi wananchi na hata kwa serikali? CHADEMA isiyoweza kushindana kwa lengo la kuibadili CCM madarakani haitakuwa na maana yoyote kwetu. Ni heri ing’atuke tu.

Halafu, umesifu harakati za Mwembe Yanga. Sijui kama umejiuliza kuwa lugha aliyotumia Dr. Slaa kumuelezea Kikwete na serikali yake wakati ule ingechukuliwaje ingekuwa katika utawala huu wa JPM? Elewa kuwa ile CHADEMA iliyokukosha wakati ule iliyokuwa na jeuri ya kuchapisha orodha ya mafisadi akiwemo Rais kama kiongozi wa mafisadi papa iliwezekana wakati ule. Leo hii Mchapishe JPM kivile halafu umtangaze pale Mwembe Yanga kama fisadi uone upepo utakavyokuvumia.

Uko sahihi kwa kiasi fulani kwamba CHADEMA “ile” ndiyo iliyochagiza ujio wa Magufuli CCM. Na Magufuli sio mjinga kuachia ile CHADEMA iendelee na mambo yake. Moto wake anaujua. Ile kushika hatamu tu, kapiga marufuku “siasa huria”, maandamano, Bunge live na kudhibiti media zote kutangaza habari za upinzani huku yeye akifanywa newsmaker mkuu. Kajaza polisi wa kufuatilia mazungumzo ya watu n.k.

Kwa kifupi ni kuwa Magufuli haitaki kabisa CHADEMA “iliyofanikisha” ujio wake madarakani. Kwake, “vyama rafiki” ni km UDP, TLP, UMD na NRA. Naona maelezo yako hapa yakizingatiwa na Mbowe kikamilifu, basi CHADEMA itatimiza sifa zote za kuwa “chama rafiki” kwa CCM.

Kwa vile tayari tuna vyama rafiki vya kutosha na Magufuli tayari yupo anatekeleza ajenda/ilani zote kama unavyodai na hatuna gerentii kwamba “vichaa” ndani ya CHADEMA watatulia, itakuwa vyema ukishauri CHADEMA kianze mchakato wa kujifuta (disband). Kimeshakamilisha umuhimu wake. Kama huo SIO mtizamo wako ni bora utuelimishe kama kuna kitu cha kipekee CHADEMA kinaweza kufanya tofauti na vyama vingine vilivyopo.
 
Hakuna kitu kinachowauma CCM kama Kukosa $900m ..na CDM wamekaza
 
Back
Top Bottom