Mwamba ana mzigo mzito kipindi hiki. Anatakiwa afanye maamuzi magumu ambayo yatakuwa kufa au kupona kwa Chadema.
Wakubali, wakatae, huu uchaguzi umekwisha na hakuna vikwazo wala matamko ya wazungu yanayoweza kubadili matokeo. Na hakuna mzungu yeyote anayeweza kutuporomeshea mabomu kila Chadema au Lissu. Hatuna kitu muhimu chakutosha, kufanya wazungu wakianzishe. Na Chadema wakifanikiwa kuwekea serikali vikwazo, watakao umia zaidi ni wananchi ambao Chadema itarudi kuwaomba kura.
Ukweli ni kuwa Chadema ilituvutia wengi sana enzi zile za Mwembe Yanga, na ni ile Chadema ndo ilikuwa chagizo kutufikisha hapa tulipo. Kutuletea Magu.
Kwahiyo kwa wanaojinasibu na utendaji wa Magu (ambao kiukweli amejitahidi kutekeleza ilani yao iliyopita), wasisahau kuwa utedaji huo uliuchagizwa na Chadema ya Mwembe Yanga.
Nini sasa hatma ya hiki chama, kilichoikomboa Tanzania toka mikononi mwa wanaccm wachache?
Maamuzi ya Mbowe ya sasa, yatakuwa na umuhimu mkubwa sana kwa hatma ya Chadema kama chama cha siasa zenye ushawishi nchini.
Ushauri wangu:
1.) Aruhusu akina mama waende bungeni kupitia viti maalum ili sera zao zipate nafasi ya kusikika kwa hii miaka 5. Wakipotea kabisa hewani, itawabidi
2025 waanze kujinadi upya. Wachaguwe tu wanawake makini. Sio wakwenda kufanya fujo. Iwe kwamba, wakisimama kuongea, wasikilizaji tubaki tunaongelea hoja waliyoitoa na sio wao kama personality.
Isitoshe, Chadema inahitaji hiyo ruzuku ili iendelee kujiendesha. Haiwezi kutegemea misaada ya wazungu tu 100%. Isitoshe inasemekana wafadhili wenyewe
wameaminishwa na Lissu, pesa yao haiko salama ikipelekwa kwenye chama moja kwa moja, ni lazima ipitie kwake. Sasa uendeshaji wa chama kwa kusubiri allowance
toka Ubelgiji kwa TL, itakuwa shughuli, na Mwamba analijua hili.
2.) Uongozi mkuu wa Chadema ujiuzuru. Chadema inahitaji kuleta uongozi mpya, uliosoma ili ibadili aina ya siasa inazofanya. Na kutumia akina Boni kama
injini ya chama, haisaidii. Maana watakuwa wanaendelea kutumia nguvu na fujo badala ya akili.
Chadema inahitaji busara sana kwenye uongozi wake, na viongozi wanye nia nzuri na siasa za chama, sio manufaa yao binafsi.
Mwamba lazima awe na uhakika na madhumuni ya viongozi wanaomzunguka.(Ukiangalia movie ya Tundu Lissu kwenye huu uchaguzi, ni kana kwamba
Chadema ilikuwa inafanya kazi kutimiza malengo ya Lissu, na sio Lissu, kufanya kazi kutimiza malengo ya Chadema).
3.) Mbowe aendelee kumtilia shaka Zitto Zuberi Kabwe. Mbowe hajawahi kumuamini Zitto tangu amfukuze kwenye chama chake, na asitegemee kuwa Zitto yule amebadilika.
4.) Mwamba kama mtu mzima, akubali yaishe. Nilishawahi kushauri hili huko nyuma kabla ya uchaguzi. Ile kauli ya Mwamba ya 2016 kuwa Jiwe watamchinjia baharini, ilimkera
mlengwa na alishasema hivyo wazi. Alisema hawezi kukaa na mtu aliyesema wakamchinjie baharini.
Namsihi aombe kuonana na mkulu kwa njia yakusema wanataka maridhiano, aombe radhi kiutu uzima yaishe.
Sote tunamjua Mkulu alivyo kiburi. Mwenye akili timamu asitegemee mkulu ndo awaite kutafuta maridhiano nao. Wahenga wanasema, mkubwa hakosei. Sasa huyu tumtake, tusimtake
ndo mkuu kwa sasa. Chadema hawawezi shinda vita ya NANI ZAIDI?!!
Wakubali yaishe, ili waanze kukijenga chama chao upya.
5.) Chadema ichukuwe tahadhari na hawa washauri wao ambao ni wanaharakati na celebrities wa mitandaoni. Wajiulize nini malengo yao? Wengi wao, harakati zao za mitandaoni
ndo zinazowaweka mjini. Hata yule dada mwenye mdomo mchafu, matusi ndo yanayompa traffic, traffic ya clicks ndo inampa kula. Sio kwamba anafanya afanyavyo sababu ya
mapenzi yake kwa Chadema. Wengine chuki zao kwa CCM ni zakulazimisha ili waendelee kuwepo mjini.
Je, Chadema inataka kujihusisha na watu wa aina gani? Na mambo ya aina gani?
Kila lenye heri kwa Chama hiki Muhimu nchini ✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿
Wakubali, wakatae, huu uchaguzi umekwisha na hakuna vikwazo wala matamko ya wazungu yanayoweza kubadili matokeo. Na hakuna mzungu yeyote anayeweza kutuporomeshea mabomu kila Chadema au Lissu. Hatuna kitu muhimu chakutosha, kufanya wazungu wakianzishe. Na Chadema wakifanikiwa kuwekea serikali vikwazo, watakao umia zaidi ni wananchi ambao Chadema itarudi kuwaomba kura.
Ukweli ni kuwa Chadema ilituvutia wengi sana enzi zile za Mwembe Yanga, na ni ile Chadema ndo ilikuwa chagizo kutufikisha hapa tulipo. Kutuletea Magu.
Kwahiyo kwa wanaojinasibu na utendaji wa Magu (ambao kiukweli amejitahidi kutekeleza ilani yao iliyopita), wasisahau kuwa utedaji huo uliuchagizwa na Chadema ya Mwembe Yanga.
Nini sasa hatma ya hiki chama, kilichoikomboa Tanzania toka mikononi mwa wanaccm wachache?
Maamuzi ya Mbowe ya sasa, yatakuwa na umuhimu mkubwa sana kwa hatma ya Chadema kama chama cha siasa zenye ushawishi nchini.
Ushauri wangu:
1.) Aruhusu akina mama waende bungeni kupitia viti maalum ili sera zao zipate nafasi ya kusikika kwa hii miaka 5. Wakipotea kabisa hewani, itawabidi
2025 waanze kujinadi upya. Wachaguwe tu wanawake makini. Sio wakwenda kufanya fujo. Iwe kwamba, wakisimama kuongea, wasikilizaji tubaki tunaongelea hoja waliyoitoa na sio wao kama personality.
Isitoshe, Chadema inahitaji hiyo ruzuku ili iendelee kujiendesha. Haiwezi kutegemea misaada ya wazungu tu 100%. Isitoshe inasemekana wafadhili wenyewe
wameaminishwa na Lissu, pesa yao haiko salama ikipelekwa kwenye chama moja kwa moja, ni lazima ipitie kwake. Sasa uendeshaji wa chama kwa kusubiri allowance
toka Ubelgiji kwa TL, itakuwa shughuli, na Mwamba analijua hili.
2.) Uongozi mkuu wa Chadema ujiuzuru. Chadema inahitaji kuleta uongozi mpya, uliosoma ili ibadili aina ya siasa inazofanya. Na kutumia akina Boni kama
injini ya chama, haisaidii. Maana watakuwa wanaendelea kutumia nguvu na fujo badala ya akili.
Chadema inahitaji busara sana kwenye uongozi wake, na viongozi wanye nia nzuri na siasa za chama, sio manufaa yao binafsi.
Mwamba lazima awe na uhakika na madhumuni ya viongozi wanaomzunguka.(Ukiangalia movie ya Tundu Lissu kwenye huu uchaguzi, ni kana kwamba
Chadema ilikuwa inafanya kazi kutimiza malengo ya Lissu, na sio Lissu, kufanya kazi kutimiza malengo ya Chadema).
3.) Mbowe aendelee kumtilia shaka Zitto Zuberi Kabwe. Mbowe hajawahi kumuamini Zitto tangu amfukuze kwenye chama chake, na asitegemee kuwa Zitto yule amebadilika.
4.) Mwamba kama mtu mzima, akubali yaishe. Nilishawahi kushauri hili huko nyuma kabla ya uchaguzi. Ile kauli ya Mwamba ya 2016 kuwa Jiwe watamchinjia baharini, ilimkera
mlengwa na alishasema hivyo wazi. Alisema hawezi kukaa na mtu aliyesema wakamchinjie baharini.
Namsihi aombe kuonana na mkulu kwa njia yakusema wanataka maridhiano, aombe radhi kiutu uzima yaishe.
Sote tunamjua Mkulu alivyo kiburi. Mwenye akili timamu asitegemee mkulu ndo awaite kutafuta maridhiano nao. Wahenga wanasema, mkubwa hakosei. Sasa huyu tumtake, tusimtake
ndo mkuu kwa sasa. Chadema hawawezi shinda vita ya NANI ZAIDI?!!
Wakubali yaishe, ili waanze kukijenga chama chao upya.
5.) Chadema ichukuwe tahadhari na hawa washauri wao ambao ni wanaharakati na celebrities wa mitandaoni. Wajiulize nini malengo yao? Wengi wao, harakati zao za mitandaoni
ndo zinazowaweka mjini. Hata yule dada mwenye mdomo mchafu, matusi ndo yanayompa traffic, traffic ya clicks ndo inampa kula. Sio kwamba anafanya afanyavyo sababu ya
mapenzi yake kwa Chadema. Wengine chuki zao kwa CCM ni zakulazimisha ili waendelee kuwepo mjini.
Je, Chadema inataka kujihusisha na watu wa aina gani? Na mambo ya aina gani?
Kila lenye heri kwa Chama hiki Muhimu nchini ✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿✌🏿