Zee la kitaa
JF-Expert Member
- Oct 25, 2017
- 403
- 211
Chadema kama chama kikuu cha upinzani kimeonyesha udhaifu na upungufu mkubwa kiuongozi. Ni chama ambacho kimeshindwa kutatua changamoto za uongozi na kuleta porojo kila kukicha.
Kuanzia ajenda za kununuliwa wanachama wao inaonyesha hiki chama ni kichanga sana katika siasa. Hivi kweli chama na viongozi wa chama kikuu cha upinzani katika taifa kinasimama na kusema eti wanachama wake wananunuliwa huku wale wanaotoka vyama vingine kuingia chadema wakiitwa mashujaa. Huu upuuzi gani; halafu chama kinajinadi kuwa chama cha demokrasia. Kwanza ni aibu kwa chama kushindwa kusimamia viongozi wake hadi wakanunuliwa; pili ni aibu kufika hadharani kusema wanachama wako kununuliwa kwa porojo za kuungaunga bila Evidence. Chadema wameshindwa kusimamia demokrasia na uwazi katika chama chao wamebaki na ramri na kuitana majina. Hiki chama kinaendelea kupoteza imani kwa wananchi na aibu kubwa itakuwa kipigo cha mbwa mwitu katika chaguzi za marudio zinazoendelea.
Naomba kuwasilisha.
Kuanzia ajenda za kununuliwa wanachama wao inaonyesha hiki chama ni kichanga sana katika siasa. Hivi kweli chama na viongozi wa chama kikuu cha upinzani katika taifa kinasimama na kusema eti wanachama wake wananunuliwa huku wale wanaotoka vyama vingine kuingia chadema wakiitwa mashujaa. Huu upuuzi gani; halafu chama kinajinadi kuwa chama cha demokrasia. Kwanza ni aibu kwa chama kushindwa kusimamia viongozi wake hadi wakanunuliwa; pili ni aibu kufika hadharani kusema wanachama wako kununuliwa kwa porojo za kuungaunga bila Evidence. Chadema wameshindwa kusimamia demokrasia na uwazi katika chama chao wamebaki na ramri na kuitana majina. Hiki chama kinaendelea kupoteza imani kwa wananchi na aibu kubwa itakuwa kipigo cha mbwa mwitu katika chaguzi za marudio zinazoendelea.
Naomba kuwasilisha.