Chama kinachojinadi ni mbadala kina viongozi wanaonunuliwa Mwenyekiti ana tuhuma za kuhongwa bilioni 5 ili kumpokea mtu waliyesema ni fisadi,chama hiko hiko kinachosema kinawakomboa watanzania katibu wake mkuu anashutumiwa kununuliwa na CCM leo madiwani wake wanashutumiwa kununuliwa na CCM hiki ni chama au viongozi wao ni bidhaa?
Hivi unajua kwanini Halmsahuri zetu zinanuka RUSHWA na UFISADI??Umeshajiuliza hata siku moja??Umejiuliza ni kwanini miaka 55 hakuna Halmsahuri yenye HATI safi,na kama ipo basi RUSHWA kubwa imetumika unalijua hili??Ukishalijua hili basi usiwe unakubali kila kitu unachoambiwa.Sasa nakupa shule ndogo tu uitafakari nategemea tutaelewana:
1.Madiwani/Wenyeviti wa mitaa ndiyo wanaofanya kazi kubwa sana kwenye maeneo yetu kuliko Wakuu wa mikoa/Wilaya na Wabunge.
2.Hawa wote ndiyo ambao hawalipwi posho wala mishahara
3.Wengi wao ni darasa la sababu au kidato cha nne na wapo basi ni wachache sana ambao wamemaliza chuo kikuu na kuna wengine hata KUSOMA,KUANDIKA na KUHESABU ni shida hawa ndiyo tunawapa wasimamie serikali zetu za mtaa au halmashauri.
Tanzania yetu hasa mikoani/wilayani na kwenye Halmashauri zetu tunategemea kupata maendeleo kutoka kwao,hawa ambao Wakurugenzi,Wakuu wa WIlaya na Wakuu wa Mkoa wanawapa pesa kidogo tu ili kufanikisha madeal yao.Unategemea huyu akipewa milioni tano na kiinua mgongo cha mil11 akatae,sidhani kama ni rahisi si kwa CCM wala Chadema.
Tunachotakiwa ni kuwapigia debe hawa walipwe kama walipwavyo wabunge hata wapewe 1.5M kwa mwezi Rushwa na Ufisadi kwenye Halmashauri zetu zitakuwa hadithi.
Waweke Sheria kwamba Diwani lazima awe ana atleast cheti cha ufaulu kidato cha sita,tukianza huku lazima tutapaa kimaendeleo,vinginevyo ukichanganya na KKK za wakuu wa mikoa na wilaya tutasota sana.
SIkubaliani na anayepokea wala anayetoa RUSHWA,na Rushwa si chama ni watu binafsi.Siichukii CCM na wachukia wachumia tumbo wote walioko ndani ya CCM pamoja na wale wote wanaowasupport upumbavu huu.
Nilitegemea upige vita wote hawa waliopokea na waliotoa wote ni wakufunga tu hakuna msafi hapo,hivyo usiwalaumu waliojua kwamba ahwa wamepewa RUSHWA.
Mkuu ukila EMBE MBICHI meno yako ndiyo yatakayokuwa na GANZI na si ya mwanao.Kikubwa tupige vita RUSHWA period