Lobapula
JF-Expert Member
- Jun 19, 2011
- 2,391
- 1,586
Hivi karibunii kumekuwepo na shutuma za madiwa wa CHADEMA kunuliwa na viongozi kutoka CCM.Shutuma hizo tulianza kuziskia katika vyombo vya habari ambapo Mchungaji Peter Msingwa alilalamika kuwa madiwani huko Iringa wana nunuliwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi.
Wiki iliyopita pia tumeona Wabunge Lema wa Arusha na Joshua Nassar wakilalamika na kumshutum mmoja wa wakuu wa wilaya akihusishwa na njama za kununyua madiwani wa CHADEMA ili waende CCM.
Swali kubwa wana bodi hapa ni kujiuliza kama tunakua na madiwani kwenye Chama Chetu ambao wana endekeza njaa mpaka kununuliwa tuna viongozi wa aina gani?
Kama mwaka 2015 tulijinadi sisi CHADEMA ndio tunaleta mabadiliko leo hii madiwani na viongozi wetu wana nunuliwa hadharani tulitegemea mabadiliko ya namna ganii?
Kama madiwani wa CHADEMA ambao hawa ndio wamiliki wa halmashauri wana nunuliwa kwa kuendekeza njaa je ngazi za vijiji NA WENYEVITI WA VITONGOJI HALI IKOJE?
HISTORIA YA KUNUNULIWA
Zitto Zuber Kabwe aliwahi kumtuhumu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa kuwa alihonmgwa na Nimrodi Mkono hivyo akaacha kupiga kampeni katika jimbo la Musoma vijijini na haikuishia hapo tu Gazeti la Raia Tanzania liliwahi kuandika Mbowe na Mtei wamehongwa Bilioni 5 ili kumpitisha Lowasa kugombea urais kupitia CHADEMA na kwa shutuma hizo sio Mbowe wala Mtei waliokanusha wala kufungua kesi ya kudhalilishwa na gazeti hilo.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Slaa mpaka leo anashutumiwa kuwa alihongwa na kununuliwa na CCM ndio maana akakikimbia chama kipindi cha uchaguzi.
Sasa tunapokua na chama ambacho Katibu Mkuu anashutumiwa kununuliwa,Mwenyekiti anashutumiwa kuhongwa,madiwani wananunuliwa tuna chama cha aina gani?
Kama viongozi wa CHADEMA wananunuliwa je kuna tofauti gani ya ki maadili na CCM wanaowanunua?
Wiki iliyopita pia tumeona Wabunge Lema wa Arusha na Joshua Nassar wakilalamika na kumshutum mmoja wa wakuu wa wilaya akihusishwa na njama za kununyua madiwani wa CHADEMA ili waende CCM.
Swali kubwa wana bodi hapa ni kujiuliza kama tunakua na madiwani kwenye Chama Chetu ambao wana endekeza njaa mpaka kununuliwa tuna viongozi wa aina gani?
Kama mwaka 2015 tulijinadi sisi CHADEMA ndio tunaleta mabadiliko leo hii madiwani na viongozi wetu wana nunuliwa hadharani tulitegemea mabadiliko ya namna ganii?
Kama madiwani wa CHADEMA ambao hawa ndio wamiliki wa halmashauri wana nunuliwa kwa kuendekeza njaa je ngazi za vijiji NA WENYEVITI WA VITONGOJI HALI IKOJE?
HISTORIA YA KUNUNULIWA
Zitto Zuber Kabwe aliwahi kumtuhumu Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa kuwa alihonmgwa na Nimrodi Mkono hivyo akaacha kupiga kampeni katika jimbo la Musoma vijijini na haikuishia hapo tu Gazeti la Raia Tanzania liliwahi kuandika Mbowe na Mtei wamehongwa Bilioni 5 ili kumpitisha Lowasa kugombea urais kupitia CHADEMA na kwa shutuma hizo sio Mbowe wala Mtei waliokanusha wala kufungua kesi ya kudhalilishwa na gazeti hilo.
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Slaa mpaka leo anashutumiwa kuwa alihongwa na kununuliwa na CCM ndio maana akakikimbia chama kipindi cha uchaguzi.
Sasa tunapokua na chama ambacho Katibu Mkuu anashutumiwa kununuliwa,Mwenyekiti anashutumiwa kuhongwa,madiwani wananunuliwa tuna chama cha aina gani?
Kama viongozi wa CHADEMA wananunuliwa je kuna tofauti gani ya ki maadili na CCM wanaowanunua?